クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany * - 対訳の目次

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

対訳 節: (38) 章: 戦利品章
قُل لِّلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِن يَنتَهُواْ يُغۡفَرۡ لَهُم مَّا قَدۡ سَلَفَ وَإِن يَعُودُواْ فَقَدۡ مَضَتۡ سُنَّتُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Waambie wale walio kufuru: Wakikoma watasamehewa yaliyo kwisha pita. Na wakiyarudia basi imekwisha pita mifano ya wa zamani.
Hakika juu ya vitisho hivi, mlango wa matarajio ungali wazi. Basi ewe Nabii wa rehema! Waambie hawa wapinzani kuwa wakikoma, wakaacha inadi yao na ushirikina wao, basi hapana shaka Mwenyezi Mungu atawasamehe vile vitendo vyao vilivyo kwisha pita. Na wakiendelea na upotovu wao, na wakarudia tena kukupigeni vita, basi mwendo wa Haki kwa walio tangulia umethibiti utakuwa ule ule, nao ni kuwa Haki lazima iushinde upotovu, pindi ikiwa wale watu wa Haki wakishika ut'iifu na njia za ushindi.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 節: (38) 章: 戦利品章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany - 対訳の目次

クルアーン・スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany

閉じる