Check out the new design

Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassarar Sawahil - Cibiyar fassara ta Ruwwad * - Teburin Bayani kan wasu Fassarori


Fassarar Ma'anoni Sura: Al'najm   Aya:

An-Najm

وَٱلنَّجۡمِ إِذَا هَوَىٰ
Ninaapa kwa nyota inapotua.
Tafsiran larabci:
مَا ضَلَّ صَاحِبُكُمۡ وَمَا غَوَىٰ
Mwenzenu huyu hakupotea, wala hakukosea.
Tafsiran larabci:
وَمَا يَنطِقُ عَنِ ٱلۡهَوَىٰٓ
Wala hatamki kwa matamanio.
Tafsiran larabci:
إِنۡ هُوَ إِلَّا وَحۡيٞ يُوحَىٰ
Hayakuwa haya ila ni ufunuo uliofunuliwa.
Tafsiran larabci:
عَلَّمَهُۥ شَدِيدُ ٱلۡقُوَىٰ
Amemfundisha aliye Mwingi wa nguvu.
Tafsiran larabci:
ذُو مِرَّةٖ فَٱسۡتَوَىٰ
Mwenye kutua, akatulia.
Tafsiran larabci:
وَهُوَ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡأَعۡلَىٰ
Naye yuko juu kabisa upeo wa macho.
Tafsiran larabci:
ثُمَّ دَنَا فَتَدَلَّىٰ
Kisha akakaribia na akateremka.
Tafsiran larabci:
فَكَانَ قَابَ قَوۡسَيۡنِ أَوۡ أَدۡنَىٰ
Akawa ni kama baina ya mipinde miwili, au karibu zaidi.
Tafsiran larabci:
فَأَوۡحَىٰٓ إِلَىٰ عَبۡدِهِۦ مَآ أَوۡحَىٰ
Akamfunulia mja wake (Mwenyezi Mungu) alichomfunulia.
Tafsiran larabci:
مَا كَذَبَ ٱلۡفُؤَادُ مَا رَأَىٰٓ
Moyo haukusema uwongo uliyoyaona.
Tafsiran larabci:
أَفَتُمَٰرُونَهُۥ عَلَىٰ مَا يَرَىٰ
Je, mnabishana naye kwa aliyoyaona?
Tafsiran larabci:
وَلَقَدۡ رَءَاهُ نَزۡلَةً أُخۡرَىٰ
Na akamwona mara nyingine.
Tafsiran larabci:
عِندَ سِدۡرَةِ ٱلۡمُنتَهَىٰ
Penye Mkunazi wa mwisho.
Tafsiran larabci:
عِندَهَا جَنَّةُ ٱلۡمَأۡوَىٰٓ
Karibu yake ndiyo ipo Bustani ya mbinguni inayokaliwa.
Tafsiran larabci:
إِذۡ يَغۡشَى ٱلسِّدۡرَةَ مَا يَغۡشَىٰ
Kilipoufunika huo Mkunazi hicho kilichoufunika.
Tafsiran larabci:
مَا زَاغَ ٱلۡبَصَرُ وَمَا طَغَىٰ
Jicho halikuhangaika wala halikuruka mpaka.
Tafsiran larabci:
لَقَدۡ رَأَىٰ مِنۡ ءَايَٰتِ رَبِّهِ ٱلۡكُبۡرَىٰٓ
Kwa yakini aliona katika Ishara kubwa kabisa za Mola wake Mlezi.
Tafsiran larabci:
أَفَرَءَيۡتُمُ ٱللَّٰتَ وَٱلۡعُزَّىٰ
Je, mmemuona Lata na Uzza?
Tafsiran larabci:
وَمَنَوٰةَ ٱلثَّالِثَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰٓ
Na Manaat, mwingine wa tatu?
Tafsiran larabci:
أَلَكُمُ ٱلذَّكَرُ وَلَهُ ٱلۡأُنثَىٰ
Je, nyinyi mnao wana wanaume na Yeye ndio awe na wanawake?
Tafsiran larabci:
تِلۡكَ إِذٗا قِسۡمَةٞ ضِيزَىٰٓ
Huo ni mgawanyo wa dhuluma!
Tafsiran larabci:
إِنۡ هِيَ إِلَّآ أَسۡمَآءٞ سَمَّيۡتُمُوهَآ أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُم مَّآ أَنزَلَ ٱللَّهُ بِهَا مِن سُلۡطَٰنٍۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَمَا تَهۡوَى ٱلۡأَنفُسُۖ وَلَقَدۡ جَآءَهُم مِّن رَّبِّهِمُ ٱلۡهُدَىٰٓ
Hayo hayakuwa ila ni majina mliyowapa nyinyi na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuleta uthibitisho wowote juu ya hayo. Hawafuati ila dhana tu na kipendacho nafsi. Na kwa yakini uwongofu ulikwisha wafikia kutoka kwa Mola wao Mlezi.
Tafsiran larabci:
أَمۡ لِلۡإِنسَٰنِ مَا تَمَنَّىٰ
Ati mtu anakipata kila anachokitamani?
Tafsiran larabci:
فَلِلَّهِ ٱلۡأٓخِرَةُ وَٱلۡأُولَىٰ
Mwenyezi Mungu tu ndiye Mwenye dunia na Akhera.
Tafsiran larabci:
۞ وَكَم مِّن مَّلَكٖ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ لَا تُغۡنِي شَفَٰعَتُهُمۡ شَيۡـًٔا إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ أَن يَأۡذَنَ ٱللَّهُ لِمَن يَشَآءُ وَيَرۡضَىٰٓ
Na wako Malaika wangapi mbinguni, ambao uombezi wao hautafaa chochote isipokuwa baada ya Mwenyezi Mungu kutoa idhini kwa amtakaye na kumridhia.
Tafsiran larabci:
إِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ لَيُسَمُّونَ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ تَسۡمِيَةَ ٱلۡأُنثَىٰ
Hakika wale wasioamini Akhera bila ya shaka wao ndio wanawaita Malaika kwa majina ya kike.
Tafsiran larabci:
وَمَا لَهُم بِهِۦ مِنۡ عِلۡمٍۖ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّۖ وَإِنَّ ٱلظَّنَّ لَا يُغۡنِي مِنَ ٱلۡحَقِّ شَيۡـٔٗا
Nao hawana elimu yoyote kwa hayo isipokuwa wanafuata dhana tu. Na dhana haisaidii chochote mbele ya haki.
Tafsiran larabci:
فَأَعۡرِضۡ عَن مَّن تَوَلَّىٰ عَن ذِكۡرِنَا وَلَمۡ يُرِدۡ إِلَّا ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا
Basi mwachilie mbali anayeupa kisogo ukumbusho wetu, na wala hataki ila maisha ya dunia.
Tafsiran larabci:
ذَٰلِكَ مَبۡلَغُهُم مِّنَ ٱلۡعِلۡمِۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِمَنِ ٱهۡتَدَىٰ
Huo ndio mwisho wao wa elimu. Hakika Mola wako Mlezi ndiye anayemjua zaidi mwenye kuipotea njia yake, na Yeye ndiye anayemjua zaidi mwenye kuongoka.
Tafsiran larabci:
وَلِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِ لِيَجۡزِيَ ٱلَّذِينَ أَسَٰٓـُٔواْ بِمَا عَمِلُواْ وَيَجۡزِيَ ٱلَّذِينَ أَحۡسَنُواْ بِٱلۡحُسۡنَى
Ni vya Mwenyezi Mungu vyote vilivyomo mbinguni na vilivyomo katika ardhi, ili awalipe wale waliotenda ubaya kwa waliyoyatenda, na wale waliotenda mema awalipe mema.
Tafsiran larabci:
ٱلَّذِينَ يَجۡتَنِبُونَ كَبَٰٓئِرَ ٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡفَوَٰحِشَ إِلَّا ٱللَّمَمَۚ إِنَّ رَبَّكَ وَٰسِعُ ٱلۡمَغۡفِرَةِۚ هُوَ أَعۡلَمُ بِكُمۡ إِذۡ أَنشَأَكُم مِّنَ ٱلۡأَرۡضِ وَإِذۡ أَنتُمۡ أَجِنَّةٞ فِي بُطُونِ أُمَّهَٰتِكُمۡۖ فَلَا تُزَكُّوٓاْ أَنفُسَكُمۡۖ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَنِ ٱتَّقَىٰٓ
Ambao wanajiweka mbali na madhambi makuu na vitendo vichafu, isipokuwa makosa hafifu. Hakika Mola wako Mlezi ni Mkunjufu wa maghfira, naye anakujueni sana tangu alipokuumbeni kutoka kwenye ardhi, na mlipokuwa mimba matumboni mwa mama zenu. Basi msijione watakatifu. Yeye anamjua sana mwenye kujikinga akawa mbali na maovu.
Tafsiran larabci:
أَفَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي تَوَلَّىٰ
Je, umemwona yule aliyegeuka akaenda zake?
Tafsiran larabci:
وَأَعۡطَىٰ قَلِيلٗا وَأَكۡدَىٰٓ
Na akapeana kidogo, kisha akajizuia?
Tafsiran larabci:
أَعِندَهُۥ عِلۡمُ ٱلۡغَيۡبِ فَهُوَ يَرَىٰٓ
Je, anayo huyo elimu ya ghaibu, basi ndiyo anaona?
Tafsiran larabci:
أَمۡ لَمۡ يُنَبَّأۡ بِمَا فِي صُحُفِ مُوسَىٰ
Au hakuambiwa yaliyomo katika Vitabu vya Musa?
Tafsiran larabci:
وَإِبۡرَٰهِيمَ ٱلَّذِي وَفَّىٰٓ
Na vya Ibrahimu aliyetimiza ahadi?
Tafsiran larabci:
أَلَّا تَزِرُ وَازِرَةٞ وِزۡرَ أُخۡرَىٰ
Ya kwamba hakika nafsi iliyobeba madhambi haibebi madhambi ya mwengine?
Tafsiran larabci:
وَأَن لَّيۡسَ لِلۡإِنسَٰنِ إِلَّا مَا سَعَىٰ
Na ya kwamba hatapata mtu ila aliyoyafanya mwenyewe?
Tafsiran larabci:
وَأَنَّ سَعۡيَهُۥ سَوۡفَ يُرَىٰ
Na kwamba vitendo vyake vitaonekana?
Tafsiran larabci:
ثُمَّ يُجۡزَىٰهُ ٱلۡجَزَآءَ ٱلۡأَوۡفَىٰ
Kisha ndio atalipwa malipo yake kwa hayo kwa ukamilifu.
Tafsiran larabci:
وَأَنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلۡمُنتَهَىٰ
Na kwamba kwa Mola wako Mlezi ndiyo mwisho.
Tafsiran larabci:
وَأَنَّهُۥ هُوَ أَضۡحَكَ وَأَبۡكَىٰ
Na kwamba Yeye ndiye anayeleta kicheko na kilio.
Tafsiran larabci:
وَأَنَّهُۥ هُوَ أَمَاتَ وَأَحۡيَا
Na kwamba Yeye ndiye anayefisha na kuhuisha.
Tafsiran larabci:
وَأَنَّهُۥ خَلَقَ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰ
Na kwamba Yeye ndiye aliyeumba jozi, dume na jike
Tafsiran larabci:
مِن نُّطۡفَةٍ إِذَا تُمۡنَىٰ
Kutokana na mbegu ya uzazi inapomiminwa.
Tafsiran larabci:
وَأَنَّ عَلَيۡهِ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰ
Na kwamba ni juu yake ufufuo mwengine.
Tafsiran larabci:
وَأَنَّهُۥ هُوَ أَغۡنَىٰ وَأَقۡنَىٰ
Na kwamba ni Yeye ndiye anayetosheleza na kukinaisha.
Tafsiran larabci:
وَأَنَّهُۥ هُوَ رَبُّ ٱلشِّعۡرَىٰ
Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii'ra.
Tafsiran larabci:
وَأَنَّهُۥٓ أَهۡلَكَ عَادًا ٱلۡأُولَىٰ
Na kwamba Yeye ndiye aliyewaangamiza 'Adi wa kwanza.
Tafsiran larabci:
وَثَمُودَاْ فَمَآ أَبۡقَىٰ
Na Thamudi hakuwabakisha.
Tafsiran larabci:
وَقَوۡمَ نُوحٖ مِّن قَبۡلُۖ إِنَّهُمۡ كَانُواْ هُمۡ أَظۡلَمَ وَأَطۡغَىٰ
Na kabla yao kaumu ya Nuhu. Na hao hakika walikuwa ni madhalimu zaidi, na waovu zaidi.
Tafsiran larabci:
وَٱلۡمُؤۡتَفِكَةَ أَهۡوَىٰ
Na miji iliyopinduliwa, ni Yeye aliyeipindua.
Tafsiran larabci:
فَغَشَّىٰهَا مَا غَشَّىٰ
Vikaifunika vilivyofunika.
Tafsiran larabci:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكَ تَتَمَارَىٰ
Basi neema gani ya Mola wako Mlezi unayoifanyia shaka?
Tafsiran larabci:
هَٰذَا نَذِيرٞ مِّنَ ٱلنُّذُرِ ٱلۡأُولَىٰٓ
Hili ni onyo katika maonyo yale yale ya zamani.
Tafsiran larabci:
أَزِفَتِ ٱلۡأٓزِفَةُ
Kiyama kimekaribia!
Tafsiran larabci:
لَيۡسَ لَهَا مِن دُونِ ٱللَّهِ كَاشِفَةٌ
Hapana wa kukifichua isipokuwa Mwenyezi Mungu.
Tafsiran larabci:
أَفَمِنۡ هَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ تَعۡجَبُونَ
Je, mnayastaajabia maneno haya?
Tafsiran larabci:
وَتَضۡحَكُونَ وَلَا تَبۡكُونَ
Na mnacheka, wala hamlii?
Tafsiran larabci:
وَأَنتُمۡ سَٰمِدُونَ
Nanyi mmeghafilika?
Tafsiran larabci:
فَٱسۡجُدُواْۤ لِلَّهِۤ وَٱعۡبُدُواْ۩
Basi msujudieni Mwenyezi Mungu, na mumuabudu.
Tafsiran larabci:
 
Fassarar Ma'anoni Sura: Al'najm
Teburin Jerin Sunayen Surori Lambar shafi
 
Fassarar Ma'anonin Alqura'ni - Fassarar Sawahil - Cibiyar fassara ta Ruwwad - Teburin Bayani kan wasu Fassarori

Fassara ta wani gungu na cibiyar fassara ta Ruwwad tare da haɗin gwiwar Ƙungiyar Da'awa ta Rabwah da Ƙungiyar Hidimar Abun ciki na Musulunci a harsuna.

Rufewa