クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis * - 対訳の目次


対訳 節: (213) 章: 雌牛章
كَانَ ٱلنَّاسُ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ فَبَعَثَ ٱللَّهُ ٱلنَّبِيِّـۧنَ مُبَشِّرِينَ وَمُنذِرِينَ وَأَنزَلَ مَعَهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ لِيَحۡكُمَ بَيۡنَ ٱلنَّاسِ فِيمَا ٱخۡتَلَفُواْ فِيهِۚ وَمَا ٱخۡتَلَفَ فِيهِ إِلَّا ٱلَّذِينَ أُوتُوهُ مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَتۡهُمُ ٱلۡبَيِّنَٰتُ بَغۡيَۢا بَيۡنَهُمۡۖ فَهَدَى ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لِمَا ٱخۡتَلَفُواْ فِيهِ مِنَ ٱلۡحَقِّ بِإِذۡنِهِۦۗ وَٱللَّهُ يَهۡدِي مَن يَشَآءُ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٍ
Watu walikuwa ni kundi moja, wameafikiana katika kumuamini Mwenyezi Mungu, kisha walitafautiana katika dini yao.Hapo ndipo Mwenyezi Mungu Aliwatuma Manabii, wakiwa ni walinganizi wa dini ya Mwenyezi Mungu, ni wabashiri wa Pepo kwa anayemtii Mwenyezi Mungu na ni waonyi wa Moto kwa anayemkanusha na kumuasi. Na Akateremsha, pamoja nao, vitabu vya mbinguni vilivyokusanya haki, ili wahukumu baina ya watu kwa yaliyomo ndani, katika yale waliyotafautiana juu yake. Na hawakutafautiana juu ya jambo la Mtume na Kitbu alichokuja nacho, kwa uhasidi na udhalimu, isipokuwa ni wale ambao Mwenyezi Mungu Amewapa Taurati na wakayajua yaliyomo ndani miongoni mwa hoja na hukumu. Hapo Mwenyezi Mungu, kwa fadhila zake, aliwaafikia Waumini kuipambanua haki na batili na kuyajua yale waliotafautiana juu yake. Mwenyezi Mungu Anampa taufiki amtakaye, miongoni mwa waja wake, kufuata njia iliyonyooka.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 節: (213) 章: 雌牛章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis - 対訳の目次

クルアーン・スワヒリ語対訳 - Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

閉じる