Check out the new design

《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 拉瓦德翻译中心。 * - 译解目录


含义的翻译 章: 哈格   段:

Al-Haqqah

ٱلۡحَآقَّةُ
Tukio la haki.
阿拉伯语经注:
مَا ٱلۡحَآقَّةُ
Nini hilo Tukio la haki?
阿拉伯语经注:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحَآقَّةُ
Na nini kitakujulisha nini hilo Tukio la haki?
阿拉伯语经注:
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ وَعَادُۢ بِٱلۡقَارِعَةِ
Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unaositusha.
阿拉伯语经注:
فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهۡلِكُواْ بِٱلطَّاغِيَةِ
Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.
阿拉伯语经注:
وَأَمَّا عَادٞ فَأُهۡلِكُواْ بِرِيحٖ صَرۡصَرٍ عَاتِيَةٖ
Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usiozuilika.
阿拉伯语经注:
سَخَّرَهَا عَلَيۡهِمۡ سَبۡعَ لَيَالٖ وَثَمَٰنِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومٗاۖ فَتَرَى ٱلۡقَوۡمَ فِيهَا صَرۡعَىٰ كَأَنَّهُمۡ أَعۡجَازُ نَخۡلٍ خَاوِيَةٖ
Aliowapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yaliyo wazi ndani.
阿拉伯语经注:
فَهَلۡ تَرَىٰ لَهُم مِّنۢ بَاقِيَةٖ
Basi je! Unamwona mmoja wao aliyebaki?
阿拉伯语经注:
وَجَآءَ فِرۡعَوۡنُ وَمَن قَبۡلَهُۥ وَٱلۡمُؤۡتَفِكَٰتُ بِٱلۡخَاطِئَةِ
Na Firauni na waliomtangulia, na miji iliyopinduliwa chini juu, walileta khatia.
阿拉伯语经注:
فَعَصَوۡاْ رَسُولَ رَبِّهِمۡ فَأَخَذَهُمۡ أَخۡذَةٗ رَّابِيَةً
akamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato uliozidi nguvu.
阿拉伯语经注:
إِنَّا لَمَّا طَغَا ٱلۡمَآءُ حَمَلۡنَٰكُمۡ فِي ٱلۡجَارِيَةِ
Maji yalipofurika Sisi tulikupandisheni katika safina.
阿拉伯语经注:
لِنَجۡعَلَهَا لَكُمۡ تَذۡكِرَةٗ وَتَعِيَهَآ أُذُنٞ وَٰعِيَةٞ
Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalosikia liyahifadhi.
阿拉伯语经注:
فَإِذَا نُفِخَ فِي ٱلصُّورِ نَفۡخَةٞ وَٰحِدَةٞ
Na litapopulizwa barugumu mpulizo mmoja tu.
阿拉伯语经注:
وَحُمِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ وَٱلۡجِبَالُ فَدُكَّتَا دَكَّةٗ وَٰحِدَةٗ
Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja.
阿拉伯语经注:
فَيَوۡمَئِذٖ وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ
Siku hiyo ndio Tukio litatukia.
阿拉伯语经注:
وَٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَهِيَ يَوۡمَئِذٖ وَاهِيَةٞ
Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.
阿拉伯语经注:
وَٱلۡمَلَكُ عَلَىٰٓ أَرۡجَآئِهَاۚ وَيَحۡمِلُ عَرۡشَ رَبِّكَ فَوۡقَهُمۡ يَوۡمَئِذٖ ثَمَٰنِيَةٞ
Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.
阿拉伯语经注:
يَوۡمَئِذٖ تُعۡرَضُونَ لَا تَخۡفَىٰ مِنكُمۡ خَافِيَةٞ
Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.
阿拉伯语经注:
فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ فَيَقُولُ هَآؤُمُ ٱقۡرَءُواْ كِتَٰبِيَهۡ
Basi ama atakayepewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!
阿拉伯语经注:
إِنِّي ظَنَنتُ أَنِّي مُلَٰقٍ حِسَابِيَهۡ
Hakika nilijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.
阿拉伯语经注:
فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ
Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza.
阿拉伯语经注:
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ
Katika Bustani ya juu.
阿拉伯语经注:
قُطُوفُهَا دَانِيَةٞ
Matunda yake ya karibu.
阿拉伯语经注:
كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَآ أَسۡلَفۡتُمۡ فِي ٱلۡأَيَّامِ ٱلۡخَالِيَةِ
Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyotanguliza katika siku zilizopita.
阿拉伯语经注:
وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِشِمَالِهِۦ فَيَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي لَمۡ أُوتَ كِتَٰبِيَهۡ
Na ama atakayepewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingelipewa kitabu changu!
阿拉伯语经注:
وَلَمۡ أَدۡرِ مَا حِسَابِيَهۡ
Wala nisingelijua nini hisabu yangu.
阿拉伯语经注:
يَٰلَيۡتَهَا كَانَتِ ٱلۡقَاضِيَةَ
Laiti mauti ndiyo yangelikuwa ya kunimaliza kabisa.
阿拉伯语经注:
مَآ أَغۡنَىٰ عَنِّي مَالِيَهۡۜ
Mali yangu hayakunifaa kitu.
阿拉伯语经注:
هَلَكَ عَنِّي سُلۡطَٰنِيَهۡ
Madaraka yangu yamenipotea.
阿拉伯语经注:
خُذُوهُ فَغُلُّوهُ
(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!
阿拉伯语经注:
ثُمَّ ٱلۡجَحِيمَ صَلُّوهُ
Kisha mtupeni Motoni!
阿拉伯语经注:
ثُمَّ فِي سِلۡسِلَةٖ ذَرۡعُهَا سَبۡعُونَ ذِرَاعٗا فَٱسۡلُكُوهُ
Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabini!
阿拉伯语经注:
إِنَّهُۥ كَانَ لَا يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ ٱلۡعَظِيمِ
Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu.
阿拉伯语经注:
وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ
Wala hahimizi kulisha masikini.
阿拉伯语经注:
فَلَيۡسَ لَهُ ٱلۡيَوۡمَ هَٰهُنَا حَمِيمٞ
Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu.
阿拉伯语经注:
وَلَا طَعَامٌ إِلَّا مِنۡ غِسۡلِينٖ
Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.
阿拉伯语经注:
لَّا يَأۡكُلُهُۥٓ إِلَّا ٱلۡخَٰطِـُٔونَ
Chakula hicho hawakili ila wakosefu.
阿拉伯语经注:
فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَا تُبۡصِرُونَ
Basi ninaapa kwa mnavyoviona.
阿拉伯语经注:
وَمَا لَا تُبۡصِرُونَ
Na msivyoviona.
阿拉伯语经注:
إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ
Kwa hakika hii ni kauli iliyoletwa na Mjumbe mwenye heshima.
阿拉伯语经注:
وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَاعِرٖۚ قَلِيلٗا مَّا تُؤۡمِنُونَ
Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayoyaamini.
阿拉伯语经注:
وَلَا بِقَوۡلِ كَاهِنٖۚ قَلِيلٗا مَّا تَذَكَّرُونَ
Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayoyakumbuka.
阿拉伯语经注:
تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
阿拉伯语经注:
وَلَوۡ تَقَوَّلَ عَلَيۡنَا بَعۡضَ ٱلۡأَقَاوِيلِ
Na lau kama angelituzulia baadhi ya maneno tu.
阿拉伯语经注:
لَأَخَذۡنَا مِنۡهُ بِٱلۡيَمِينِ
Bila ya shaka tungelimshika kwa mkono wa kulia.
阿拉伯语经注:
ثُمَّ لَقَطَعۡنَا مِنۡهُ ٱلۡوَتِينَ
Kisha kwa hakika tungelimkata mshipa mkubwa wa moyo!
阿拉伯语经注:
فَمَا مِنكُم مِّنۡ أَحَدٍ عَنۡهُ حَٰجِزِينَ
Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeliweza kutuzuia.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّهُۥ لَتَذۡكِرَةٞ لِّلۡمُتَّقِينَ
Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wacha Mungu.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّا لَنَعۡلَمُ أَنَّ مِنكُم مُّكَذِّبِينَ
Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanaokadhibisha.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّهُۥ لَحَسۡرَةٌ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanaokataa.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّهُۥ لَحَقُّ ٱلۡيَقِينِ
Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.
阿拉伯语经注:
فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 章: 哈格
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 拉瓦德翻译中心。 - 译解目录

由拉瓦德翻译中心团队与拉布瓦 الدعوة协会和伊斯兰内容服务协会合作翻译。

关闭