Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani * - Lexique des traductions

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduction des sens Verset: (17) Sourate: AL-AHQÂF
وَٱلَّذِي قَالَ لِوَٰلِدَيۡهِ أُفّٖ لَّكُمَآ أَتَعِدَانِنِيٓ أَنۡ أُخۡرَجَ وَقَدۡ خَلَتِ ٱلۡقُرُونُ مِن قَبۡلِي وَهُمَا يَسۡتَغِيثَانِ ٱللَّهَ وَيۡلَكَ ءَامِنۡ إِنَّ وَعۡدَ ٱللَّهِ حَقّٞ فَيَقُولُ مَا هَٰذَآ إِلَّآ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na ambaye amewafyonya wazazi wake na akawaambia: Ati ndio mnanitisha kuwa nitafufuliwa, na hali vizazi vingi vimekwisha pita kabla yangu! Na hao wazazi humwomba msaada Mwenyezi Mungu (na humwambia mtoto wao): Ole wako! Amini! Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli. Na yeye husema: Hayakuwa haya ila ni visa vya watu wa kale.
Na waliwafyonya wazazi wao kwa kuchukia na kuchoka nao, walipo wataka waamini kufufuliwa, na wakawaambia: Mnaniambia tutatoka makaburini na mataifa mangapi yamepita kabla yangu na hapana hata mmoja aliye fufuliwa kutoka makaburini? Na hao wazazi wake wanaomba msaada kwa Mwenyezi Mungu jinsi ya kuona ni makuu makosa ya mwana wao, wakisema kwa kumshikilia aamini: Utaangamia wewe kama hukuamini. Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu ya kufufua ni kweli. Naye bado amekakamia kukadhibisha kwa kusema: Hayo mnayo yasema si chochote ila ni hadithi za uwongo za watu wa kale!
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Verset: (17) Sourate: AL-AHQÂF
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani - Lexique des traductions

Traduction des sens du noble Coran en langue Swahili, par Ali Muhsin al-Barwani.

Fermeture