क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - स्वाहीली अनुवाद - अब्दुल्लाह मुहम्मद तथा नासिर ख़मीस

4 : 60

قَدۡ كَانَتۡ لَكُمۡ أُسۡوَةٌ حَسَنَةٞ فِيٓ إِبۡرَٰهِيمَ وَٱلَّذِينَ مَعَهُۥٓ إِذۡ قَالُواْ لِقَوۡمِهِمۡ إِنَّا بُرَءَٰٓؤُاْ مِنكُمۡ وَمِمَّا تَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ كَفَرۡنَا بِكُمۡ وَبَدَا بَيۡنَنَا وَبَيۡنَكُمُ ٱلۡعَدَٰوَةُ وَٱلۡبَغۡضَآءُ أَبَدًا حَتَّىٰ تُؤۡمِنُواْ بِٱللَّهِ وَحۡدَهُۥٓ إِلَّا قَوۡلَ إِبۡرَٰهِيمَ لِأَبِيهِ لَأَسۡتَغۡفِرَنَّ لَكَ وَمَآ أَمۡلِكُ لَكَ مِنَ ٱللَّهِ مِن شَيۡءٖۖ رَّبَّنَا عَلَيۡكَ تَوَكَّلۡنَا وَإِلَيۡكَ أَنَبۡنَا وَإِلَيۡكَ ٱلۡمَصِيرُ

Kwa hakika mlikuwa na kiigizo kizuri, (enyi Waumini), kwa Ibrãhîm na wale waliokuwa pamoja naye waliposema kuwaambia wakanushaji Allah Mtukufu, «Sisi tumejiepusha na nyinyi na vile mnavyoviabudu kinyume na Allah Mtukufu. Tumewakanusha nyinyi na tumeukataa ukafiri mlionao, na umejitokeza nje uadui na machukivu ya milele baina yetu sisi na nyinyi madamu bado mko kwenye ukanushaji wenu, mpaka mmuamini Allah Mtukufu Peke Yake.» Lakini haliingii kwenye kuigiza tendo la Ibrãhîm la kumuombea msamaha baba yake, kwa kuwa hilo lilitokea kabla ya Ibrãhîm kudhihirikiwa kuwa baba yake ni adui wa Allah Mtukufu, na alipodhihirikiwa kuwa yeye ni adui wa Allah Mtukufu alijiepusha naye. Mola wetu! Kwako wewe tumetegemea, na kwako wewe tumerejea kwa kutubia, na kwako wewe ndiko marejeo Siku ya Kiyama. info
التفاسير: |
prev

Al-Mumtahanah

next
:
0:00 0:00