Check out the new design

क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - सवाहिली अनुवाद - अनुवाद अग्रदूत केंद्र * - अनुवादों की सूची


अर्थों का अनुवाद सूरा: अत्-तौबा   आयत:
يَحۡلِفُونَ بِٱللَّهِ لَكُمۡ لِيُرۡضُوكُمۡ وَٱللَّهُ وَرَسُولُهُۥٓ أَحَقُّ أَن يُرۡضُوهُ إِن كَانُواْ مُؤۡمِنِينَ
Wanawaapia kwa Mwenyezi Mungu ili wawaridhishe nyinyi, ilhali Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndio wanaostahiki zaidi kwamba wao wawaridhishe ikiwa wao ni Waumini.
अरबी तफ़सीरें:
أَلَمۡ يَعۡلَمُوٓاْ أَنَّهُۥ مَن يُحَادِدِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ فَأَنَّ لَهُۥ نَارَ جَهَنَّمَ خَٰلِدٗا فِيهَاۚ ذَٰلِكَ ٱلۡخِزۡيُ ٱلۡعَظِيمُ
Je, hawajui ya kwamba anayempinga Mwenyezi Mungu na Mtume wake, basi huyo hakika ana Moto wa Jahannam adumu humo? Hiyo ndiyo hizaya kubwa.
अरबी तफ़सीरें:
يَحۡذَرُ ٱلۡمُنَٰفِقُونَ أَن تُنَزَّلَ عَلَيۡهِمۡ سُورَةٞ تُنَبِّئُهُم بِمَا فِي قُلُوبِهِمۡۚ قُلِ ٱسۡتَهۡزِءُوٓاْ إِنَّ ٱللَّهَ مُخۡرِجٞ مَّا تَحۡذَرُونَ
Wanafiki wanaogopa kwamba iteremshwe Sura juu yao itakayowaambia yale yaliyo katika nyoyo zao. Sema: Fanyeni stihizai! Hakika Mwenyezi Mungu atayatoa nje hayo mnayoyaogopa.
अरबी तफ़सीरें:
وَلَئِن سَأَلۡتَهُمۡ لَيَقُولُنَّ إِنَّمَا كُنَّا نَخُوضُ وَنَلۡعَبُۚ قُلۡ أَبِٱللَّهِ وَءَايَٰتِهِۦ وَرَسُولِهِۦ كُنتُمۡ تَسۡتَهۡزِءُونَ
Na ukiwauliza, bila shaka watasema: Hakika tulikuwa tukipiga porojo na kucheza tu. Sema: Kwani mlikuwa mkimfanyia masikhara Mwenyezi Mungu, na ishara zake, na Mtume wake?
अरबी तफ़सीरें:
لَا تَعۡتَذِرُواْ قَدۡ كَفَرۡتُم بَعۡدَ إِيمَٰنِكُمۡۚ إِن نَّعۡفُ عَن طَآئِفَةٖ مِّنكُمۡ نُعَذِّبۡ طَآئِفَةَۢ بِأَنَّهُمۡ كَانُواْ مُجۡرِمِينَ
Msitoe udhuru. Hakika mmekwisha kufuru baada ya kuamini kwenu! Tukilisamehe kundi moja miongoni mwenu, tunaliadhibu kundi jingine kwa kuwa wao wamekuwa wahalifu.
अरबी तफ़सीरें:
ٱلۡمُنَٰفِقُونَ وَٱلۡمُنَٰفِقَٰتُ بَعۡضُهُم مِّنۢ بَعۡضٖۚ يَأۡمُرُونَ بِٱلۡمُنكَرِ وَيَنۡهَوۡنَ عَنِ ٱلۡمَعۡرُوفِ وَيَقۡبِضُونَ أَيۡدِيَهُمۡۚ نَسُواْ ٱللَّهَ فَنَسِيَهُمۡۚ إِنَّ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ هُمُ ٱلۡفَٰسِقُونَ
Wanaume wanafiki na wanawake wanafiki, wote ni hali moja. Huamrisha maovu na hukataza mema, na huifumba mikono yao. Walimsahau Mwenyezi Mungu, basi na Yeye pia akawasahau. Hakika wanafiki ndio wavukao mipaka.
अरबी तफ़सीरें:
وَعَدَ ٱللَّهُ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَٱلۡمُنَٰفِقَٰتِ وَٱلۡكُفَّارَ نَارَ جَهَنَّمَ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ هِيَ حَسۡبُهُمۡۚ وَلَعَنَهُمُ ٱللَّهُۖ وَلَهُمۡ عَذَابٞ مُّقِيمٞ
Mwenyezi Mungu amewaahidi wanafiki wanaume na wanafiki wanawake na makafiri Moto wa Jahannamu watadumu humo. Hiyo ndiyo inawatosha, na Mwenyezi Mungu amewalaani; nao wana adhabu ya kudumu.
अरबी तफ़सीरें:
 
अर्थों का अनुवाद सूरा: अत्-तौबा
सूरों की सूची पृष्ठ संख्या
 
क़ुरआन के अर्थों का अनुवाद - सवाहिली अनुवाद - अनुवाद अग्रदूत केंद्र - अनुवादों की सूची

अनुवाद अनुवाद अग्रदूत केंद्र द्वारा नियुक्त एक समूह ने अल-रब्वाह आह्वान संस्था और भाषाओं में इस्लामिक सामग्री की सेवा करने वाली संस्था के सहयोग से किया है।

बंद करें