Check out the new design

クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis * - 対訳の目次


対訳 章: 悔悟章   節:
ثُمَّ يَتُوبُ ٱللَّهُ مِنۢ بَعۡدِ ذَٰلِكَ عَلَىٰ مَن يَشَآءُۗ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Na atakayerudi nyuma akaacha ukafiri wake baada ya hilo, na akaingia kwenye Uislamu, basi Mwenyezi Mungu Anaikubali toba ya Anayemtaka katika wao na Anamsamehe dhambi zake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, ni mwingi wa kurehemu.
アラビア語 クルアーン注釈:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِنَّمَا ٱلۡمُشۡرِكُونَ نَجَسٞ فَلَا يَقۡرَبُواْ ٱلۡمَسۡجِدَ ٱلۡحَرَامَ بَعۡدَ عَامِهِمۡ هَٰذَاۚ وَإِنۡ خِفۡتُمۡ عَيۡلَةٗ فَسَوۡفَ يُغۡنِيكُمُ ٱللَّهُ مِن فَضۡلِهِۦٓ إِن شَآءَۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلِيمٌ حَكِيمٞ
Enyi mkusanyiko wa Waumini, hakika washirikina ni najisi na ni wachafu, hivyo basi msiwape nafasi kusongea kwenye eneo la Ḥarām baada ya mwaka huu wa tisa wa hijria (kalenda ya Kiislamu). Na iwapo mtachelea umasikini, kwa kukatikiwa na biashara zao, Mwenyezi Mungu Atawapa badala yake na Atawatosheleza kwa fadhila Zake Atakapo. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi mno wa hali zenu, ni Mwingi wa hekima katika kuyapeleka mambo yenu.
アラビア語 クルアーン注釈:
قَٰتِلُواْ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَلَا بِٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَلَا يُحَرِّمُونَ مَا حَرَّمَ ٱللَّهُ وَرَسُولُهُۥ وَلَا يَدِينُونَ دِينَ ٱلۡحَقِّ مِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ حَتَّىٰ يُعۡطُواْ ٱلۡجِزۡيَةَ عَن يَدٖ وَهُمۡ صَٰغِرُونَ
Enyi Waislamu, wapigeni vita Makafiri ambao hawamuamini Mwenyezi Mungu, wala hawaamini Kufufuliwa na Kulipwa, wala hawajiepushi na yale ambayo Mwenyezi Mungu na Mtume Wake wameyakataza, wala hawajilazimishi na hukumu za sheria ya Uislamu, miongoni mwa Mayahudi na Wanaswara, mpaka watoe jizia, ambayo nyinyi mnawalazimisha nayo, kwa mikono yao wakiwa wanyenyekevu na wanyonge.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَقَالَتِ ٱلۡيَهُودُ عُزَيۡرٌ ٱبۡنُ ٱللَّهِ وَقَالَتِ ٱلنَّصَٰرَى ٱلۡمَسِيحُ ٱبۡنُ ٱللَّهِۖ ذَٰلِكَ قَوۡلُهُم بِأَفۡوَٰهِهِمۡۖ يُضَٰهِـُٔونَ قَوۡلَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِن قَبۡلُۚ قَٰتَلَهُمُ ٱللَّهُۖ أَنَّىٰ يُؤۡفَكُونَ
Hakika wamemshirikisha Mwenyezi Mungu Mayahudi walipodai kwamba 'Uzayr ni mwana wa Mwenyezi Mungu. Na wamemshirikisha Mwenyezi Mungu Wanaswara walipodai kwamba Al-Masīh( ni mwana wa Mwenyezi Mungu, Neno hili wamelizua wao wenyewe, na wao kwa hili wanafananisha na neno la washirikina kabla yao. Mwenyezi Mungu Awalaani washirikina wote. Vipi wao wajiepusha na ukweli na kuelekea kwenye urongo?
アラビア語 クルアーン注釈:
ٱتَّخَذُوٓاْ أَحۡبَارَهُمۡ وَرُهۡبَٰنَهُمۡ أَرۡبَابٗا مِّن دُونِ ٱللَّهِ وَٱلۡمَسِيحَ ٱبۡنَ مَرۡيَمَ وَمَآ أُمِرُوٓاْ إِلَّا لِيَعۡبُدُوٓاْ إِلَٰهٗا وَٰحِدٗاۖ لَّآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۚ سُبۡحَٰنَهُۥ عَمَّا يُشۡرِكُونَ
Mayahudi na Wanaswara wamewafanya wanavyuoni na watu wema kuwa ni waola wenye kuwaekea hukumu za sheria, wakawa wanajilazimisha kuzifuata na wanaacha sheria za Mwenyezi Mungu. Na pia walimfanya Al- Masīḥ, 'Īsā mwana wa Maryam, kuwa ni mungu, wakamuabudu. Na hakika Mwenyezi Mungu Amewaamrisha wao wamuabudu Yeye Peke Yake, bila ya mwingine. Yeye Ndiye Mungu wa haki. Hakuna mungu anayestahiki kuabudiwa kwa haki isipokuwa Yeye. Amejiepusha na Ametakasika na kila kile wanachokizua watu wa ushirikina na upotevu.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 章: 悔悟章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis - 対訳の目次

Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

閉じる