Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. * - Tippudi firooji ɗii


Firo maanaaji Aaya: (75) Simoore: Simoore pellon
وَتَرَى ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ حَآفِّينَ مِنۡ حَوۡلِ ٱلۡعَرۡشِ يُسَبِّحُونَ بِحَمۡدِ رَبِّهِمۡۚ وَقُضِيَ بَيۡنَهُم بِٱلۡحَقِّۚ وَقِيلَ ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na utawaona Malaika, ewe Nabii, wameizunguka 'Arshi ya Mwingi wa rehema, wanamtakasa Mola wao na kumuepusha na kila kisichofaa kunasibishwa nacho, (na utaona kuwa) Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka Amehukumu baina ya viumbe kwa uhaki na uadilifu, Akawakalisha wenye kuamini Peponi na wenye kukufuru Motoni. Na hapo kutasemwa, «Shukrani zote ni za Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe wote kwa uamuzi Aliyoutoa baina ya watu wa Peponi na Motoni, shukrani ya kutambua wema na hisani na shukrani ya kutambua uadilifu na hekima.»
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Aaya: (75) Simoore: Simoore pellon
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. - Tippudi firooji ɗii

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo fayde e ɗemngal sawaahili, firi ɗum ko Doktoor Abdullaay Muhammad Abuubakri. E mawɗo Naasir Kamiis.

Uddude