Check out the new design

क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - स्वाहीली अनुवाद - अब्दुल्लाह मुहम्मद तथा नासिर ख़मीस * - अनुवादों की सूची


अर्थों का अनुवाद सूरा: अल्-आला   आयत:
وَيَتَجَنَّبُهَا ٱلۡأَشۡقَى
na atajiepusha na mawaidha aliye mbaya asiyemuogopa Mola wake
अरबी तफ़सीरें:
ٱلَّذِي يَصۡلَى ٱلنَّارَ ٱلۡكُبۡرَىٰ
atakayeingia kwenye Moto wa Jahanamu akiadhibika kwa ukali wake.
अरबी तफ़सीरें:
ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحۡيَىٰ
Kisha hatakuwa ni mwenye kufa akapumzika wala ni mwenye kuishi akanufaika.
अरबी तफ़सीरें:
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن تَزَكَّىٰ
Hakika amefuzu mwenye kuisafisha nafsi yake na tabia mbovu,
अरबी तफ़सीरें:
وَذَكَرَ ٱسۡمَ رَبِّهِۦ فَصَلَّىٰ
na akamtaja Mwenyezi Mungu, akampwekesha, akamuomba, akafanya vitendo vya kumridhisha na akasimamisha Swala kwa nyakati zake kwa kutaka radhi za Mwenyezi Mungu na kufuata sheria Aliyoiweka.
अरबी तफ़सीरें:
بَلۡ تُؤۡثِرُونَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا
Hakika yenu, nyinyi watu, mnafadhilisha pambo la maisha ya kilimwengu juu ya starehe za Akhera.
अरबी तफ़सीरें:
وَٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ وَأَبۡقَىٰٓ
Na hakika ya mambo ni kuwa nyumba ya Akhera na starehe zake ni bora zaidi kuliko ulimwngu na ni yenye kusalia zaidi.
अरबी तफ़सीरें:
إِنَّ هَٰذَا لَفِي ٱلصُّحُفِ ٱلۡأُولَىٰ
Haya mlioosimuliwa ndani ya Sura hii ni miongoni mwa yaliyotajwa kimaana katika Kurasa zilizotangulia kuteremshwa kabla ya Qur’ani.
अरबी तफ़सीरें:
صُحُفِ إِبۡرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ
Nazo ni Kurasa za Ibrāhīm na Mūsā, amani ziwashukie.
अरबी तफ़सीरें:
 
अर्थों का अनुवाद सूरा: अल्-आला
सूरों की सूची पृष्ठ संख्या
 
क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - स्वाहीली अनुवाद - अब्दुल्लाह मुहम्मद तथा नासिर ख़मीस - अनुवादों की सूची

अनुवाद डॉक्टर अब्दुल्लाह मुहम्मद अबू बक्र और शैख़ नासिर ख़मीस ने किया है।

बंद करें