क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - सवाहिली अनुवाद - अली मुहसिन बरवानी * - अनुवादों की सूची

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

अर्थों का अनुवाद आयत: (9) सूरा: सूरा अल्-अन्फ़ाल
إِذۡ تَسۡتَغِيثُونَ رَبَّكُمۡ فَٱسۡتَجَابَ لَكُمۡ أَنِّي مُمِدُّكُم بِأَلۡفٖ مِّنَ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةِ مُرۡدِفِينَ
Mlipo kuwa mkimuomba msaada Mola wenu Mlezi, naye akakujibuni kuwa: Kwa yakini Mimi nitakusaidieni kwa Malaika elfu wanao fuatana mfululizo.
Na enyi Waumini! Kumbukeni nanyi mnagawana ngawira na mnakhitalifiana, mlipo omba uwokovu na msaada, na mkaandikiwa kuwa hapana la kukuepusheni na vita. Mwenyezi Mungu alikuitikieni maombi yenu, akakuungeni mkono kwa kukuleteeni (Malaika) Roho zilizo safi nyingi zinazo fika elfu zinazo fuatana, zikija moja baada ya moja. Walipo jua wapiganaji Waumini kuwa hapana njia ya kuepukana na vita wakaomba msaada kwa Mwenyezi Mungu, naye Mwenyezi Mungu Mtukufu akawaitikia, na akawaunga mkono kwa Malaika elfu walio fuatana. Yaani alianza kwa kupeleka msaada kwa vikosi vilivyo fuatana ili iwe wepesi kwa kila kikosi kuelekea pahala pake katika vita pasiwepo kukaa bure au kupigana makumbo. Na ifikapo misaada ya majeshi ya vita roho hufurahi na moyo huingia nguvu. Na hayo ndiyo aliyo yakusudia Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kauli yake: "Na Mwenyezi Mungu hakufanya haya ila kuwa ni bishara na ili nyoyo zenu zituwe." Na ushindi daima unatokana na Mwenyezi Mungu.
अरबी तफ़सीरें:
 
अर्थों का अनुवाद आयत: (9) सूरा: सूरा अल्-अन्फ़ाल
सूरों की सूची पृष्ठ संख्या
 
क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - सवाहिली अनुवाद - अली मुहसिन बरवानी - अनुवादों की सूची

पवित्र क़ुरआन के अर्थों का सवाहिली अनुवाद - अनुवादक : अली मुहसिन बरवानी

बंद करें