Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo saawaahiliiwo - Ali Muhsin Al-barwaany * - Tippudi firooji ɗii

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Firo maanaaji Aaya: (125) Simoore: Simoore rewɓe
وَمَنۡ أَحۡسَنُ دِينٗا مِّمَّنۡ أَسۡلَمَ وَجۡهَهُۥ لِلَّهِ وَهُوَ مُحۡسِنٞ وَٱتَّبَعَ مِلَّةَ إِبۡرَٰهِيمَ حَنِيفٗاۗ وَٱتَّخَذَ ٱللَّهُ إِبۡرَٰهِيمَ خَلِيلٗا
Na nani aliye bora kwa dini kuliko yule aliye usilimisha uso wake kwa Mwenyezi Mungu, naye akawa mwema, na anafuata mila ya Ibrahim mwongofu? Na Mwenyezi Mungu alimfanya Ibrahim kuwa ni rafiki mwendani.
Msingi wa vitendo vyema ni itikadi iliyo sawa. Na bora ya dini ni kumtakasikia niya Mwenyezi Mungu Mtukufu, ukawa uso wako, na akili yako, na nafsi yako, yote haitaki kitu isipo kuwa kumridhi Mwenyezi Mungu Subhanahu. Kwa hivyo basi ndio fahamu zako zitanyooka sawa kuufahamu ujumbe wa Mitume, na ndio utaweza kushika daima vitendo vilivyo bora, na ukamfuata Baba wa Manabii, Ibrahim a.s. Kwani dini yake Ibrahim ndiyo Dini ya Mwenyezi Mungu, na ndiyo Dini inayo elekeza kutaka Haki daima. Na kwa Ibrahim ndiyo umekutana umoja wa Dini, kwa Waislamu, na Mayahudi na Wakristo. Basi ifuateni njia yake. Mwenyezi Mungu hakika amemkirimu Ibrahim, akamwita "Rafiki Mwendani".
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Aaya: (125) Simoore: Simoore rewɓe
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo saawaahiliiwo - Ali Muhsin Al-barwaany - Tippudi firooji ɗii

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo fayde e ɗemngal sawahili, firi ɗum ko Ali Muhsin Al-barwani

Uddude