Check out the new design

કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સવાહિલી ભાષાતર - મરકઝ રુવાદ અત્-તરજુમા * - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા


શબ્દોનું ભાષાંતર સૂરહ: અલ્ હાકકહ   આયત:

Al-Haqqah

ٱلۡحَآقَّةُ
Tukio la haki.
અરબી તફસીરો:
مَا ٱلۡحَآقَّةُ
Nini hilo Tukio la haki?
અરબી તફસીરો:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحَآقَّةُ
Na nini kitakachokujulisha nini hilo Tukio la haki?
અરબી તફસીરો:
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ وَعَادُۢ بِٱلۡقَارِعَةِ
Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unaositusha.
અરબી તફસીરો:
فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهۡلِكُواْ بِٱلطَّاغِيَةِ
Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.
અરબી તફસીરો:
وَأَمَّا عَادٞ فَأُهۡلِكُواْ بِرِيحٖ صَرۡصَرٍ عَاتِيَةٖ
Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usiozuilika.
અરબી તફસીરો:
سَخَّرَهَا عَلَيۡهِمۡ سَبۡعَ لَيَالٖ وَثَمَٰنِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومٗاۖ فَتَرَى ٱلۡقَوۡمَ فِيهَا صَرۡعَىٰ كَأَنَّهُمۡ أَعۡجَازُ نَخۡلٍ خَاوِيَةٖ
Aliowapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yaliyo wazi ndani.
અરબી તફસીરો:
فَهَلۡ تَرَىٰ لَهُم مِّنۢ بَاقِيَةٖ
Basi je! Unamwona mmoja wao aliyebaki?
અરબી તફસીરો:
وَجَآءَ فِرۡعَوۡنُ وَمَن قَبۡلَهُۥ وَٱلۡمُؤۡتَفِكَٰتُ بِٱلۡخَاطِئَةِ
Na Firauni na waliomtangulia, na miji iliyopinduliwa chini juu, walileta khatia.
અરબી તફસીરો:
فَعَصَوۡاْ رَسُولَ رَبِّهِمۡ فَأَخَذَهُمۡ أَخۡذَةٗ رَّابِيَةً
Akamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato uliozidi nguvu.
અરબી તફસીરો:
إِنَّا لَمَّا طَغَا ٱلۡمَآءُ حَمَلۡنَٰكُمۡ فِي ٱلۡجَارِيَةِ
Maji yalipofurika Sisi tulikupandisheni katika safina.
અરબી તફસીરો:
لِنَجۡعَلَهَا لَكُمۡ تَذۡكِرَةٗ وَتَعِيَهَآ أُذُنٞ وَٰعِيَةٞ
Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalosikia liyahifadhi.
અરબી તફસીરો:
فَإِذَا نُفِخَ فِي ٱلصُّورِ نَفۡخَةٞ وَٰحِدَةٞ
Na litapopulizwa barugumu mpulizo mmoja tu.
અરબી તફસીરો:
وَحُمِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ وَٱلۡجِبَالُ فَدُكَّتَا دَكَّةٗ وَٰحِدَةٗ
Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja.
અરબી તફસીરો:
فَيَوۡمَئِذٖ وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ
Siku hiyo ndio Tukio litatukia.
અરબી તફસીરો:
وَٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَهِيَ يَوۡمَئِذٖ وَاهِيَةٞ
Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.
અરબી તફસીરો:
وَٱلۡمَلَكُ عَلَىٰٓ أَرۡجَآئِهَاۚ وَيَحۡمِلُ عَرۡشَ رَبِّكَ فَوۡقَهُمۡ يَوۡمَئِذٖ ثَمَٰنِيَةٞ
Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.
અરબી તફસીરો:
يَوۡمَئِذٖ تُعۡرَضُونَ لَا تَخۡفَىٰ مِنكُمۡ خَافِيَةٞ
Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.
અરબી તફસીરો:
فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ فَيَقُولُ هَآؤُمُ ٱقۡرَءُواْ كِتَٰبِيَهۡ
Basi ama atakayepewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!
અરબી તફસીરો:
إِنِّي ظَنَنتُ أَنِّي مُلَٰقٍ حِسَابِيَهۡ
Hakika nilijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.
અરબી તફસીરો:
فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ
Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza.
અરબી તફસીરો:
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ
Katika Bustani ya juu.
અરબી તફસીરો:
قُطُوفُهَا دَانِيَةٞ
Matunda yake ya karibu.
અરબી તફસીરો:
كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَآ أَسۡلَفۡتُمۡ فِي ٱلۡأَيَّامِ ٱلۡخَالِيَةِ
Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyotanguliza katika siku zilizopita.
અરબી તફસીરો:
وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِشِمَالِهِۦ فَيَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي لَمۡ أُوتَ كِتَٰبِيَهۡ
Na ama atakayepewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingelipewa kitabu changu!
અરબી તફસીરો:
وَلَمۡ أَدۡرِ مَا حِسَابِيَهۡ
Wala nisingelijua nini hisabu yangu.
અરબી તફસીરો:
يَٰلَيۡتَهَا كَانَتِ ٱلۡقَاضِيَةَ
Laiti mauti ndiyo yangelikuwa ya kunimaliza kabisa.
અરબી તફસીરો:
مَآ أَغۡنَىٰ عَنِّي مَالِيَهۡۜ
Mali yangu hayakunifaa kitu.
અરબી તફસીરો:
هَلَكَ عَنِّي سُلۡطَٰنِيَهۡ
Madaraka yangu yamenipotea.
અરબી તફસીરો:
خُذُوهُ فَغُلُّوهُ
(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!
અરબી તફસીરો:
ثُمَّ ٱلۡجَحِيمَ صَلُّوهُ
Kisha mtupeni Motoni!
અરબી તફસીરો:
ثُمَّ فِي سِلۡسِلَةٖ ذَرۡعُهَا سَبۡعُونَ ذِرَاعٗا فَٱسۡلُكُوهُ
Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabini!
અરબી તફસીરો:
إِنَّهُۥ كَانَ لَا يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ ٱلۡعَظِيمِ
Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu.
અરબી તફસીરો:
وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ
Wala hahimizi kulisha masikini.
અરબી તફસીરો:
فَلَيۡسَ لَهُ ٱلۡيَوۡمَ هَٰهُنَا حَمِيمٞ
Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu.
અરબી તફસીરો:
وَلَا طَعَامٌ إِلَّا مِنۡ غِسۡلِينٖ
Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.
અરબી તફસીરો:
لَّا يَأۡكُلُهُۥٓ إِلَّا ٱلۡخَٰطِـُٔونَ
Chakula hicho hawakili ila wakosefu.
અરબી તફસીરો:
فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَا تُبۡصِرُونَ
Basi ninaapa kwa mnavyoviona.
અરબી તફસીરો:
وَمَا لَا تُبۡصِرُونَ
Na msivyoviona.
અરબી તફસીરો:
إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ
Kwa hakika hii ni kauli iliyoletwa na Mjumbe mwenye heshima.
અરબી તફસીરો:
وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَاعِرٖۚ قَلِيلٗا مَّا تُؤۡمِنُونَ
Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayoyaamini.
અરબી તફસીરો:
وَلَا بِقَوۡلِ كَاهِنٖۚ قَلِيلٗا مَّا تَذَكَّرُونَ
Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayoyakumbuka.
અરબી તફસીરો:
تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
અરબી તફસીરો:
وَلَوۡ تَقَوَّلَ عَلَيۡنَا بَعۡضَ ٱلۡأَقَاوِيلِ
Na lau kama angelituzulia baadhi ya maneno tu.
અરબી તફસીરો:
لَأَخَذۡنَا مِنۡهُ بِٱلۡيَمِينِ
Bila ya shaka tungelimshika kwa mkono wa kulia.
અરબી તફસીરો:
ثُمَّ لَقَطَعۡنَا مِنۡهُ ٱلۡوَتِينَ
Kisha kwa hakika tungelimkata mshipa mkubwa wa moyo!
અરબી તફસીરો:
فَمَا مِنكُم مِّنۡ أَحَدٍ عَنۡهُ حَٰجِزِينَ
Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeliweza kutuzuia.
અરબી તફસીરો:
وَإِنَّهُۥ لَتَذۡكِرَةٞ لِّلۡمُتَّقِينَ
Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wacha Mungu.
અરબી તફસીરો:
وَإِنَّا لَنَعۡلَمُ أَنَّ مِنكُم مُّكَذِّبِينَ
Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanaokadhibisha.
અરબી તફસીરો:
وَإِنَّهُۥ لَحَسۡرَةٌ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanaokataa.
અરબી તફસીરો:
وَإِنَّهُۥ لَحَقُّ ٱلۡيَقِينِ
Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.
અરબી તફસીરો:
فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.
અરબી તફસીરો:
 
શબ્દોનું ભાષાંતર સૂરહ: અલ્ હાકકહ
સૂરહ માટે અનુક્રમણિકા પેજ નંબર
 
કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સવાહિલી ભાષાતર - મરકઝ રુવાદ અત્-તરજુમા - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા

રુવાદ ભાષાંતર કેન્દ્રની ટીમ દ્વારા અને રબ્વાહ ઇસ્લામિક પ્રચાર કાર્યાલય અને વિવિધ ભાષાઓમાં ઇસ્લામની સામગ્રી પ્રસ્તુત કરતું સંગઠનના સહયોગથી

બંધ કરો