クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis * - 対訳の目次


対訳 節: (186) 章: イムラ―ン家章
۞ لَتُبۡلَوُنَّ فِيٓ أَمۡوَٰلِكُمۡ وَأَنفُسِكُمۡ وَلَتَسۡمَعُنَّ مِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ مِن قَبۡلِكُمۡ وَمِنَ ٱلَّذِينَ أَشۡرَكُوٓاْ أَذٗى كَثِيرٗاۚ وَإِن تَصۡبِرُواْ وَتَتَّقُواْ فَإِنَّ ذَٰلِكَ مِنۡ عَزۡمِ ٱلۡأُمُورِ
Mtapewa mtihani, tena mtapewa mtihani, enyi Waumini, katika mali yenu kwa kutakiwa mtoe matumizi ya wajibu na yanayopendekezwa na kwa mikasa inayoyakumba. Pia mtapewa mtihani katika nafsi zenu kwa kutakiwa mtekeleze ya wajibu ya kumtii Mwenyezi Mungu na kwa misiba inayowafikia ya majaraha au mauaji na kuwakosa vipenzi vyenu. Hilo litaendelea mpaka apambanuke mwenye imani ya kweli na mwenginewe. Na mtasikia, tena mtasikia, kutoka kwa Mayahudi, Wanaswara na washirikina maneno yatakayoudhi masikizi yenu katika matamshi ya ushirikina na kuitukana dini yenu. Na iwapo mtasubiri, enyi Waumini, juu ya hayo yote na mkamcha Mwenyezi Mungu kwa kujilazimisha kumtii Yeye na kujiepusha na kumuasi, hakika hilo ni miongoni mwa mambo ambayo yanakusudiwa kidhati na kushindaniwa.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 節: (186) 章: イムラ―ン家章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis - 対訳の目次

クルアーン・スワヒリ語対訳 - Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

閉じる