Check out the new design

क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - स्वाहीली अनुवाद - अब्दुल्लाह मुहम्मद तथा नासिर ख़मीस * - अनुवादों की सूची


अर्थों का अनुवाद सूरा: आले इम्रान   आयत:
يَوۡمَ تَجِدُ كُلُّ نَفۡسٖ مَّا عَمِلَتۡ مِنۡ خَيۡرٖ مُّحۡضَرٗا وَمَا عَمِلَتۡ مِن سُوٓءٖ تَوَدُّ لَوۡ أَنَّ بَيۡنَهَا وَبَيۡنَهُۥٓ أَمَدَۢا بَعِيدٗاۗ وَيُحَذِّرُكُمُ ٱللَّهُ نَفۡسَهُۥۗ وَٱللَّهُ رَءُوفُۢ بِٱلۡعِبَادِ
Na katika Siku ya Kiyama, Siku ya Malipo, kila nafsi italikuta jema lolote ililolifanya linaingojea likiwa limeongezwa ili ilipwe nalo. Na pia baya iliolifanya italikuta linaingojea vilevile, hapo itatamani lau ilikuwa baina yake na hilo tendo baya zama zirefu. Basi jitayarisheni kwa Siku hii, na muogope mateso ya Mola Aliye Jabari. Na pamoja na ukali wa mateso Yake, Yeye, Aliyetakata na sifa za upungufu, ni Msifika kwa ukamilifu wa huruma kwa waja.
अरबी तफ़सीरें:
قُلۡ إِن كُنتُمۡ تُحِبُّونَ ٱللَّهَ فَٱتَّبِعُونِي يُحۡبِبۡكُمُ ٱللَّهُ وَيَغۡفِرۡ لَكُمۡ ذُنُوبَكُمۡۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Sema, ewe Mtume, «Ikiwa nyinyi munampenda Mwenyezi Mungu kikweli, nifuateni mimi na kuniaminini, ndani na nje, ndipo Mwenyezi Mungu Atawapenda na Atawasamehe madhambi yenu.Kwani Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe madhambi ya waja Wake Waumini, ni Mwingi wa rehema kwao.» Aya hii tukufu yamhukumu kila anayedai kumpenda Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na akawa hamfuati Nabii Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kama ipasavyo kufuatwa, na wala hamtii katika maamrisho yake na makatazo yake, kuwa yeye ni mrongo katika madai yake mpaka amfuate Mtume , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kama ipasavyo kufuatwa.
अरबी तफ़सीरें:
قُلۡ أَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَۖ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ ٱلۡكَٰفِرِينَ
Sema, ewe Mtume, «Mtiini Mwenyezi Mungu kwa kufuata Kitabu Chake, na mtiini Mtume kwa kufuata mwenendo wake wakati wa uhai wake na baada ya kufa kwake.Wakiwa watakupa mgongo na kukamaa kwenye ukafiri na upotevu walionao, wao hawatakuwa wanastahili mapenzi ya Mwenyezi Mungu. Kwani Mwenyezi Mungu Hawapendi makafiri.
अरबी तफ़सीरें:
۞ إِنَّ ٱللَّهَ ٱصۡطَفَىٰٓ ءَادَمَ وَنُوحٗا وَءَالَ إِبۡرَٰهِيمَ وَءَالَ عِمۡرَٰنَ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ
Hakika Mwenyezi Mungu Amemchagua Ādam, Nūḥ, jamii ya Ibrāhīm na jamii ya 'Imrān Akawafanya kuwa ni bora wa watu wa zama zao.
अरबी तफ़सीरें:
ذُرِّيَّةَۢ بَعۡضُهَا مِنۢ بَعۡضٖۗ وَٱللَّهُ سَمِيعٌ عَلِيمٌ
Manabii hawa na Mitume ni mlolongo wa usafi wenye kuungana katika kumtakasa Mwenyezi Munguna, kumpwekesha na kutenda vitendo vinavyoambatana na wahyi Wake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyasikia maneno ya waja Wake, ni Mjuzi wa vitendo vyao na Atawalipa kwavyo.
अरबी तफ़सीरें:
إِذۡ قَالَتِ ٱمۡرَأَتُ عِمۡرَٰنَ رَبِّ إِنِّي نَذَرۡتُ لَكَ مَا فِي بَطۡنِي مُحَرَّرٗا فَتَقَبَّلۡ مِنِّيٓۖ إِنَّكَ أَنتَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ
kumbuka, ewe Mtume, ilivyokuwa kuhusu mambo ya Maryam na mama yake na mtoto wake 'Īsā, amani imshukie, ili kuwarudi, kwa hayo, wale wanoadai uungu wa 'Īsā au kuwa yeye ni Mwana wa Mwenyezi Mungu, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, aliposema mke wa 'Imran wakati aliposhika mimba, «Ewe Mola wangu, mimi nimekutakasia kilioko ndani ya tumbo langu kiwe ni chako Peke Yako kwa kutumikia Baitulmaqdis. Basi takabali kutoka kwangu. Hakika Wewe Peke Yako Ndiye Msikizi wa dua yangu, Ndiye Mjuzi wa nia yangu.»
अरबी तफ़सीरें:
فَلَمَّا وَضَعَتۡهَا قَالَتۡ رَبِّ إِنِّي وَضَعۡتُهَآ أُنثَىٰ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا وَضَعَتۡ وَلَيۡسَ ٱلذَّكَرُ كَٱلۡأُنثَىٰۖ وَإِنِّي سَمَّيۡتُهَا مَرۡيَمَ وَإِنِّيٓ أُعِيذُهَا بِكَ وَذُرِّيَّتَهَا مِنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ ٱلرَّجِيمِ
Mimba yake ilipotimia na akamzaa mtoto wake alisema, «Mola wangu, mimi nimemzaa mwanamke ambaye hafai kwa kutumikia Baitulmaqdis,» Na Mwenyezi Mungu Anajua zaidi kwa alichokizaa na atamjaalia kuwa na jambo kubwa. Mke wa 'Imran aliendelea kusema, «Na Mwanamume niliyemtaka kwa kutumika si kama Mwanamke kwa hilo. Kwa kuwa mwanamume ni mwenye nguvu zaidi wa kutumika na kusimamia utumishi. Na mimi nimempa jina la Maryam. Na mimi nimemlinda kwako, yeye na watoto wake , kutokana na Shetani aliyefukuzwa kwenye rehema Yako.»
अरबी तफ़सीरें:
فَتَقَبَّلَهَا رَبُّهَا بِقَبُولٍ حَسَنٖ وَأَنۢبَتَهَا نَبَاتًا حَسَنٗا وَكَفَّلَهَا زَكَرِيَّاۖ كُلَّمَا دَخَلَ عَلَيۡهَا زَكَرِيَّا ٱلۡمِحۡرَابَ وَجَدَ عِندَهَا رِزۡقٗاۖ قَالَ يَٰمَرۡيَمُ أَنَّىٰ لَكِ هَٰذَاۖ قَالَتۡ هُوَ مِنۡ عِندِ ٱللَّهِۖ إِنَّ ٱللَّهَ يَرۡزُقُ مَن يَشَآءُ بِغَيۡرِ حِسَابٍ
Mwenyezi Mungu Akamjibu maombi yake na Akaikubali nadhiri yake na kuipokea vizuri na Akamsimamia binti yake, Maryam, kwa kumtunza na Akamkuza makuzi mazuri. Mwenyezi Mungu Akamsahilishia kwa kumjaalia Zakaria, amani imshukie, kuwa ni mlezi wake; naye akamuweka mahali pake pa kuabudu. Na alikuwa kila akimjia mahali hapo, anakuta ana chakula kizuri kilichotayarishwa. Akasema, «Ewe Maryam, umepata kutoka wapi chakula hiki kizuri?» Akasema, «Hiyo ni riziki itokayo kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu Anamruzuku Anayemtaka miongoni mwa waja Wake bila ya hesabu.»
अरबी तफ़सीरें:
 
अर्थों का अनुवाद सूरा: आले इम्रान
सूरों की सूची पृष्ठ संख्या
 
क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - स्वाहीली अनुवाद - अब्दुल्लाह मुहम्मद तथा नासिर ख़मीस - अनुवादों की सूची

अनुवाद डॉक्टर अब्दुल्लाह मुहम्मद अबू बक्र और शैख़ नासिर ख़मीस ने किया है।

बंद करें