Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. * - Tippudi firooji ɗii


Firo maanaaji Aaya: (24) Simoore: Simoore rewɓe
۞ وَٱلۡمُحۡصَنَٰتُ مِنَ ٱلنِّسَآءِ إِلَّا مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُكُمۡۖ كِتَٰبَ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡۚ وَأُحِلَّ لَكُم مَّا وَرَآءَ ذَٰلِكُمۡ أَن تَبۡتَغُواْ بِأَمۡوَٰلِكُم مُّحۡصِنِينَ غَيۡرَ مُسَٰفِحِينَۚ فَمَا ٱسۡتَمۡتَعۡتُم بِهِۦ مِنۡهُنَّ فَـَٔاتُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ فَرِيضَةٗۚ وَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ فِيمَا تَرَٰضَيۡتُم بِهِۦ مِنۢ بَعۡدِ ٱلۡفَرِيضَةِۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمٗا
Na ni haramu kwenu kuwaoa wanawake walioolewa, isipokuwa wale mliowateka katika jihadi. Hao ni halali kwenu kuwaoa baada ya kutakasika vizazi vyao kwa kipindi kimoja cha hedhi. Mwenyezi Mungu Amewaandikia uharamu wa kuwaoa hao, na Amewaruhusu kuwaoa wangineo, miongoni mwa wale Aliowahalalishia kuwataka kwa ndoa mkitumia pesa zenu kujihifadhi msitende haramu. Basi wale mliostarehe nao, miongoni mwao, kwa ndoa sahihi, wapeni mahari yao ambayo ni haki yao iliyolazimishwa na Mwenyezi Mungu juu yenu. Na si makosa kwenu, kwa makubaliano yaliyofikiwa baina yenu kwa kuridhiana, kupunguza au kuongeza kiwango cha mahari baada ya kuamuliwa kiwango chake. Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mambo ya waja Wake, ni Mwenye hekima katika hukumu zake na uendeshaji Wake.
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Aaya: (24) Simoore: Simoore rewɓe
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. - Tippudi firooji ɗii

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo fayde e ɗemngal sawaahili, firi ɗum ko Doktoor Abdullaay Muhammad Abuubakri. E mawɗo Naasir Kamiis.

Uddude