Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis * - Daftar isi terjemahan


Terjemahan makna Ayah: (15) Surah: Surah Al-Fatḥ
سَيَقُولُ ٱلۡمُخَلَّفُونَ إِذَا ٱنطَلَقۡتُمۡ إِلَىٰ مَغَانِمَ لِتَأۡخُذُوهَا ذَرُونَا نَتَّبِعۡكُمۡۖ يُرِيدُونَ أَن يُبَدِّلُواْ كَلَٰمَ ٱللَّهِۚ قُل لَّن تَتَّبِعُونَا كَذَٰلِكُمۡ قَالَ ٱللَّهُ مِن قَبۡلُۖ فَسَيَقُولُونَ بَلۡ تَحۡسُدُونَنَاۚ بَلۡ كَانُواْ لَا يَفۡقَهُونَ إِلَّا قَلِيلٗا
Watasema wale walioachwa nyuma utakapoondoka, ewe Nabii, wewe na Maswahaba wako kuelekea kwenye ngawira za Khaybar ambazo Mwenyezi Mungu Aliwaahidi nyinyi kuwa mtazipata, «Tuacheni tuende na nyinyi huko Khaybar» wakiwa wanataka kwa hilo kubadilisha ahadi ya Mwenyezi Mungu kwenu. Waambie, «Hamtatoka pamoja na sisi kwenda Khaybar, kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Alitwambia kabla hatujarudi Madina kwamba ngawira za Khaybar ni za wale waliohudhuria Ḥudaybiyah pamoja na sisi.» Watasema, «Mambo sivyo kama mnavyosema. Mwenyezi Mungu Hakuwaamrisha nyinyi hili. Nyinyi mnatukataza kutoka na nyinyi kwa uhasidi wenu tusije tukapata ngawira pamoja na nyinyi.» Mambo sivyo kama walivyodai, bali wao walikuwa hawaelewi amri za Mwenyezi Mungu kuhusu haki zao na wajibu wao wa kidini isipokuwa kidogo.
Tafsir berbahasa Arab:
 
Terjemahan makna Ayah: (15) Surah: Surah Al-Fatḥ
Daftar surah Nomor Halaman
 
Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Abdullah Muhammad dan Nasir Khamis - Daftar isi terjemahan

Terjemahan makna Al-Qur`ān Al-Karīm ke bahasa Sawahili oleh Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakar dan Syekh Nasir Khamis

Tutup