Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. * - Tippudi firooji ɗii


Firo maanaaji Aaya: (12) Simoore: Simoore rewɓe
۞ وَلَكُمۡ نِصۡفُ مَا تَرَكَ أَزۡوَٰجُكُمۡ إِن لَّمۡ يَكُن لَّهُنَّ وَلَدٞۚ فَإِن كَانَ لَهُنَّ وَلَدٞ فَلَكُمُ ٱلرُّبُعُ مِمَّا تَرَكۡنَۚ مِنۢ بَعۡدِ وَصِيَّةٖ يُوصِينَ بِهَآ أَوۡ دَيۡنٖۚ وَلَهُنَّ ٱلرُّبُعُ مِمَّا تَرَكۡتُمۡ إِن لَّمۡ يَكُن لَّكُمۡ وَلَدٞۚ فَإِن كَانَ لَكُمۡ وَلَدٞ فَلَهُنَّ ٱلثُّمُنُ مِمَّا تَرَكۡتُمۚ مِّنۢ بَعۡدِ وَصِيَّةٖ تُوصُونَ بِهَآ أَوۡ دَيۡنٖۗ وَإِن كَانَ رَجُلٞ يُورَثُ كَلَٰلَةً أَوِ ٱمۡرَأَةٞ وَلَهُۥٓ أَخٌ أَوۡ أُخۡتٞ فَلِكُلِّ وَٰحِدٖ مِّنۡهُمَا ٱلسُّدُسُۚ فَإِن كَانُوٓاْ أَكۡثَرَ مِن ذَٰلِكَ فَهُمۡ شُرَكَآءُ فِي ٱلثُّلُثِۚ مِنۢ بَعۡدِ وَصِيَّةٖ يُوصَىٰ بِهَآ أَوۡ دَيۡنٍ غَيۡرَ مُضَآرّٖۚ وَصِيَّةٗ مِّنَ ٱللَّهِۗ وَٱللَّهُ عَلِيمٌ حَلِيمٞ
Na nyinyi, enyi wanaume, muna nusu ya kilioachwa na wake zenu baada ya kufa kwao, iwapo hawana watoto wa kiume au wa kike, na ikiwa wana watoto, basi mtapata robo ya walichokiacha ambacho mtakirithi baada ya kutekeleza wasia wao unaofaa au baada ya kulipa deni lao kwa wastahiki. Na wake zenu, enyi waume, watapata robo ya mlichokiacha iwapo hamuna mwana wa kiume au wa kike kutoka kwao, hao wake zenu, au wengineo mliokuwa mumewaoa. Na iwapo mtakuwa na mwana wa kiume au wa kike, basi hao wake zenu watapata thumni ya mlichokiacha. Hiyo robo au thumni itagawanywa kati yao; na iwapo ni mke mmoja, basi hiyo robo au thumni itakuwa ndio fungu lake. Hii ni baada ya kutekeleza kile mlichousia kitekelezwe katika nyasia zifaazo, au kulipa deni lenu. Na iwapo mwanamume au mwanamke atakufa, na akawa hana mwana wala mzazi, na akawa na ndugu mmoja wa kwa mama, wa kiume au wa kike, basi kila mmoja kati yao wawili atapata sudusi; wakiwa ni zaidi ya mmoja watashirikiana katika theluthi itakayogawanywa baina yao kwa usawa bila kutafautisha baina ya mwanamume na mwanamke. Hili ndilo fungu Alilowaekea Mwenyezi Mungu ndugu wa kwa mama, wa kiume na wa kike, likiwa ni urithi wao, baada ya kutekeleza wasia wa aliyekufa iwapo aliusia chochote ambacho hakina madhara kwa mawarithi au baada ya kulipa madeni yake. Kwa hili Amewausia Mola wenu, wasia wenye manufaa kwenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi mno kwa yanayowafaa viumbe Wake, ni Mpole, Hana haraka ya kuwaadhibu.
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Aaya: (12) Simoore: Simoore rewɓe
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. - Tippudi firooji ɗii

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo fayde e ɗemngal sawaahili, firi ɗum ko Doktoor Abdullaay Muhammad Abuubakri. E mawɗo Naasir Kamiis.

Uddude