Traduction des sens du Noble Coran - Traduction en Swahili - 'AbdaLlah Muhammad et Nasser Khamîs * - Lexique des traductions


Traduction des sens Verset: (53) Sourate: AL-AHZÂB
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَدۡخُلُواْ بُيُوتَ ٱلنَّبِيِّ إِلَّآ أَن يُؤۡذَنَ لَكُمۡ إِلَىٰ طَعَامٍ غَيۡرَ نَٰظِرِينَ إِنَىٰهُ وَلَٰكِنۡ إِذَا دُعِيتُمۡ فَٱدۡخُلُواْ فَإِذَا طَعِمۡتُمۡ فَٱنتَشِرُواْ وَلَا مُسۡتَـٔۡنِسِينَ لِحَدِيثٍۚ إِنَّ ذَٰلِكُمۡ كَانَ يُؤۡذِي ٱلنَّبِيَّ فَيَسۡتَحۡيِۦ مِنكُمۡۖ وَٱللَّهُ لَا يَسۡتَحۡيِۦ مِنَ ٱلۡحَقِّۚ وَإِذَا سَأَلۡتُمُوهُنَّ مَتَٰعٗا فَسۡـَٔلُوهُنَّ مِن وَرَآءِ حِجَابٖۚ ذَٰلِكُمۡ أَطۡهَرُ لِقُلُوبِكُمۡ وَقُلُوبِهِنَّۚ وَمَا كَانَ لَكُمۡ أَن تُؤۡذُواْ رَسُولَ ٱللَّهِ وَلَآ أَن تَنكِحُوٓاْ أَزۡوَٰجَهُۥ مِنۢ بَعۡدِهِۦٓ أَبَدًاۚ إِنَّ ذَٰلِكُمۡ كَانَ عِندَ ٱللَّهِ عَظِيمًا
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkazifuata Sheria Zake kivitendo, msiingie nyumba za Mtume, isipokuwa kwa ruhusa yake, kwa kula chakula bila ya kungoja kuiva kwake. Lakini mkiitwa ingieni, na mkimaliza kula ondokeni, bila ya kujipumbaza kwa mazungumzo baina yenu. Kwani kule kungoja kwenu na kujipumbaza kwenu kunamkera Nabii, naye anawaonea haya kuwatoa kwenye hizo nyumba pamoja na kuwa hiyo ni haki yake, na Mwenyezi Mungu Haoni haya kuieleza haki na kuifunua. Na mkiwaomba wake za Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, wawapatie kitu chochote mnachokihitajia katika vyombo vya nyumbani na mfano wake, basi waombeni mkiwa nyuma ya pazia. Kufanya kwenu hivyo kunatakasa zaidi nyoyo zenu na nyoyo zao na kuziepusha na mawazo ambayo yanawapitia wanaume kuhusu mambo ya wanawake na wanawake kuhusu mambo ya wanaume, kwani kuona ndio sababu ya kufitinika. Na haifai kwenu kumkera Mtume wa Mwenyezi Mungu wala kuwaoa wake zake baada ya kufa kwake kabisa, kwa kuwa wao ni mama zenu, na haifai mtu kumuoa mamake. Hakika kumkera kwenu Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na kuwaoa wake zake baada yake ni dhambi kubwa kwa Mwenyezi Mungu. Ummah huu ulitekeleza amri hii na ulijiepusha na kile Mwenyezi Mungu Aliukataza nacho.
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Verset: (53) Sourate: AL-AHZÂB
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - Traduction en Swahili - 'AbdaLlah Muhammad et Nasser Khamîs - Lexique des traductions

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Fermeture