Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. * - Tippudi firooji ɗii


Firo maanaaji Aaya: (8) Simoore: Simoore jeddondiral
أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلَّذِينَ نُهُواْ عَنِ ٱلنَّجۡوَىٰ ثُمَّ يَعُودُونَ لِمَا نُهُواْ عَنۡهُ وَيَتَنَٰجَوۡنَ بِٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡعُدۡوَٰنِ وَمَعۡصِيَتِ ٱلرَّسُولِۖ وَإِذَا جَآءُوكَ حَيَّوۡكَ بِمَا لَمۡ يُحَيِّكَ بِهِ ٱللَّهُ وَيَقُولُونَ فِيٓ أَنفُسِهِمۡ لَوۡلَا يُعَذِّبُنَا ٱللَّهُ بِمَا نَقُولُۚ حَسۡبُهُمۡ جَهَنَّمُ يَصۡلَوۡنَهَاۖ فَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ
Je, huwaoni, ewe Mtume, Mayahudi waliokatazwa wasizungumze kwa siri maneno yanayowatia shaka Waumini, kisha wanarudi kufanya yale waliyokatazwa, na wanazungumza kwa siri maneno ya dhambi, uadui na kuenda kinyume na amri ya Mtume? Na wanapokujia hawa Mayahudi kwa jambo lolote miongoni mwa mambo, wanakuamkia kwa maamkizi ambayo siyo yale Mwenyezi Mungu Aliyoyafanya ni maamkizi yako, na wanasema, «As-sām ‘alayka» yaani, Mauti yakushukie! Na wanasema wakiambiana wao kwa wao, «Si Atuangamize Mwenyezi Mungu kwa yale tunayomuambia Muhammad, iwapo ni Mtume kikweli.» Moto wa Jahanamu utawatosha: wataungia na watalihisi joto lake, na ubaya wa marejeo ni huo.
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Aaya: (8) Simoore: Simoore jeddondiral
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. - Tippudi firooji ɗii

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo fayde e ɗemngal sawaahili, firi ɗum ko Doktoor Abdullaay Muhammad Abuubakri. E mawɗo Naasir Kamiis.

Uddude