クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany * - 対訳の目次

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

対訳 節: (88) 章: ユースフ章
فَلَمَّا دَخَلُواْ عَلَيۡهِ قَالُواْ يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡعَزِيزُ مَسَّنَا وَأَهۡلَنَا ٱلضُّرُّ وَجِئۡنَا بِبِضَٰعَةٖ مُّزۡجَىٰةٖ فَأَوۡفِ لَنَا ٱلۡكَيۡلَ وَتَصَدَّقۡ عَلَيۡنَآۖ إِنَّ ٱللَّهَ يَجۡزِي ٱلۡمُتَصَدِّقِينَ
Basi walipo ingia kwa Yusuf walisema: Ewe Mheshimiwa! Imetupata shida, sisi na watu wetu. Na tumeleta mali kidogo. Basi tupimie kipimo na fanya kama unatupa sadaka. Hakika Mwenyezi Mungu huwalipa watoao sadaka.
Nduguze Yusuf walimwitikia baba yao kwa matakwa yake. Wakatoka kwenda Misri, na wakajaribu kukutana na mtawala wake ambaye baadae ikadhihiri kuwa ndiye Yusuf! Walipo ingia kwake walisema: Ewe Mheshimiwa! Sisi na watu wetu tumepata shida ya njaa na madhara ya mwili na nafsi. Na tumekuletea mali chache ndio bidhaa yetu. Nayo ni ya kukataliwa kwa kuwa ni kidogo na mbaya, wala haitoshi kwa hayo tunayo taraji kwako. Lakini sisi tunataraji kwako utupimie kwa ukamilifu na utacho tuzidishia kiwe ni sadaka unayo tupa. Kwani hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu huwalipa wenye kutoa sadaka thawabu njema kabisa.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 節: (88) 章: ユースフ章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany - 対訳の目次

クルアーン・スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany

閉じる