Check out the new design

Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis * - Daftar isi terjemahan


Terjemahan makna Surah: Az-Zukhruf   Ayah:
وَإِنَّهُۥ لَعِلۡمٞ لِّلسَّاعَةِ فَلَا تَمۡتَرُنَّ بِهَا وَٱتَّبِعُونِۚ هَٰذَا صِرَٰطٞ مُّسۡتَقِيمٞ
Kwa hakika kuteremka kwa Īsā, amani imshukie, kabla ya Siku ya Kiyama, ni dalili ya kukaribia Wakati huo, basi msitie shaka kuwa hilo ni lenye kuwa hapana budi. Na nifuateni mimi katika yale ninayowatolea habari kutoka kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka. Hii ni njia imara inayoelekea Peponi, isiyo na mpeto.
Tafsir berbahasa Arab:
وَلَا يَصُدَّنَّكُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُۖ إِنَّهُۥ لَكُمۡ عَدُوّٞ مُّبِينٞ
Na asiwazuie Shetani, kwa kutia kwake wasiwasi kwa watu, kunitii mimi katika yale ninayowaamrisha na ninayowakataza, kwani yeye ni adui kwenu ambaye uadui wake uko waziwazi.
Tafsir berbahasa Arab:
وَلَمَّا جَآءَ عِيسَىٰ بِٱلۡبَيِّنَٰتِ قَالَ قَدۡ جِئۡتُكُم بِٱلۡحِكۡمَةِ وَلِأُبَيِّنَ لَكُم بَعۡضَ ٱلَّذِي تَخۡتَلِفُونَ فِيهِۖ فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Na Īsā alipowajia Wana wa lsrāīl kwa dalili zilizofunuka wazi alisema, «Nimewajia na unabii, na ili niwaeleze baadhi ya mambo ya yale mnayotafautiana kwayo katika mambo ya Dini. Basi mcheni Mwenyezi Mungu kwa kufuata amri Zake na kuepuka makatazo Yake, na mnitii mimi katika yale ninayowaamrisha ya kumcha Mwenyezi Mungu na kumtii.
Tafsir berbahasa Arab:
إِنَّ ٱللَّهَ هُوَ رَبِّي وَرَبُّكُمۡ فَٱعۡبُدُوهُۚ هَٰذَا صِرَٰطٞ مُّسۡتَقِيمٞ
«Hakika Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Ndiye Mola wangu na Mola wenu nyote, basi muabuduni Yeye Peke Yake na msimshirikishe na Yeye kitu chochote. Hili nililowaamrisha la kumcha Mwenyezi Mungu na kumpwekesha kwa ustahiki wa kuabudiwa ndio njia iliolingana sawa, nayo ni Dini ya Mwenyezi Mungu ya kweli Ambaye Hakubali kutoka kwa yoyote dini isiyokuwa hiyo.”
Tafsir berbahasa Arab:
فَٱخۡتَلَفَ ٱلۡأَحۡزَابُ مِنۢ بَيۡنِهِمۡۖ فَوَيۡلٞ لِّلَّذِينَ ظَلَمُواْ مِنۡ عَذَابِ يَوۡمٍ أَلِيمٍ
Hapo makundi ya watu yakatafautiana kuhusu jambo la Īsā, amani imshukie, na wakawa mapote: kati yao kuna waliokubali kuwa yeye ni mja wa Mwenyezi Mungu na ni Mtume Wake, na hiyo ndio kauli ya kweli, na kati yao kuna wanaodai kuwa yeye ni mwana wa Mwenyezi Mungu , na kati yao kuna wanaosema kwamba yeye ni Mwenyezi Mungu, Ametukuka Mwenyezi Mungu kutukuka kukubwa na kutakasika na neno lao hilo. Basi maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama ni yenye kuwapata wale waliomsifu Īsā kwa sifa ambazo sizo zile Mwenyezi Mungu Alizomsifu nazo.
Tafsir berbahasa Arab:
هَلۡ يَنظُرُونَ إِلَّا ٱلسَّاعَةَ أَن تَأۡتِيَهُم بَغۡتَةٗ وَهُمۡ لَا يَشۡعُرُونَ
Je, kwani wana kutu chochote wanachokingojea watu wa makundi hayo waliotafautiana kuhusu Īsā isipokuwa ni kujiwa na Kiyama kwa ghafla na hali wao hawahisi wala hawatambui?
Tafsir berbahasa Arab:
ٱلۡأَخِلَّآءُ يَوۡمَئِذِۭ بَعۡضُهُمۡ لِبَعۡضٍ عَدُوٌّ إِلَّا ٱلۡمُتَّقِينَ
Marafiki katika kumuasi Mwenyezi Mungu duniani watatengana wao kwa wao Siku ya Kiyama. Lakini wale waliofanya urafiki juu ya uchaji Mwenyezi Mungu, urafiki wao utadumu duniani na Akhera.
Tafsir berbahasa Arab:
يَٰعِبَادِ لَا خَوۡفٌ عَلَيۡكُمُ ٱلۡيَوۡمَ وَلَآ أَنتُمۡ تَحۡزَنُونَ
Wataambiwa hawa wachamungu, «Enyi waja wangu! Hamna khofu yoyote Leo ya kupata mateso yangu, wala nyinyi hamtahuzunika juu ya hadhi za kilimwengu mlizozikosa.”
Tafsir berbahasa Arab:
ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ بِـَٔايَٰتِنَا وَكَانُواْ مُسۡلِمِينَ
Wale walioziamini aya zetu na wakayafuata kivitendo yale walioletewa na Mitume wao, wakawa ni wenye kumtii Mwenyezi Mungu, Mola wa viumbe vyote, kwa nyoyo zao na viungo vyao,
Tafsir berbahasa Arab:
ٱدۡخُلُواْ ٱلۡجَنَّةَ أَنتُمۡ وَأَزۡوَٰجُكُمۡ تُحۡبَرُونَ
wataambiwa, «Ingieni Peponi , nyinyi na wendani wenu Waumini, mkistareheshwa humo na mkifurahishwa.”
Tafsir berbahasa Arab:
يُطَافُ عَلَيۡهِم بِصِحَافٖ مِّن ذَهَبٖ وَأَكۡوَابٖۖ وَفِيهَا مَا تَشۡتَهِيهِ ٱلۡأَنفُسُ وَتَلَذُّ ٱلۡأَعۡيُنُۖ وَأَنتُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ
Watazungushiwa, hawa waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mitume Wake, chakula ndani ya vyombo vya dhahabu na vinywaji ndani ya gilasi za dhahabu. Na humo watakuwa na kila ambacho nafsi zao zinakitamani na macho yao yanapendezwa nacho, na wao humo watakaa milele.
Tafsir berbahasa Arab:
وَتِلۡكَ ٱلۡجَنَّةُ ٱلَّتِيٓ أُورِثۡتُمُوهَا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Na hii Pepo ambayo Mwenyezi Mungu Amewarithisha, ni kwa sababu ya kile mlichokuwa mkikifanya ulimwenguni cha mambo ya kheri na matendo mema, na akaifanya, kwa wema Wake na rehema Yake, ni malipo yenu.
Tafsir berbahasa Arab:
لَكُمۡ فِيهَا فَٰكِهَةٞ كَثِيرَةٞ مِّنۡهَا تَأۡكُلُونَ
Mtakuwa nayo, humo Peponi, matunda mengi ya kila aina ya nyinyi kuyala.
Tafsir berbahasa Arab:
 
Terjemahan makna Surah: Az-Zukhruf
Daftar surah Nomor Halaman
 
Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis - Daftar isi terjemahan

Diterjemahkan oleh Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakar dan Syekh Nasir Khamis.

Tutup