クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis * - 対訳の目次


対訳 節: (251) 章: 雌牛章
فَهَزَمُوهُم بِإِذۡنِ ٱللَّهِ وَقَتَلَ دَاوُۥدُ جَالُوتَ وَءَاتَىٰهُ ٱللَّهُ ٱلۡمُلۡكَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَعَلَّمَهُۥ مِمَّا يَشَآءُۗ وَلَوۡلَا دَفۡعُ ٱللَّهِ ٱلنَّاسَ بَعۡضَهُم بِبَعۡضٖ لَّفَسَدَتِ ٱلۡأَرۡضُ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ ذُو فَضۡلٍ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ
Hapo waliwashinda kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, na Dāwūd, Amani imshukiye, alimuua Jālūt, kiongozi wa majabari. Na Mwenyezi Mungu, Aliyeshinda na kutukuka, baada ya hapo, Akampa Dāwūd ufalme na utume katika Wana wa Isrāīl, na Alimfundisha Aliyoyataka miongoni mwa elimu. Na lau kama si himaya ya Mwenyezi Mungu, kwa kuwatumia baadhi ya watu- nao ni wale watiifu Kwake na wanaomuamini- kuwazuia wengine- nao ni wanaomuasi Mwenyezi Mungu na kumshirikisha-, basi ardhi ingaliharibika kwa ushindi wa ukafiri na kupata nguvu uharibifu na wenye kufanya maasia. Lakini Mwenyezi Mungu ni Mwenye fadhila kwa viumbe wote.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 節: (251) 章: 雌牛章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis - 対訳の目次

クルアーン・スワヒリ語対訳 - Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

閉じる