Check out the new design

Traduction des sens du Noble Coran - La traduction swahili - 'Abd Allah Muhammad et Nâsir Khamîs * - Lexique des traductions


Traduction des sens Sourate: Al Ahzâb   Verset:
يَسۡـَٔلُكَ ٱلنَّاسُ عَنِ ٱلسَّاعَةِۖ قُلۡ إِنَّمَا عِلۡمُهَا عِندَ ٱللَّهِۚ وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّ ٱلسَّاعَةَ تَكُونُ قَرِيبًا
Wanakuuliza watu , ewe Mtume, kuhusu kipindi cha Kiyama kwa njia ya kukiona ni kitu ambacho ni mbali kutokea na kwa njia ya kukikanusha. Waambie, «Hakika ya mambo ni kwamba Ujuzi wa kipindi cha Kiyama uko kwa Mwenyezi Mungu.» Na ni lipi linalokujuza wewe, ewe Mtume kwamba huenda Kiyama kikawa karibu?
Les exégèses en arabe:
إِنَّ ٱللَّهَ لَعَنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ وَأَعَدَّ لَهُمۡ سَعِيرًا
Mwenyezi Mungu Amewafukuza makafiri kwenye rehema Yake duniani na Akhera na Amewaandalia huko Akhera Moto wenye kuwashwa ulio na joto kali,
Les exégèses en arabe:
خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۖ لَّا يَجِدُونَ وَلِيّٗا وَلَا نَصِيرٗا
hali ya kukaa milele humo. Hawatapata mtegemewa wa kuwasaidia na kuwatetea, wala mwenye himaya wa kuwahami, Akawatoa Motoni.
Les exégèses en arabe:
يَوۡمَ تُقَلَّبُ وُجُوهُهُمۡ فِي ٱلنَّارِ يَقُولُونَ يَٰلَيۡتَنَآ أَطَعۡنَا ٱللَّهَ وَأَطَعۡنَا ٱلرَّسُولَا۠
Siku zitakapogeuzwa nyuso za makafiri Motoni, huku wakisema kwa kujuta na kuduwaa, «Tunatamani lau tungalimtii Mwenyezi Mungu na tungalimtii Mtume Wake duniani tukawa watu wa Peponi.»
Les exégèses en arabe:
وَقَالُواْ رَبَّنَآ إِنَّآ أَطَعۡنَا سَادَتَنَا وَكُبَرَآءَنَا فَأَضَلُّونَا ٱلسَّبِيلَا۠
Na watasema makafiri Siku ya Kiyama, «Mola wetu! Kwa kweli sisi tumewatii viongozi wetu katika upotevu na wakubwa wetu katika ushirikina wakatuepusha na njia ya uongofu na Imani.
Les exégèses en arabe:
رَبَّنَآ ءَاتِهِمۡ ضِعۡفَيۡنِ مِنَ ٱلۡعَذَابِ وَٱلۡعَنۡهُمۡ لَعۡنٗا كَبِيرٗا
Mola wetu! Waadhibu Motoni mara mbili zaidi ya adhabu unayotuadhibu kwayo, na uwafukuze kutoka kwenye rehema mafukuzo makali.» Katika hii pana dalili ya kwamba kumtii asiyekuwa Mwenyezi Mungu katika kuenda kinyume na amri Yake na amri ya Mtume Wake, kunapasisha kupata hasira za Mwenyezi Mungu na mateso Yake, na kwamba mfuasi na mfuatwa watashirikiana kwenye adhabu. Basi ajihadhari na hilo Muislamu.
Les exégèses en arabe:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَكُونُواْ كَٱلَّذِينَ ءَاذَوۡاْ مُوسَىٰ فَبَرَّأَهُ ٱللَّهُ مِمَّا قَالُواْۚ وَكَانَ عِندَ ٱللَّهِ وَجِيهٗا
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata Sheria Zake kivitendo, msimkere Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa maneno wala kwa vitendo, wala msiwe mfano wa wale waliomkera Nabii wa Mwenyezi Mungu Mūsā, Mwenyezi Mungu Akamuepusha na kile walichokisema cha urongo na uzushi, na yeye alikuwa kwa Mwenyezi Mungu ni mwenye cheo kikubwa na utukufu.
Les exégèses en arabe:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَقُولُواْ قَوۡلٗا سَدِيدٗا
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkazifuata Sheria Zake kivitendo, fanyeni matendo ya kumtii na mjiepushe na matendo ya kumuasi, ili msistahili kupata mateso hayo. Na semeni, katika hali zenu zote na mambo yenu yote, maneno ya kunyoka na yanayolingana na usawa, yasiyokuwa na urongo na ubatilifu.
Les exégèses en arabe:
يُصۡلِحۡ لَكُمۡ أَعۡمَٰلَكُمۡ وَيَغۡفِرۡ لَكُمۡ ذُنُوبَكُمۡۗ وَمَن يُطِعِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ فَقَدۡ فَازَ فَوۡزًا عَظِيمًا
Mkimuogopa Mwenyezi Mungu na mkasema maneno ya sawa, Mwenyezi Mungu Atawasamehe dhambi zenu, Na mwenye kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, katika kile alichokiamrisha na akakikataza, basi huyo amefaulu kupata utukufu mkubwa duniani na Akhera.
Les exégèses en arabe:
إِنَّا عَرَضۡنَا ٱلۡأَمَانَةَ عَلَى ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَٱلۡجِبَالِ فَأَبَيۡنَ أَن يَحۡمِلۡنَهَا وَأَشۡفَقۡنَ مِنۡهَا وَحَمَلَهَا ٱلۡإِنسَٰنُۖ إِنَّهُۥ كَانَ ظَلُومٗا جَهُولٗا
Sisi tuliiorodhesha amana- ambayo Mwenyezi Mungu Amewapatia waliokalifishwa na Sheria waitunze, nayo ni kufuata maamrisho na kujiepusha na makatazo- kwa mbingu, ardhi na majabali, vikakataa kuibeba na vikaogopa visiweze kusimama kuitekeleza, na akaibeba binadamu na akashikamana nayo pamoja na udhaifu Wake. Hakika yeye ni mwingi wa udhalimu na ujinga wa nafsi yake.
Les exégèses en arabe:
لِّيُعَذِّبَ ٱللَّهُ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَٱلۡمُنَٰفِقَٰتِ وَٱلۡمُشۡرِكِينَ وَٱلۡمُشۡرِكَٰتِ وَيَتُوبَ ٱللَّهُ عَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِۗ وَكَانَ ٱللَّهُ غَفُورٗا رَّحِيمَۢا
Ili mwisho wa binadamu kuibeba amana uwe ni Mwenyezi Mungu kuwaadhibu wanafiki wa kiume wanaodhihirisha Uislamu na kuficha ukafiri na wanafiki wa kike, na wanaume wanaomshirikisha katika ibada ya Mwenyezi Mungu asiyekuwa Yeye na wanawake washirikina, na ili Awakubalie toba Waumini wa kiume na Waumini wa kike kwa kuzificha dhambi zao na kuacha kuwaadhibu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa msamaha kwa wenye kutubia miongoni mwa waja Wake, ni Mwenye huruma kwao.
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Sourate: Al Ahzâb
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - La traduction swahili - 'Abd Allah Muhammad et Nâsir Khamîs - Lexique des traductions

Traduit par le Dr. 'Abd Allah Muhammad Abû Bakr et Cheikh Nâsir Khamîs.

Fermeture