Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani * - Lexique des traductions

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduction des sens Verset: (246) Sourate: AL-BAQARAH
أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلۡمَلَإِ مِنۢ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ مِنۢ بَعۡدِ مُوسَىٰٓ إِذۡ قَالُواْ لِنَبِيّٖ لَّهُمُ ٱبۡعَثۡ لَنَا مَلِكٗا نُّقَٰتِلۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِۖ قَالَ هَلۡ عَسَيۡتُمۡ إِن كُتِبَ عَلَيۡكُمُ ٱلۡقِتَالُ أَلَّا تُقَٰتِلُواْۖ قَالُواْ وَمَا لَنَآ أَلَّا نُقَٰتِلَ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ وَقَدۡ أُخۡرِجۡنَا مِن دِيَٰرِنَا وَأَبۡنَآئِنَاۖ فَلَمَّا كُتِبَ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقِتَالُ تَوَلَّوۡاْ إِلَّا قَلِيلٗا مِّنۡهُمۡۚ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِٱلظَّٰلِمِينَ
Hukuwaona watukufu katika Wana wa Israili baada ya Musa, walipo mwambia Nabii wao: Tuwekee mfalme ili tupigane katika Njia ya Mwenyezi Mungu? Akasema: Je, haielekei ikiwa mtaandikiwa vita kuwa msipigane? Wakasema: Itakuwaje tusipigane katika Njia ya Mwenyezi Mungu, na hali tumetolewa majumbani kwetu na watoto wetu? Lakini walipo andikiwa kupigana waligeuka, isipo kuwa wachache miongoni mwao. Na Mwenyezi Mungu anawajua madhaalimu.
Zingatia khabari hii ya ajabu ya baadhi ya Wana wa Israili baada ya zama za Musa. Walimtaka Nabii wao wa wakati ule awawekee mtawala ataye weza kuwakusanya baada ya mfarakano walio kuwa nao, awaongoze chini ya bendera ya kutukuza Neno la Mwenyezi Mungu na kurejeza utukufu wao. Yule Nabii akawauliza kuhakikisha kama wana ukweli katika jambo hilo: "Je haiwezi kuwa nyinyi mtaingia woga mkatae kupigana pindi mkifaridhiwa mpigane?" Wakakataa hayo wakisema: "Itakuwaje tusipigane kurejeza haki zetu, na hali sisi tumefukuzwa makwetu na adui?" Mwenyezi Mungu alipo waitikia yale wayatakayo na akaandikia vita wakakataa ila kikundi cha wachache tu miongoni mwao. Na kule kukataa kwao ni dhulma kujidhulumu nafsi zao, na Nabii wao na Dini yao. Na Mwenyezi Mungu anayajua hayo kwao, na atawalipa malipo ya madhaalimu.
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Verset: (246) Sourate: AL-BAQARAH
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani - Lexique des traductions

Traduction des sens du noble Coran en langue Swahili, par Ali Muhsin al-Barwani.

Fermeture