Check out the new design

क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - सवाहिली अनुवाद - अली मुहसिन बरवानी * - अनुवादों की सूची

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

अर्थों का अनुवाद सूरा: अल्-लैल   आयत:

Al-Lail

وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰ
Naapa kwa usiku unapo funika!
Naapa kwa usiku kinapo enea kiza chake!
अरबी तफ़सीरें:
وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ
Na mchana unapo dhihiri!
Na naapa kwa mchana unapo zagaa mwangaza wake!
अरबी तफ़सीरें:
وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ
Na kwa Aliye umba dume na jike!
Na naapa kwa Mjuzi aliye umba viwili viwili, dume na jike, katika kila vinavyo zaliwa!
अरबी तफ़सीरें:
إِنَّ سَعۡيَكُمۡ لَشَتَّىٰ
Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.
Hakika juhudi zenu bila ya shaka zimekhitalifiana; kwani wapo wenye kubahatika katika juhudi zao, na wako wasio bahatika.
अरबी तफ़सीरें:
فَأَمَّا مَنۡ أَعۡطَىٰ وَٱتَّقَىٰ
Ama mwenye kutoa na akamchamngu!
Ama mwenye kutoa katika Njia ya Mwenyezi Mungu, na akamkhofu Mola wake Mlezi, na kwa hivyo akaepuka anayo yakataza,
अरबी तफ़सीरें:
وَصَدَّقَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ
Na akaliwafiki lilio jema!
Na akayakinika kufuata fadhila njema, nayo ni Imani kumuamini Mwenyezi Mungu kwa kumjua,
अरबी तफ़सीरें:
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡيُسۡرَىٰ
Tutamsahilishia yawe mepesi.
Basi Sisi tutamtengenezea awe katika khulka ya wepesi na raha kwa kumwongoza kwenye njia ya kheri.
अरबी तफ़सीरें:
وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسۡتَغۡنَىٰ
Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake!
Ama mwenye kufanya ubakhili kwa mali yake asitoe haki ya Mwenyezi Mungu iliomo humo, na akawa hana haja na yatokayo kwa Mwenyezi Mungu,
अरबी तफ़सीरें:
وَكَذَّبَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ
Na akakanusha lilio jema!
Na akakadhibisha khulka nzuri,
अरबी तफ़सीरें:
 
अर्थों का अनुवाद सूरा: अल्-लैल
सूरों की सूची पृष्ठ संख्या
 
क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - सवाहिली अनुवाद - अली मुहसिन बरवानी - अनुवादों की सूची

अनुवाद अली मुहसिन बरवानी द्वारा किया गया।

बंद करें