Check out the new design

क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - स्वाहीली अनुवाद - अब्दुल्लाह मुहम्मद तथा नासिर ख़मीस * - अनुवादों की सूची


अर्थों का अनुवाद सूरा: अन्-नह़्ल   आयत:
لِيَكۡفُرُواْ بِمَآ ءَاتَيۡنَٰهُمۡۚ فَتَمَتَّعُواْ فَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَ
Ili wapate kuzikanusha neema zetu kwao, na miongoni mwazo ni kuondolewa matatizo. Basi jistarehesheni na ulimwengu wenu, nao mwisho wake ni kutoweka, hapo mtajua mwisho wa ukanushaji wenu na uasi wenu.
अरबी तफ़सीरें:
وَيَجۡعَلُونَ لِمَا لَا يَعۡلَمُونَ نَصِيبٗا مِّمَّا رَزَقۡنَٰهُمۡۗ تَٱللَّهِ لَتُسۡـَٔلُنَّ عَمَّا كُنتُمۡ تَفۡتَرُونَ
Na miongoni mwa uovu wa matendo yao ni kwamba wao wanawatengea masanamu waliowafanya ni waungu, wasiojua chochote na wasionufaisha wala kudhuru, sehemu ya mali zao walizoruzukiwa na Mwenyezi Mungu ili kujisongeza kwao. Ninaapa kwa Mwenyezi Mungu! Mtaulizwa tena mtaulizwa Siku ya Kiyama kuhusu yale ya urongo ambayo mlikuwa mkimzulia Mwenyezi mungu.
अरबी तफ़सीरें:
وَيَجۡعَلُونَ لِلَّهِ ٱلۡبَنَٰتِ سُبۡحَٰنَهُۥ وَلَهُم مَّا يَشۡتَهُونَ
Na makafiri wanamsingizia Mwenyezi Mungu kuwa ana watoto wa kike na huwa wakisema, «Malaika ni watoto wa kike wa Mwenyezi Mungu». Ameepukana Mwenyezi Mungu na neno lao. Na wanajichukulia wao wenyewe watoto wa kiume wanaowapenda.
अरबी तफ़सीरें:
وَإِذَا بُشِّرَ أَحَدُهُم بِٱلۡأُنثَىٰ ظَلَّ وَجۡهُهُۥ مُسۡوَدّٗا وَهُوَ كَظِيمٞ
Na pindi anapokuja mwenye kumpasha habari mmoja wao ya kuzaliwa mtoto wa kike, uso wake hapohapo unageuka mweusi, kwa kuyachukia aliyoyasikia, na akajawa na hasira na huzuni.
अरबी तफ़सीरें:
يَتَوَٰرَىٰ مِنَ ٱلۡقَوۡمِ مِن سُوٓءِ مَا بُشِّرَ بِهِۦٓۚ أَيُمۡسِكُهُۥ عَلَىٰ هُونٍ أَمۡ يَدُسُّهُۥ فِي ٱلتُّرَابِۗ أَلَا سَآءَ مَا يَحۡكُمُونَ
Anajificha kwa kuchukia asionekane na watu wake, akiona aibu na kuingiwa na huzuni kwa habari iliyomchukiza ya kuzaliwa mtoto wa kike, huku akiwa ametunduwaa juu ya tukio la mtoto huyo aliyezaliwa: je, amuache kuishi kwenye hali ya unyonge na utwevu au amzike mchangani akiwa hai? Jueni mtanabahi kwamba ni uamuzi mbaya mno wanaouamua ya kuwafanya watoto wa kike ni wa Mwenyezi Mungu na watoto wakiume ni wao.
अरबी तफ़सीरें:
لِلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ مَثَلُ ٱلسَّوۡءِۖ وَلِلَّهِ ٱلۡمَثَلُ ٱلۡأَعۡلَىٰۚ وَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ
Wale wasioiamini Akhera na wasiofanya matendo ya kuwafaa huko wana sifa mbaya za ulemevu, uhitaji, ujinga na ukafiri, na Mwenyezi Mungu Ana sifa tukufu za ukamilifu, kujitosheleza na viumbe Vyake. Na Yeye Ndiye Mshindi katika mamlaka Yake, ni Mwenye hekima katika uendeshaji Wake.
अरबी तफ़सीरें:
وَلَوۡ يُؤَاخِذُ ٱللَّهُ ٱلنَّاسَ بِظُلۡمِهِم مَّا تَرَكَ عَلَيۡهَا مِن دَآبَّةٖ وَلَٰكِن يُؤَخِّرُهُمۡ إِلَىٰٓ أَجَلٖ مُّسَمّٗىۖ فَإِذَا جَآءَ أَجَلُهُمۡ لَا يَسۡتَـٔۡخِرُونَ سَاعَةٗ وَلَا يَسۡتَقۡدِمُونَ
Lau kwamba Mwenyezi Mungu Anawapatiliza watu kwa ukafiri wao na uzushi wao, Hangalimuacha juu ya ardhi mtu yoyote mwenye kutembea, lakini Anawabakisha mpaka wakati uliopanagwa, nao ni mwisho wa muda wao wa kuishi, basi utakapofika wakati wao wa kuondoka duniani, hawatacheleweshwa nao hata muda mchache wala hawatatangulia.
अरबी तफ़सीरें:
وَيَجۡعَلُونَ لِلَّهِ مَا يَكۡرَهُونَۚ وَتَصِفُ أَلۡسِنَتُهُمُ ٱلۡكَذِبَ أَنَّ لَهُمُ ٱلۡحُسۡنَىٰۚ لَا جَرَمَ أَنَّ لَهُمُ ٱلنَّارَ وَأَنَّهُم مُّفۡرَطُونَ
Na miongoni mwa maovu yao, ni kwamba wao wanawafanya ni wa Mwenyezi Mungu watoto wa kike ambao wao wenyewe wanawachukia. Na ndimi zao zinasema urongo kwamba wao watakuwa na mwisho mwema. Kwa kweli, wao watakuwa na Moto na wao ni wenye kuachwa humo na kusahauliwa.
अरबी तफ़सीरें:
تَٱللَّهِ لَقَدۡ أَرۡسَلۡنَآ إِلَىٰٓ أُمَمٖ مِّن قَبۡلِكَ فَزَيَّنَ لَهُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ أَعۡمَٰلَهُمۡ فَهُوَ وَلِيُّهُمُ ٱلۡيَوۡمَ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ
Naapa kwa Mwenyezi Mungu, hakika tumewapeleka Mitume kwa makundi ya watu kabla yako, ewe Mtume, Shetani akawapambia matendo waliyoyafanya ya ukafiri, ukanushaji na kuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Yeye anasimamia kazi ya kuwapoteza wao ulimwenguuni, na hao wenye kupotezwa, watakuwa na adhabu kali yenye kuumiza kesho akhera.
अरबी तफ़सीरें:
وَمَآ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ إِلَّا لِتُبَيِّنَ لَهُمُ ٱلَّذِي ٱخۡتَلَفُواْ فِيهِ وَهُدٗى وَرَحۡمَةٗ لِّقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ
Na hatukukuteremshia Qur’ani, ewe Mtume, isipokuwa ni uwafunulie watu wazi yale ambayo walikuwa wakitafautiana juu yake, ya dini na hukumu, ili hoja zisimame kwao kwa maelezo yako ambayo hayauachii upotofu njia ya kuingia nyoyoni. Na kwa kuwa Qur’ani ni uongofu, haitoi nafasi ya kutunduwaa, nayo ni rehema kwa Waumini katika kufuata kwao uongofu na kujiepusha kwao na upotevu.
अरबी तफ़सीरें:
 
अर्थों का अनुवाद सूरा: अन्-नह़्ल
सूरों की सूची पृष्ठ संख्या
 
क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - स्वाहीली अनुवाद - अब्दुल्लाह मुहम्मद तथा नासिर ख़मीस - अनुवादों की सूची

अनुवाद डॉक्टर अब्दुल्लाह मुहम्मद अबू बक्र और शैख़ नासिर ख़मीस ने किया है।

बंद करें