Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. * - Tippudi firooji ɗii


Firo maanaaji Aaya: (4) Simoore: Simoore sujjannde
ٱللَّهُ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَا فِي سِتَّةِ أَيَّامٖ ثُمَّ ٱسۡتَوَىٰ عَلَى ٱلۡعَرۡشِۖ مَا لَكُم مِّن دُونِهِۦ مِن وَلِيّٖ وَلَا شَفِيعٍۚ أَفَلَا تَتَذَكَّرُونَ
Mwenyezi Mungu Ndiye Ambaye aliumba mbingu na ardhi na vilivyoko baina yake kwa Siku sita kwa hekima Anayoijua. Na Yeye ni Muweza wa kuziumba kwa neno «Kuwa» na likawa, kisha Akalingana, Kutakasika na kuwa juu ni Kwake - nako ni kuwa juu na kunyanyuka- juu ya ‘Arsh Yake , kulingana kunakonasibiana na utukufu Wake, hakusemwi kuko namna gani wala hakufananishwi na vile binadamu wanavyolingana. Hamna nyinyi, enyi watu, mtegemewa wa kumtegemezea mambo yenu, au muombezi wa kuwaombea nyinyi mbele ya Mwenyezi Mungu, ili muokoke na adhabu Yake. Basi kwani nyinyi hamwaidhiki na mkafikiria, enyi watu, mkampwekesha Mwenyezi Mungu kwa uungu na mkamtakasia ibada?
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Aaya: (4) Simoore: Simoore sujjannde
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. - Tippudi firooji ɗii

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo fayde e ɗemngal sawaahili, firi ɗum ko Doktoor Abdullaay Muhammad Abuubakri. E mawɗo Naasir Kamiis.

Uddude