Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani * - Lexique des traductions

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduction des sens Verset: (108) Sourate: HOUD
۞ وَأَمَّا ٱلَّذِينَ سُعِدُواْ فَفِي ٱلۡجَنَّةِ خَٰلِدِينَ فِيهَا مَا دَامَتِ ٱلسَّمَٰوَٰتُ وَٱلۡأَرۡضُ إِلَّا مَا شَآءَ رَبُّكَۖ عَطَآءً غَيۡرَ مَجۡذُوذٖ
Na ama wale walio bahatika, wao watakuwamo Peponi wakidumu humo muda wa kudumu mbingu na ardhi, isipo kuwa apendavyo Mola wako Mlezi. Hicho ni kipawa kisio na ukomo.
Ama wale ambao Mwenyezi Mungu amewajaalia kuwa na bahati njema wataingia Peponi wadumu humo tangu mwanzo, mara baada ya kwisha hisabiwa. Huko hakuna mwisho. Isipo kuwa kikundi ambacho Mwenyezi Mungu anataka kukiakhirisha kisiingie pamoja na wale wa mwanzo - na hao ni wale Waumini walio fanya maasi. Hao watacheleweshwa Motoni kwa kadiri ya kupata adabu ya kuwasafisha wapate kuingia Peponi. Na Mwenyezi Mungu atawalipa hawa walio bahatika malipo bora kabisa ya kudumu, yasio na kasoro, wala yasio katika.
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Verset: (108) Sourate: HOUD
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani - Lexique des traductions

Traduction des sens du noble Coran en langue Swahili, par Ali Muhsin al-Barwani.

Fermeture