Check out the new design

क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - सवाहिली अनुवाद - अनुवाद अग्रदूत केंद्र * - अनुवादों की सूची


अर्थों का अनुवाद सूरा: अन्-नज्म   आयत:

An-Najm

وَٱلنَّجۡمِ إِذَا هَوَىٰ
Ninaapa kwa nyota inapotua.
अरबी तफ़सीरें:
مَا ضَلَّ صَاحِبُكُمۡ وَمَا غَوَىٰ
Mwenzenu huyu hakupotea, wala hakukosea.
अरबी तफ़सीरें:
وَمَا يَنطِقُ عَنِ ٱلۡهَوَىٰٓ
Wala hatamki kwa matamanio.
अरबी तफ़सीरें:
إِنۡ هُوَ إِلَّا وَحۡيٞ يُوحَىٰ
Hayakuwa haya ila ni ufunuo uliofunuliwa.
अरबी तफ़सीरें:
عَلَّمَهُۥ شَدِيدُ ٱلۡقُوَىٰ
Amemfundisha aliye Mwingi wa nguvu.
अरबी तफ़सीरें:
ذُو مِرَّةٖ فَٱسۡتَوَىٰ
Mwenye kutua, akatulia.
अरबी तफ़सीरें:
وَهُوَ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡأَعۡلَىٰ
Naye yuko juu kabisa upeo wa macho.
अरबी तफ़सीरें:
ثُمَّ دَنَا فَتَدَلَّىٰ
Kisha akakaribia na akateremka.
अरबी तफ़सीरें:
فَكَانَ قَابَ قَوۡسَيۡنِ أَوۡ أَدۡنَىٰ
Akawa ni kama baina ya mipinde miwili, au karibu zaidi.
अरबी तफ़सीरें:
فَأَوۡحَىٰٓ إِلَىٰ عَبۡدِهِۦ مَآ أَوۡحَىٰ
Akamfunulia mja wake (Mwenyezi Mungu) alichomfunulia.
अरबी तफ़सीरें:
مَا كَذَبَ ٱلۡفُؤَادُ مَا رَأَىٰٓ
Moyo haukusema uwongo uliyoyaona.
अरबी तफ़सीरें:
أَفَتُمَٰرُونَهُۥ عَلَىٰ مَا يَرَىٰ
Je, mnabishana naye kwa aliyoyaona?
अरबी तफ़सीरें:
وَلَقَدۡ رَءَاهُ نَزۡلَةً أُخۡرَىٰ
Na akamwona mara nyingine.
अरबी तफ़सीरें:
عِندَ سِدۡرَةِ ٱلۡمُنتَهَىٰ
Penye Mkunazi wa mwisho.
अरबी तफ़सीरें:
عِندَهَا جَنَّةُ ٱلۡمَأۡوَىٰٓ
Karibu yake ndiyo ipo Bustani ya mbinguni inayokaliwa.
अरबी तफ़सीरें:
إِذۡ يَغۡشَى ٱلسِّدۡرَةَ مَا يَغۡشَىٰ
Kilipoufunika huo Mkunazi hicho kilichoufunika.
अरबी तफ़सीरें:
مَا زَاغَ ٱلۡبَصَرُ وَمَا طَغَىٰ
Jicho halikuhangaika wala halikuruka mpaka.
अरबी तफ़सीरें:
لَقَدۡ رَأَىٰ مِنۡ ءَايَٰتِ رَبِّهِ ٱلۡكُبۡرَىٰٓ
Kwa yakini aliona katika Ishara kubwa kabisa za Mola wake Mlezi.
अरबी तफ़सीरें:
أَفَرَءَيۡتُمُ ٱللَّٰتَ وَٱلۡعُزَّىٰ
Je, mmemuona Lata na Uzza?
अरबी तफ़सीरें:
وَمَنَوٰةَ ٱلثَّالِثَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰٓ
Na Manaat, mwingine wa tatu?
अरबी तफ़सीरें:
أَلَكُمُ ٱلذَّكَرُ وَلَهُ ٱلۡأُنثَىٰ
Je, nyinyi mnao wana wanaume na Yeye ndio awe na wanawake?
अरबी तफ़सीरें:
تِلۡكَ إِذٗا قِسۡمَةٞ ضِيزَىٰٓ
Huo ni mgawanyo wa dhuluma!
अरबी तफ़सीरें:
إِنۡ هِيَ إِلَّآ أَسۡمَآءٞ سَمَّيۡتُمُوهَآ أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُم مَّآ أَنزَلَ ٱللَّهُ بِهَا مِن سُلۡطَٰنٍۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَمَا تَهۡوَى ٱلۡأَنفُسُۖ وَلَقَدۡ جَآءَهُم مِّن رَّبِّهِمُ ٱلۡهُدَىٰٓ
Hayo hayakuwa ila ni majina mliyowapa nyinyi na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuleta uthibitisho wowote juu ya hayo. Hawafuati ila dhana tu na kipendacho nafsi. Na kwa yakini uwongofu ulikwisha wafikia kutoka kwa Mola wao Mlezi.
अरबी तफ़सीरें:
أَمۡ لِلۡإِنسَٰنِ مَا تَمَنَّىٰ
Ati mtu anakipata kila anachokitamani?
अरबी तफ़सीरें:
فَلِلَّهِ ٱلۡأٓخِرَةُ وَٱلۡأُولَىٰ
Mwenyezi Mungu tu ndiye Mwenye dunia na Akhera.
अरबी तफ़सीरें:
۞ وَكَم مِّن مَّلَكٖ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ لَا تُغۡنِي شَفَٰعَتُهُمۡ شَيۡـًٔا إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ أَن يَأۡذَنَ ٱللَّهُ لِمَن يَشَآءُ وَيَرۡضَىٰٓ
Na wako Malaika wangapi mbinguni, ambao uombezi wao hautafaa chochote isipokuwa baada ya Mwenyezi Mungu kutoa idhini kwa amtakaye na kumridhia.
अरबी तफ़सीरें:
إِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ لَيُسَمُّونَ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ تَسۡمِيَةَ ٱلۡأُنثَىٰ
Hakika wale wasioamini Akhera bila ya shaka wao ndio wanawaita Malaika kwa majina ya kike.
अरबी तफ़सीरें:
وَمَا لَهُم بِهِۦ مِنۡ عِلۡمٍۖ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّۖ وَإِنَّ ٱلظَّنَّ لَا يُغۡنِي مِنَ ٱلۡحَقِّ شَيۡـٔٗا
Nao hawana elimu yoyote kwa hayo isipokuwa wanafuata dhana tu. Na dhana haisaidii chochote mbele ya haki.
अरबी तफ़सीरें:
فَأَعۡرِضۡ عَن مَّن تَوَلَّىٰ عَن ذِكۡرِنَا وَلَمۡ يُرِدۡ إِلَّا ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا
Basi mwachilie mbali anayeupa kisogo ukumbusho wetu, na wala hataki ila maisha ya dunia.
अरबी तफ़सीरें:
ذَٰلِكَ مَبۡلَغُهُم مِّنَ ٱلۡعِلۡمِۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِمَنِ ٱهۡتَدَىٰ
Huo ndio mwisho wao wa elimu. Hakika Mola wako Mlezi ndiye anayemjua zaidi mwenye kuipotea njia yake, na Yeye ndiye anayemjua zaidi mwenye kuongoka.
अरबी तफ़सीरें:
وَلِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِ لِيَجۡزِيَ ٱلَّذِينَ أَسَٰٓـُٔواْ بِمَا عَمِلُواْ وَيَجۡزِيَ ٱلَّذِينَ أَحۡسَنُواْ بِٱلۡحُسۡنَى
Ni vya Mwenyezi Mungu vyote vilivyomo mbinguni na vilivyomo katika ardhi, ili awalipe wale waliotenda ubaya kwa waliyoyatenda, na wale waliotenda mema awalipe mema.
अरबी तफ़सीरें:
ٱلَّذِينَ يَجۡتَنِبُونَ كَبَٰٓئِرَ ٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡفَوَٰحِشَ إِلَّا ٱللَّمَمَۚ إِنَّ رَبَّكَ وَٰسِعُ ٱلۡمَغۡفِرَةِۚ هُوَ أَعۡلَمُ بِكُمۡ إِذۡ أَنشَأَكُم مِّنَ ٱلۡأَرۡضِ وَإِذۡ أَنتُمۡ أَجِنَّةٞ فِي بُطُونِ أُمَّهَٰتِكُمۡۖ فَلَا تُزَكُّوٓاْ أَنفُسَكُمۡۖ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَنِ ٱتَّقَىٰٓ
Ambao wanajiweka mbali na madhambi makuu na vitendo vichafu, isipokuwa makosa hafifu. Hakika Mola wako Mlezi ni Mkunjufu wa maghfira, naye anakujueni sana tangu alipokuumbeni kutoka kwenye ardhi, na mlipokuwa mimba matumboni mwa mama zenu. Basi msijione watakatifu. Yeye anamjua sana mwenye kujikinga akawa mbali na maovu.
अरबी तफ़सीरें:
أَفَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي تَوَلَّىٰ
Je, umemwona yule aliyegeuka akaenda zake?
अरबी तफ़सीरें:
وَأَعۡطَىٰ قَلِيلٗا وَأَكۡدَىٰٓ
Na akapeana kidogo, kisha akajizuia?
अरबी तफ़सीरें:
أَعِندَهُۥ عِلۡمُ ٱلۡغَيۡبِ فَهُوَ يَرَىٰٓ
Je, anayo huyo elimu ya ghaibu, basi ndiyo anaona?
अरबी तफ़सीरें:
أَمۡ لَمۡ يُنَبَّأۡ بِمَا فِي صُحُفِ مُوسَىٰ
Au hakuambiwa yaliyomo katika Vitabu vya Musa?
अरबी तफ़सीरें:
وَإِبۡرَٰهِيمَ ٱلَّذِي وَفَّىٰٓ
Na vya Ibrahimu aliyetimiza ahadi?
अरबी तफ़सीरें:
أَلَّا تَزِرُ وَازِرَةٞ وِزۡرَ أُخۡرَىٰ
Ya kwamba hakika nafsi iliyobeba madhambi haibebi madhambi ya mwengine?
अरबी तफ़सीरें:
وَأَن لَّيۡسَ لِلۡإِنسَٰنِ إِلَّا مَا سَعَىٰ
Na ya kwamba hatapata mtu ila aliyoyafanya mwenyewe?
अरबी तफ़सीरें:
وَأَنَّ سَعۡيَهُۥ سَوۡفَ يُرَىٰ
Na kwamba vitendo vyake vitaonekana?
अरबी तफ़सीरें:
ثُمَّ يُجۡزَىٰهُ ٱلۡجَزَآءَ ٱلۡأَوۡفَىٰ
Kisha ndio atalipwa malipo yake kwa hayo kwa ukamilifu.
अरबी तफ़सीरें:
وَأَنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلۡمُنتَهَىٰ
Na kwamba kwa Mola wako Mlezi ndiyo mwisho.
अरबी तफ़सीरें:
وَأَنَّهُۥ هُوَ أَضۡحَكَ وَأَبۡكَىٰ
Na kwamba Yeye ndiye anayeleta kicheko na kilio.
अरबी तफ़सीरें:
وَأَنَّهُۥ هُوَ أَمَاتَ وَأَحۡيَا
Na kwamba Yeye ndiye anayefisha na kuhuisha.
अरबी तफ़सीरें:
وَأَنَّهُۥ خَلَقَ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰ
Na kwamba Yeye ndiye aliyeumba jozi, dume na jike
अरबी तफ़सीरें:
مِن نُّطۡفَةٍ إِذَا تُمۡنَىٰ
Kutokana na mbegu ya uzazi inapomiminwa.
अरबी तफ़सीरें:
وَأَنَّ عَلَيۡهِ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰ
Na kwamba ni juu yake ufufuo mwengine.
अरबी तफ़सीरें:
وَأَنَّهُۥ هُوَ أَغۡنَىٰ وَأَقۡنَىٰ
Na kwamba ni Yeye ndiye anayetosheleza na kukinaisha.
अरबी तफ़सीरें:
وَأَنَّهُۥ هُوَ رَبُّ ٱلشِّعۡرَىٰ
Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii'ra.
अरबी तफ़सीरें:
وَأَنَّهُۥٓ أَهۡلَكَ عَادًا ٱلۡأُولَىٰ
Na kwamba Yeye ndiye aliyewaangamiza 'Adi wa kwanza.
अरबी तफ़सीरें:
وَثَمُودَاْ فَمَآ أَبۡقَىٰ
Na Thamudi hakuwabakisha.
अरबी तफ़सीरें:
وَقَوۡمَ نُوحٖ مِّن قَبۡلُۖ إِنَّهُمۡ كَانُواْ هُمۡ أَظۡلَمَ وَأَطۡغَىٰ
Na kabla yao kaumu ya Nuhu. Na hao hakika walikuwa ni madhalimu zaidi, na waovu zaidi.
अरबी तफ़सीरें:
وَٱلۡمُؤۡتَفِكَةَ أَهۡوَىٰ
Na miji iliyopinduliwa, ni Yeye aliyeipindua.
अरबी तफ़सीरें:
فَغَشَّىٰهَا مَا غَشَّىٰ
Vikaifunika vilivyofunika.
अरबी तफ़सीरें:
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكَ تَتَمَارَىٰ
Basi neema gani ya Mola wako Mlezi unayoifanyia shaka?
अरबी तफ़सीरें:
هَٰذَا نَذِيرٞ مِّنَ ٱلنُّذُرِ ٱلۡأُولَىٰٓ
Hili ni onyo katika maonyo yale yale ya zamani.
अरबी तफ़सीरें:
أَزِفَتِ ٱلۡأٓزِفَةُ
Kiyama kimekaribia!
अरबी तफ़सीरें:
لَيۡسَ لَهَا مِن دُونِ ٱللَّهِ كَاشِفَةٌ
Hapana wa kukifichua isipokuwa Mwenyezi Mungu.
अरबी तफ़सीरें:
أَفَمِنۡ هَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ تَعۡجَبُونَ
Je, mnayastaajabia maneno haya?
अरबी तफ़सीरें:
وَتَضۡحَكُونَ وَلَا تَبۡكُونَ
Na mnacheka, wala hamlii?
अरबी तफ़सीरें:
وَأَنتُمۡ سَٰمِدُونَ
Nanyi mmeghafilika?
अरबी तफ़सीरें:
فَٱسۡجُدُواْۤ لِلَّهِۤ وَٱعۡبُدُواْ۩
Basi msujudieni Mwenyezi Mungu, na mumuabudu.
अरबी तफ़सीरें:
 
अर्थों का अनुवाद सूरा: अन्-नज्म
सूरों की सूची पृष्ठ संख्या
 
क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - सवाहिली अनुवाद - अनुवाद अग्रदूत केंद्र - अनुवादों की सूची

अनुवाद अनुवाद अग्रदूत केंद्र द्वारा नियुक्त एक समूह ने अल-रब्वाह आह्वान संस्था और भाषाओं में इस्लामिक सामग्री की सेवा करने वाली संस्था के सहयोग से किया है।

बंद करें