Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Ali Muhsin Albirwany * - Indice Traduzioni

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduzione dei significati Sura: Al-Zalzalah   Versetto:

Surat Az-Zalzalah

إِذَا زُلۡزِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ زِلۡزَالَهَا
Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!
Ikitisika ardhi kwa mtikiso mkubwa, na ikasukika kwa ukomo wa kutisika na kusukika kunako mkinika na ikaweza kuchukua!
Esegesi in lingua araba:
وَأَخۡرَجَتِ ٱلۡأَرۡضُ أَثۡقَالَهَا
Na itakapo toa ardhi mizigo yake!
Na ardhi ikatoa yote yaliomo katika ndani ya tumbo lake, ikiwa khazina au maiti walio kwisha zikwa!
Esegesi in lingua araba:
وَقَالَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا لَهَا
Na mtu akasema: Ina nini?
Na binaadamu akasema kwa kushtuka na khofu: Ardhi hii ina nini hata inatikisika hivi, na inatoa vilivyomo tumboni mwake, ndio Saa imefika?
Esegesi in lingua araba:
يَوۡمَئِذٖ تُحَدِّثُ أَخۡبَارَهَا
Siku hiyo itahadithia khabari zake.
Siku hiyo ardhi itamsimulia mtu khabari zake zilio mshitua,
Esegesi in lingua araba:
بِأَنَّ رَبَّكَ أَوۡحَىٰ لَهَا
Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!
Kwani Mlezi wake na Muumba wake atakuwa kaifunulia, kaipa Wahyi, na kaiamuru itetemeke na ijisuke suke, ndio ikafanya upesi kutekeleza amri.
Esegesi in lingua araba:
يَوۡمَئِذٖ يَصۡدُرُ ٱلنَّاسُ أَشۡتَاتٗا لِّيُرَوۡاْ أَعۡمَٰلَهُمۡ
Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!
Siku hiyo watu watatoka makaburini mbio, nao wamo katika mtafaruku, wapate kuziona hisabu zao na malipo yao aliyo waahidi Mwenyezi Mungu.
Esegesi in lingua araba:
فَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٍ خَيۡرٗا يَرَهُۥ
Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!
Basi mwenye kufanya hata kitu chenye uzito wa punje ya mchanga cha kheri ataiona katika daftari lake, na atapata malipo yake.
Esegesi in lingua araba:
وَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٖ شَرّٗا يَرَهُۥ
Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!
Na mwenye kufanya shari ya uzito wa chembe ya mchanga ataiona kadhaalika, na atapata malipo yake. Wala Mola wako Mlezi hatamdhulumu yeyote.
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Sura: Al-Zalzalah
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Ali Muhsin Albirwany - Indice Traduzioni

Traduzione dei significati del Nobile Corano in swahili di Ali Muhsin Albirwany

Chiudi