Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Ali Muhsin Al-Barwani * - Daftar isi terjemahan

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Terjemahan makna Ayah: (19) Surah: Surah Al-An'ām
قُلۡ أَيُّ شَيۡءٍ أَكۡبَرُ شَهَٰدَةٗۖ قُلِ ٱللَّهُۖ شَهِيدُۢ بَيۡنِي وَبَيۡنَكُمۡۚ وَأُوحِيَ إِلَيَّ هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانُ لِأُنذِرَكُم بِهِۦ وَمَنۢ بَلَغَۚ أَئِنَّكُمۡ لَتَشۡهَدُونَ أَنَّ مَعَ ٱللَّهِ ءَالِهَةً أُخۡرَىٰۚ قُل لَّآ أَشۡهَدُۚ قُلۡ إِنَّمَا هُوَ إِلَٰهٞ وَٰحِدٞ وَإِنَّنِي بَرِيٓءٞ مِّمَّا تُشۡرِكُونَ
Sema: Kitu gani ushahidi wake mkubwa kabisa? Sema: Mwenyezi Mungu. Yeye ndiye shahidi baina yangu na nyinyi. Na nimefunuliwa Qur'ani hii ili kwayo nikuonyeni nyinyi na kila inayo mfikia. Ati kweli nyinyi mnashuhudia kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu wapo miungu wengine? Sema: Mimi sishuhudii hayo. Sema: Hakika Yeye ni Mungu mmoja tu, nami ni mbali na mnao washirikisha.
Ewe Nabii! Waambie hao wanao kukanusha na wanao taka ushahidi wa Utume wako: Kitu gani chenye ushahidi mkubwa, na chenye kustahiki kusadikiwa kuliko vyote? Kisha uwambie: Hakika Mwenyezi Mungu ndiye shahidi mkubwa kushinda wote wa kushuhudia baina yangu na nyinyi katika ukweli wa haya ninayo kuleteeni. Na Yeye ndiye aliye iteremsha hii Qur'ani ili iwe ni hoja ya ukweli wangu, nipate kukuhadharisheni nyinyi na kila itakayo mfikia khabari yake. Nayo ni hoja ya kukata, inayo shuhudia ukweli wangu. Kwani nyinyi hamwezi kuleta mfano wake! Waulize: Hivyo nyinyi mnaitakidi kuwa Mwenyezi Mungu ana miungu wenziwe? Kisha uwambie: Mimi sishuhudii hayo, wala sisemi hivyo, wala sikukubalieni kwa hayo. Hapana shaka wa kuabudiwa kwa haki ni Mungu Mmoja. Na mimi ni mbali kabisa na hayo masanamu mnayo mshirikisha Naye.
Tafsir berbahasa Arab:
 
Terjemahan makna Ayah: (19) Surah: Surah Al-An'ām
Daftar surah Nomor Halaman
 
Terjemahan makna Alquran Alkarim - Terjemahan Berbahasa Sawahili - Ali Muhsin Al-Barwani - Daftar isi terjemahan

Terjemahan Makna Al-Qur`ān Al-Karīm ke Bahasa Sawahili oleh Ali Muhsin Al-Barwani

Tutup