クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany * - 対訳の目次

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

対訳 節: (76) 章: 物語章
۞ إِنَّ قَٰرُونَ كَانَ مِن قَوۡمِ مُوسَىٰ فَبَغَىٰ عَلَيۡهِمۡۖ وَءَاتَيۡنَٰهُ مِنَ ٱلۡكُنُوزِ مَآ إِنَّ مَفَاتِحَهُۥ لَتَنُوٓأُ بِٱلۡعُصۡبَةِ أُوْلِي ٱلۡقُوَّةِ إِذۡ قَالَ لَهُۥ قَوۡمُهُۥ لَا تَفۡرَحۡۖ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ ٱلۡفَرِحِينَ
Hakika Qaruni alikuwa katika watu wa Musa, lakini aliwafanyia dhulma. Na tulimpa khazina ambazo funguo zake zinawatopeza watu wenye nguvu kuzichukua. Walipo mwambia watu wake: Usijigambe! Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi wanao jigamba.
Sura hii inasimulia kisa cha Qaruni. Naye alikuwa katika kaumu ya Musa. Akapanda kiburi juu yao kwa kughurika kwa nafsi yake na mali yake. Na Mwenyezi Mungu alikuwa kampa khazina za mali mengi. Hata ikawa funguo zake tu zikiwaemea kundi la wanaume wenye nguvu! Na alipo ghurika na neema ya Mwenyezi Mungu juu yake, na akakufuru kwa sababu yake, watu walimpa nasaha, wakamwambia: Usidanganyike kwa mali yako, wala furaha kwa ajili yake isikusaliti hata ukaacha kumshukuru Mwenyezi Mungu. Kwani hakika Mwenyezi Mungu hawapendi watu walio danganyika na wakasalitika. Na funzo la kisa hichi ni kuwa makafiri walio mkataa Muhammad s.a.w. walighurika na mali yao. Basi Qur'ani inawaelezea kuwa mali yao si chochote cha kutajika ukilinganisha na mali ya Qaruni.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 節: (76) 章: 物語章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany - 対訳の目次

クルアーン・スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany

閉じる