Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. * - Tippudi firooji ɗii


Firo maanaaji Aaya: (13) Simoore: Simoore koreeji imraan
قَدۡ كَانَ لَكُمۡ ءَايَةٞ فِي فِئَتَيۡنِ ٱلۡتَقَتَاۖ فِئَةٞ تُقَٰتِلُ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ وَأُخۡرَىٰ كَافِرَةٞ يَرَوۡنَهُم مِّثۡلَيۡهِمۡ رَأۡيَ ٱلۡعَيۡنِۚ وَٱللَّهُ يُؤَيِّدُ بِنَصۡرِهِۦ مَن يَشَآءُۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّأُوْلِي ٱلۡأَبۡصَٰرِ
Hakika yalikiwa kwenu, enyi Mayahudi wakaidi, ni ushuhuda mkubwa yale mapambano ya Badr yaliyotukia baina ya makundi mawili: kundi moja linapigana kwa ajili ya Dini ya Mwenyezi Mungu, nalo ni kundi la Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na Masahaba wake, na kundi lingine lenye kumkanusha Mwenyezi Mungu, linapigana kwa ajili ya batili. Ukiwatazama Waumini kwa macho utawaona kuwa ni mara mbili ya ile idadi yao. Na Mwenyezi Mungu Alilifanya hilo kuwa ni sababu ya ushindi wa Waislamu juu yao. Na Mwenyezi Mungu Anawasaidia kwa nusura Yake anaowataka katika waja Wake. Hakika katika tukio hili pana mazingatio makubwa kwa wenye busara ambao wanaongokea kujua hukumu zake na matendo Yake.
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Aaya: (13) Simoore: Simoore koreeji imraan
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. - Tippudi firooji ɗii

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo fayde e ɗemngal sawaahili, firi ɗum ko Doktoor Abdullaay Muhammad Abuubakri. E mawɗo Naasir Kamiis.

Uddude