Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani * - Lexique des traductions

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduction des sens Verset: (30) Sourate: AN-NAHL
۞ وَقِيلَ لِلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْ مَاذَآ أَنزَلَ رَبُّكُمۡۚ قَالُواْ خَيۡرٗاۗ لِّلَّذِينَ أَحۡسَنُواْ فِي هَٰذِهِ ٱلدُّنۡيَا حَسَنَةٞۚ وَلَدَارُ ٱلۡأٓخِرَةِ خَيۡرٞۚ وَلَنِعۡمَ دَارُ ٱلۡمُتَّقِينَ
Na wataambiwa walio mcha Mungu: Mola wenu Mlezi kateremsha nini? Watasema: Kheri. Walio fanya wema katika dunia hii watapata wema. Na nyumba ya Akhera ni bora zaidi, na njema mno nyumba ya wachamngu.
Na walio muamini Mwenyezi Mungu na wakajikinga na kila linalo mghadhibisha Yeye ikiwa neno, au kitendo, au itikadi, wataambiwa: Mola wenu Mlezi kamteremshia nini Mtume wake? Wao watasema: Amemteremshia Qur'ani...ndani yake mna kheri ya duniani na Akhera kwa watu wote, na kwa hivyo wakawa miongoni mwa watu wema. Na Mwenyezi Mungu Subhanahu huwalipa wema kwa maisha mazuri katika uhai huu wa duniani. Na pahala pao Akhera ni bora na pazuri zaidi kuliko waliyo yapata duniani. Na nyumba watayo ikaa wachamngu Akhera ni hadi ya raha yake!
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Verset: (30) Sourate: AN-NAHL
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani - Lexique des traductions

Traduction des sens du noble Coran en langue Swahili, par Ali Muhsin al-Barwani.

Fermeture