クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany * - 対訳の目次

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

対訳 節: (55) 章: 夜の旅章
وَرَبُّكَ أَعۡلَمُ بِمَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۗ وَلَقَدۡ فَضَّلۡنَا بَعۡضَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ عَلَىٰ بَعۡضٖۖ وَءَاتَيۡنَا دَاوُۥدَ زَبُورٗا
Na Mola wako Mlezi anawajua vilivyo waliomo mbinguni na katika ardhi. Na hakika tumewafadhilisha baadhi ya Manabii kuliko wengine; na Daudi tulimpa Zaburi.
Na Mola wako Mlezi anajua vilivyo vyote viliomo mbinguni na ardhini, na anajua hali zao. Basi anawakhiari miongoni mwao kwa kuwapa Unabii awatakao. Naye amekukhiari wewe kwa kukupa Utume wake. Basi haiwafalii wao kuudhika na Unabii wako. Na hao Manabii si wote sawa sawa kwa daraja mbele yake Aliye tukuka shani yake. Bali baadhi yao ni bora kuliko wenginewe. Naye amewatukuza baadhi ya Manabii juu ya wengine kwa miujiza, na wingi wa wafwasi, si kwa ufalme. Basi alitukuzwa Daudi kwa kuwa kapewa Zaburi, si kwa kuwa kapewa ufalme. Basi hapana ajabu kuwa wewe, Muhammad, ukapata fadhila kubwa kabisa kwa kuwa umepewa Qur'ani.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 節: (55) 章: 夜の旅章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany - 対訳の目次

クルアーン・スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany

閉じる