કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સ્વાહિલી ભાષાતર - અલી મોહસીન અલ્ બરવાની * - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

શબ્દોનું ભાષાંતર સૂરહ: અલ્ મુદષષિર   આયત:

Surat Al-Muddathir

يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡمُدَّثِّرُ
Ewe uliye jigubika!
અરબી તફસીરો:
قُمۡ فَأَنذِرۡ
Simama uonye!
અરબી તફસીરો:
وَرَبَّكَ فَكَبِّرۡ
Na Mola wako Mlezi mtukuze!
અરબી તફસીરો:
وَثِيَابَكَ فَطَهِّرۡ
Na nguo zako, zisafishe.
અરબી તફસીરો:
وَٱلرُّجۡزَ فَٱهۡجُرۡ
Na yaliyo machafu yahame!
અરબી તફસીરો:
وَلَا تَمۡنُن تَسۡتَكۡثِرُ
Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.
અરબી તફસીરો:
وَلِرَبِّكَ فَٱصۡبِرۡ
Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!
અરબી તફસીરો:
فَإِذَا نُقِرَ فِي ٱلنَّاقُورِ
Basi litapo pulizwa barugumu,
અરબી તફસીરો:
فَذَٰلِكَ يَوۡمَئِذٖ يَوۡمٌ عَسِيرٌ
Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.
અરબી તફસીરો:
عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ غَيۡرُ يَسِيرٖ
Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.
અરબી તફસીરો:
ذَرۡنِي وَمَنۡ خَلَقۡتُ وَحِيدٗا
Niache peke yangu na niliye muumba;
અરબી તફસીરો:
وَجَعَلۡتُ لَهُۥ مَالٗا مَّمۡدُودٗا
Na nikamjaalia awe na mali mengi,
અરબી તફસીરો:
وَبَنِينَ شُهُودٗا
Na wana wanao onekana,
અરબી તફસીરો:
وَمَهَّدتُّ لَهُۥ تَمۡهِيدٗا
Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.
અરબી તફસીરો:
ثُمَّ يَطۡمَعُ أَنۡ أَزِيدَ
Kisha anatumai nimzidishie!
અરબી તફસીરો:
كَلَّآۖ إِنَّهُۥ كَانَ لِأٓيَٰتِنَا عَنِيدٗا
Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!
અરબી તફસીરો:
سَأُرۡهِقُهُۥ صَعُودًا
Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.
અરબી તફસીરો:
إِنَّهُۥ فَكَّرَ وَقَدَّرَ
Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.
અરબી તફસીરો:
فَقُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ
Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!
અરબી તફસીરો:
ثُمَّ قُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ
Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!
અરબી તફસીરો:
ثُمَّ نَظَرَ
Kisha akatazama,
અરબી તફસીરો:
ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ
Kisha akakunja kipaji, na akanuna.
અરબી તફસીરો:
ثُمَّ أَدۡبَرَ وَٱسۡتَكۡبَرَ
Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.
અરબી તફસીરો:
فَقَالَ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ يُؤۡثَرُ
Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa.
અરબી તફસીરો:
إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا قَوۡلُ ٱلۡبَشَرِ
Haya si chochote ila kauli ya binaadamu.
અરબી તફસીરો:
سَأُصۡلِيهِ سَقَرَ
Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.
અરબી તફસીરો:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سَقَرُ
Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?
અરબી તફસીરો:
لَا تُبۡقِي وَلَا تَذَرُ
Haubakishi wala hausazi.
અરબી તફસીરો:
لَوَّاحَةٞ لِّلۡبَشَرِ
Unababua ngozi iwe nyeusi.
અરબી તફસીરો:
عَلَيۡهَا تِسۡعَةَ عَشَرَ
Juu yake wapo kumi na tisa.
અરબી તફસીરો:
وَمَا جَعَلۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلنَّارِ إِلَّا مَلَٰٓئِكَةٗۖ وَمَا جَعَلۡنَا عِدَّتَهُمۡ إِلَّا فِتۡنَةٗ لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ لِيَسۡتَيۡقِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَيَزۡدَادَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِيمَٰنٗا وَلَا يَرۡتَابَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَلِيَقُولَ ٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ وَٱلۡكَٰفِرُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلٗاۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَمَا يَعۡلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَۚ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكۡرَىٰ لِلۡبَشَرِ
Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha walio kufuru, wapate kuwa na yakini walio pewa Kitabu, na wazidi Imani wale walio amini, wala wasiwe na shaka walio pewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu? Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anaye jua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binaadamu.
અરબી તફસીરો:
كَلَّا وَٱلۡقَمَرِ
Hasha! Naapa kwa mwezi!
અરબી તફસીરો:
وَٱلَّيۡلِ إِذۡ أَدۡبَرَ
Na kwa usiku unapo kucha!
અરબી તફસીરો:
وَٱلصُّبۡحِ إِذَآ أَسۡفَرَ
Na kwa asubuhi inapo pambazuka!
અરબી તફસીરો:
إِنَّهَا لَإِحۡدَى ٱلۡكُبَرِ
Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!
અરબી તફસીરો:
نَذِيرٗا لِّلۡبَشَرِ
Ni onyo kwa binaadamu,
અરબી તફસીરો:
لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَتَقَدَّمَ أَوۡ يَتَأَخَّرَ
Kwa anaye taka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.
અરબી તફસીરો:
كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا كَسَبَتۡ رَهِينَةٌ
Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyo yachuma.
અરબી તફસીરો:
إِلَّآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡيَمِينِ
Isipo kuwa watu wa kuliani.
અરબી તફસીરો:
فِي جَنَّٰتٖ يَتَسَآءَلُونَ
Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana
અરબી તફસીરો:
عَنِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
Khabari za wakosefu:
અરબી તફસીરો:
مَا سَلَكَكُمۡ فِي سَقَرَ
Ni nini kilicho kupelekeni Motoni?
અરબી તફસીરો:
قَالُواْ لَمۡ نَكُ مِنَ ٱلۡمُصَلِّينَ
Waseme: Hatukuwa miongoni walio kuwa wakiswali.
અરબી તફસીરો:
وَلَمۡ نَكُ نُطۡعِمُ ٱلۡمِسۡكِينَ
Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.
અરબી તફસીરો:
وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ ٱلۡخَآئِضِينَ
Na tulikuwa tukizama pamoja na walio zama katika maovu.
અરબી તફસીરો:
وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ
Na tulikuwa tukiikanusha siku ya malipo.
અરબી તફસીરો:
حَتَّىٰٓ أَتَىٰنَا ٱلۡيَقِينُ
Mpaka yakini ilipo tufikia.
અરબી તફસીરો:
فَمَا تَنفَعُهُمۡ شَفَٰعَةُ ٱلشَّٰفِعِينَ
Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.
અરબી તફસીરો:
فَمَا لَهُمۡ عَنِ ٱلتَّذۡكِرَةِ مُعۡرِضِينَ
Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?
અરબી તફસીરો:
كَأَنَّهُمۡ حُمُرٞ مُّسۡتَنفِرَةٞ
Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,
અરબી તફસીરો:
فَرَّتۡ مِن قَسۡوَرَةِۭ
Wanao mkimbia simba!
અરબી તફસીરો:
بَلۡ يُرِيدُ كُلُّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ أَن يُؤۡتَىٰ صُحُفٗا مُّنَشَّرَةٗ
Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo funuliwa.
અરબી તફસીરો:
كَلَّاۖ بَل لَّا يَخَافُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ
Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?
અરબી તફસીરો:
كَلَّآ إِنَّهُۥ تَذۡكِرَةٞ
Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!
અરબી તફસીરો:
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi anaye taka atakumbuka.
અરબી તફસીરો:
وَمَا يَذۡكُرُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُۚ هُوَ أَهۡلُ ٱلتَّقۡوَىٰ وَأَهۡلُ ٱلۡمَغۡفِرَةِ
Na hawatakumbuka isipo kuwa Mwenyezi Mungu atake. Uchamngu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.
અરબી તફસીરો:
 
શબ્દોનું ભાષાંતર સૂરહ: અલ્ મુદષષિર
સૂરહ માટે અનુક્રમણિકા પેજ નંબર
 
કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સ્વાહિલી ભાષાતર - અલી મોહસીન અલ્ બરવાની - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા

સ્વાહિલી ભાષામાં કુરઆન મજીદનું ભાષાતર, ભાષાતર કરનારનું નામ મોહસીન અલ્ બરવાની

બંધ કરો