કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સ્વાહિલી ભાષાતર - અલી મોહસીન અલ્ બરવાની * - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

શબ્દોનું ભાષાંતર આયત: (91) સૂરહ: અલ્ અન્આમ
وَمَا قَدَرُواْ ٱللَّهَ حَقَّ قَدۡرِهِۦٓ إِذۡ قَالُواْ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ عَلَىٰ بَشَرٖ مِّن شَيۡءٖۗ قُلۡ مَنۡ أَنزَلَ ٱلۡكِتَٰبَ ٱلَّذِي جَآءَ بِهِۦ مُوسَىٰ نُورٗا وَهُدٗى لِّلنَّاسِۖ تَجۡعَلُونَهُۥ قَرَاطِيسَ تُبۡدُونَهَا وَتُخۡفُونَ كَثِيرٗاۖ وَعُلِّمۡتُم مَّا لَمۡ تَعۡلَمُوٓاْ أَنتُمۡ وَلَآ ءَابَآؤُكُمۡۖ قُلِ ٱللَّهُۖ ثُمَّ ذَرۡهُمۡ فِي خَوۡضِهِمۡ يَلۡعَبُونَ
Na hawakumkadiria Mwenyezi Mungu kwa haki ya kadri yake, walipo sema: Mwenyezi Mungu hakumteremshia mwanaadamu chochote. Sema: Nani aliyo teremsha Kitabu alicho kuja nacho Musa, chenye nuru na uwongofu kwa watu, mlicho kifanya kurasa kurasa mkizionyesha, na mengi mkiyaficha. Na mkafunzwa mlio kuwa hamyajui nyinyi wala baba zenu? Sema: Mwenyezi Mungu. Kisha waache wacheze katika porojo lao.
Na hawa makafiri hawakumkadiria Mwenyezi Mungu na rehema yake na hikima yake kwa anavyo stahiki, walipo kanya kuteremshwa ujumbe wake kwa binaadamu yeyote! Ewe Nabii! Waambie washirikina na wanao waunga mkono katika hayo miongoni mwa Mayahudi: Nani aliye kiteremsha Kitabu alicho kuja nacho Musa, ambacho kina nuru iliyo zagaa, na uwongofu wa kuongozea? Nyinyi Mayahudi mnakifanya hicho kuwa ni maandiko yaliyo gawiwa mafungu mbali mbali. Yanayo kubaliana na mapendo yenu mnayaonyesha, na mengi mnayaficha yale yanayo kupelekeeni kuiamini na kuisadiki Qur'ani. Na kutokana na Kitabu hicho mmejifunza mambo ambayo nyinyi na baba zenu hamkuwa mkiyajua!! Na ewe Nabii! Jawabu wape wewe kwa kuwaambia: Mwenyezi Mungu ndiye aliye iteremsha Taurati. Kisha waache wakiendelea katika upotovu, wakicheza kama watoto wadogo.
અરબી તફસીરો:
 
શબ્દોનું ભાષાંતર આયત: (91) સૂરહ: અલ્ અન્આમ
સૂરહ માટે અનુક્રમણિકા પેજ નંબર
 
કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સ્વાહિલી ભાષાતર - અલી મોહસીન અલ્ બરવાની - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા

સ્વાહિલી ભાષામાં કુરઆન મજીદનું ભાષાતર, ભાષાતર કરનારનું નામ મોહસીન અલ્ બરવાની

બંધ કરો