Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. * - Tippudi firooji ɗii


Firo maanaaji Aaya: (3) Simoore: Simoore harminde (tahriim)
وَإِذۡ أَسَرَّ ٱلنَّبِيُّ إِلَىٰ بَعۡضِ أَزۡوَٰجِهِۦ حَدِيثٗا فَلَمَّا نَبَّأَتۡ بِهِۦ وَأَظۡهَرَهُ ٱللَّهُ عَلَيۡهِ عَرَّفَ بَعۡضَهُۥ وَأَعۡرَضَ عَنۢ بَعۡضٖۖ فَلَمَّا نَبَّأَهَا بِهِۦ قَالَتۡ مَنۡ أَنۢبَأَكَ هَٰذَاۖ قَالَ نَبَّأَنِيَ ٱلۡعَلِيمُ ٱلۡخَبِيرُ
Na pindi Mtume alipompa siri mke wake Hafsah, radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie, ya mazungumzo fulani, na yeye alipomwambia maneno hayo mke mwenzake 'Aishah, radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie, na Mwenyezi Mungu Akamjulisha Mtume Wake kuwa mkewe ameitoa siri yake, alimjulisha Hafsah sehemu ya maneno aliyoyatoa na akayanyamazia mengine asimwambie kwa kuchunga heshima. Basi Mtume alipomwambia Hafsah yale mazungumzo aliyoyatangaza, alisema huyo mke, «Ni nani aliyekwambia maneno hayo?» Akasema Mtume, «Aliyenambia hayo ni Mwenyezi Mungu, Aliye Mwingi wa ujuzi na utambuzi, Ambaye hakifichamani Kwake chenye kujificha chochote.
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Aaya: (3) Simoore: Simoore harminde (tahriim)
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo sawahiliiwo. - Abdullaay Muhammad e Naadir Kamiis. - Tippudi firooji ɗii

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo fayde e ɗemngal sawaahili, firi ɗum ko Doktoor Abdullaay Muhammad Abuubakri. E mawɗo Naasir Kamiis.

Uddude