Check out the new design

クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis * - 対訳の目次


対訳 章: 婦人章   節:
أُوْلَٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ لَعَنَهُمُ ٱللَّهُۖ وَمَن يَلۡعَنِ ٱللَّهُ فَلَن تَجِدَ لَهُۥ نَصِيرًا
Hao ndio ambao umezidi uharibifu wao na umeenea upotevu wao. Mwenyezi Mungu,Aliyetukuka, Amewatoa kwenye rehema Yake. Na yoyote ambaye Mwenyezi Mungu Anamfukuza kwenye rehema Yake, hutampatia wa kumnusuru na kumuepushia adhabu mbaya.
アラビア語 クルアーン注釈:
أَمۡ لَهُمۡ نَصِيبٞ مِّنَ ٱلۡمُلۡكِ فَإِذٗا لَّا يُؤۡتُونَ ٱلنَّاسَ نَقِيرًا
Je, kwani wao wana fungu la utawala? Na lau walipewa, hawangalimpa yoyote kitu chochote katika hilo, hata kama ni kadiri ya kitone kilichoko kwenye koko ya tende.
アラビア語 クルアーン注釈:
أَمۡ يَحۡسُدُونَ ٱلنَّاسَ عَلَىٰ مَآ ءَاتَىٰهُمُ ٱللَّهُ مِن فَضۡلِهِۦۖ فَقَدۡ ءَاتَيۡنَآ ءَالَ إِبۡرَٰهِيمَ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَءَاتَيۡنَٰهُم مُّلۡكًا عَظِيمٗا
Au je, kwani wao wanamhusudu Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye kwa neema za unabii na utume alizopewa na Mwenyezi Mungu na kuwahusudu Masahaba wake kwa neema ya kuongozwa kwenye Imani, kuukubali utume, kumfuata Mtume na kupewa uwezo katika ardhi, wakawa wanatamani neema hizi ziwaondokee? Hakika sisi tuliwapa watu wa kizazi cha Ibrāhīm, amani imshukiye, Vitabu Alivyoviteremsha Mwenyezi Mungu kwao, wahyi mwingine usiokuwa kitabu chenye kusomwa na tukawapa , pamoja na hayo, utawala wenye kuenea.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَمِنۡهُم مَّنۡ ءَامَنَ بِهِۦ وَمِنۡهُم مَّن صَدَّ عَنۡهُۚ وَكَفَىٰ بِجَهَنَّمَ سَعِيرًا
Miongoni mwa hawa ambao walipewa fungu la elimu, kuna aliyeamini ujumbe wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye na akafuata Sheria aliyokuja nayo kivitendo. Na miongoni mwao kuna aliyekengeuka na asiitike mwito wake na akawakataza watu kumfuata. Wenye kuwatosha nyinyi, enyi wenye kukanusha, ni moto wa Jahanamu ambao utawashwa kwenu.
アラビア語 クルアーン注釈:
إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا سَوۡفَ نُصۡلِيهِمۡ نَارٗا كُلَّمَا نَضِجَتۡ جُلُودُهُم بَدَّلۡنَٰهُمۡ جُلُودًا غَيۡرَهَا لِيَذُوقُواْ ٱلۡعَذَابَۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَزِيزًا حَكِيمٗا
Hakika wale waliokanusha aya za Mwenyezi Mungu alizoziteremsha, wahyi wa kitabu Chake, dalili na hoja Zake, tutawaingiza kwenye Moto ambao watalionja joto lake; kila zikiungua ngozi zao tunawageuzia ngozi nyengine, ili adhabu yao na uchungu vipate kuendelea. Mwenyezi Mungu Aliyetukuka ni Mshindi, hakuna chochote chenye kumlemea, ni Mwingi wa hekima katika uendeshaji mambo Wake na uamuzi Wake.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ سَنُدۡخِلُهُمۡ جَنَّٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۖ لَّهُمۡ فِيهَآ أَزۡوَٰجٞ مُّطَهَّرَةٞۖ وَنُدۡخِلُهُمۡ ظِلّٗا ظَلِيلًا
Na wale ambao nyoyo zao zilitulia kwa kumuamini Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, kuukubali ujumbe wa Mtume Wake, Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, na wakasimama imara juu ya utiifu, tutawaingiza kwenye mabustani ya Pepo ambayo, chini ya majumba yake ya fahari na miti yake, inapita mito. Watastarehe humo milele na hawatatoka humo. Watakuwa na wake humo waliotakaswa na Mwenyezi Mungu na kila maudhi. Na tutawatia kwenye vivuli vilivyoshikana vilivyorefuka Peponi.
アラビア語 クルアーン注釈:
۞ إِنَّ ٱللَّهَ يَأۡمُرُكُمۡ أَن تُؤَدُّواْ ٱلۡأَمَٰنَٰتِ إِلَىٰٓ أَهۡلِهَا وَإِذَا حَكَمۡتُم بَيۡنَ ٱلنَّاسِ أَن تَحۡكُمُواْ بِٱلۡعَدۡلِۚ إِنَّ ٱللَّهَ نِعِمَّا يَعِظُكُم بِهِۦٓۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ سَمِيعَۢا بَصِيرٗا
Mwenyezi Mungu Anawaamrisha nyinyi kutekeleza aina zote za amana mlizoaminiwa nazo kwa wenyewe, msizifanyie dharau. Na Anawaamrisha muhukumu baina ya watu kwa uadilifu na uhaki, mtakapohukumu baina yao.Hilo ni jambo bora zaidi Analowaidhia Mwenyezi Mungu na kuwaongoza mlifanye. Hakika Mweyezi Mungu Aliyetukuka ni Msikizi wa maneno yenu, Anayajua matendo yenu na Anayaona.
アラビア語 クルアーン注釈:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَ وَأُوْلِي ٱلۡأَمۡرِ مِنكُمۡۖ فَإِن تَنَٰزَعۡتُمۡ فِي شَيۡءٖ فَرُدُّوهُ إِلَى ٱللَّهِ وَٱلرَّسُولِ إِن كُنتُمۡ تُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِۚ ذَٰلِكَ خَيۡرٞ وَأَحۡسَنُ تَأۡوِيلًا
Enyi ambao mlimuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata sheria Yake kivitendo, zikubalini amri za Mwenyezi Mungu Aliyetukuka na wala msimuasi, mkubalini Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, kwa yale Aliyokuja nayo ya haki na watiini watawala wa mambo yenu isipokuwa katika kumuasi Mwenyezu Mungu. Na mnapotafautiana baina yenu katika kitu chochote, basi irudisheni hukumu yake kwenye Kitabu cha Mwenyezi Mungu Aliyetukuka na Sunnah ya Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, iwapo nyinyi mnamuamini Mwenyezi Mungu Aliyetukuka na Siku ya Mwisho Imani ipasavyo. Kurudisha huko kwenye Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunnah ni bora kwenu kuliko kubishana na kusema kwa maoni, na ni mazuri kabisa marejeo yake na mwisho wake.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 章: 婦人章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis - 対訳の目次

Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

閉じる