Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani * - Lexique des traductions

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduction des sens Verset: (245) Sourate: AL-BAQARAH
مَّن ذَا ٱلَّذِي يُقۡرِضُ ٱللَّهَ قَرۡضًا حَسَنٗا فَيُضَٰعِفَهُۥ لَهُۥٓ أَضۡعَافٗا كَثِيرَةٗۚ وَٱللَّهُ يَقۡبِضُ وَيَبۡصُۜطُ وَإِلَيۡهِ تُرۡجَعُونَ
Ni nani atakaye mkopesha Mwenyezi Mungu mkopo mwema ili amzidishie mzidisho mwingi, na Mwenyezi Mungu hukunja na hukunjua. Na Kwake Yeye mtarejea.
Na Jihadi kwa Njia ya Mwenyezi inhaitaji mali, basi toeni mali yenu. Mtu gani huyo ambaye hatoi mali yake kwa ajili ya Mwenyezi Mungu kwa radhi ya nafsi yake, na hali Mwenyezi Mungu ameahidi kuwa atamrejeshea mara nyingi sana zaidi? Na riziki zote zimo katika mkono wa Mwenyezi Mungu. Yeye ndiye humkunjia amtakaye na akamkunjulia amtakaye kwa yaliyo na maslaha yenu. Marejeo ni kwake Yeye, naye atakulipeni kwa mujibu mlivyo toa. Na ilivyo kuwa riziki zote ni kwa fadhila ya Mwenyezi na Yeye ndiye mwenye kutoa na mwenye kunyima basi ameitwa yule mwenye kutoa kuwa ni kama mkopeshaji ili kuhimiza na kupendekeza kutoa, na kutilia mkazo kuwa malipo ni mara nyingi sana duniani na Akhera.
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Verset: (245) Sourate: AL-BAQARAH
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani - Lexique des traductions

Traduction des sens du noble Coran en langue Swahili, par Ali Muhsin al-Barwani.

Fermeture