Traduction des sens du Noble Coran - Traduction en Swahili - 'AbdaLlah Muhammad et Nasser Khamîs * - Lexique des traductions


Traduction des sens Verset: (3) Sourate: AL-MOUJÂDALAH
وَٱلَّذِينَ يُظَٰهِرُونَ مِن نِّسَآئِهِمۡ ثُمَّ يَعُودُونَ لِمَا قَالُواْ فَتَحۡرِيرُ رَقَبَةٖ مِّن قَبۡلِ أَن يَتَمَآسَّاۚ ذَٰلِكُمۡ تُوعَظُونَ بِهِۦۚ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ
Na wale wanaojiharamishia wake zao kwa kuwafananisha na migongo ya mama zao kisha wakarudi nyuma na hilo neno na wakataka kuwaingilia, basi ni juu ya yule mume aliyetoa tamshi la ẓihār, katika hali hii, atoe kafara ya kule kujiharamishia, nayo ni kuacha shingo huru yenye Imani: mtumwa au kijakazi, kabla hajamuingilia yule mkewe aliyemfananisha na mgongo wa mamake. Hiyo ndiyo hukumu ya Mwenyezi Mungu kwa anayemfananisha mkewe na mgongo wa mamake, mnakumbushwa mwaidhike nayo, enyi Waumini, ili msiingie kwenye kosa la kuwafananisha wake zenu na mama zenu na kusema neno la uzushi, na mtoe kafara mnapoingia kwenye kosa hilo, na ili msirudie tena kufanya hilo. Na Mwenyezi Mungu hakifichamani chochote Kwake Yeye katika matendo yenu, na Yeye ni Mwenye kuwalipa kwayo
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Verset: (3) Sourate: AL-MOUJÂDALAH
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - Traduction en Swahili - 'AbdaLlah Muhammad et Nasser Khamîs - Lexique des traductions

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Fermeture