Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani * - Lexique des traductions

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduction des sens Verset: (41) Sourate: AN-NOUR
أَلَمۡ تَرَ أَنَّ ٱللَّهَ يُسَبِّحُ لَهُۥ مَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَٱلطَّيۡرُ صَٰٓفَّٰتٖۖ كُلّٞ قَدۡ عَلِمَ صَلَاتَهُۥ وَتَسۡبِيحَهُۥۗ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِمَا يَفۡعَلُونَ
Je! Huoni kwamba Mwenyezi Mungu vinamtakasa vilivyomo katika mbingu na ardhi, na ndege wakikunjua mbawa zao? Kila mmoja amekwisha jua Sala yake na namna ya kumtakasa kwake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyajua wayatendayo.
Ewe Nabii! Hujui kwa yakini kwamba kwa Mwenyezi Mungu hunyenyekea kila kiliomo mbinguni na duniani? Na wanamnyenyekea ndege vile vile, nao wamekunjua mbawa zao? Basi viumbe vyote hivi vinanyenyekea amri ya Mwenyezi Mungu na mipango yake. Vinamtakasa na washirika na kila lisio na laiki naye. Na kila kimojawapo kinajua kwa kujaaliwa na Mwenyezi Mungu yaliyo kiwajibikia katika unyenyekevu na kutakasa na kutimiza wadhifa wa maisha. Na Mwenyezi Mungu nyuma yao anajua kwa utimilivu wa kujua Swala ya kila mwenye kusali, na kusabihi kwa mwenye kusabihi, na yote wayafanyayo waja. Basi huwaje makafiri wakawa hawaamini?
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Verset: (41) Sourate: AN-NOUR
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani - Lexique des traductions

Traduction des sens du noble Coran en langue Swahili, par Ali Muhsin al-Barwani.

Fermeture