Check out the new design

ಪವಿತ್ರ ಕುರ್‌ಆನ್ ಅರ್ಥಾನುವಾದ - ಸ್ವಾಹಿಲಿ ಅನುವಾದ - ಅಲಿ ಮುಹ್ಸಿನ್ ಅಲ್-ಬರ್ವಾನಿ * - ಅನುವಾದಗಳ ವಿಷಯಸೂಚಿ

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

ಅರ್ಥಗಳ ಅನುವಾದ ಅಧ್ಯಾಯ: ಅನ್ನಹ್ಲ್   ಶ್ಲೋಕ:
وَٱللَّهُ جَعَلَ لَكُم مِّنۢ بُيُوتِكُمۡ سَكَنٗا وَجَعَلَ لَكُم مِّن جُلُودِ ٱلۡأَنۡعَٰمِ بُيُوتٗا تَسۡتَخِفُّونَهَا يَوۡمَ ظَعۡنِكُمۡ وَيَوۡمَ إِقَامَتِكُمۡ وَمِنۡ أَصۡوَافِهَا وَأَوۡبَارِهَا وَأَشۡعَارِهَآ أَثَٰثٗا وَمَتَٰعًا إِلَىٰ حِينٖ
Na Mwenyezi Mungu amekujaalieni majumba yenu yawe ni maskani yenu, na amekujaalieni kutokana na ngozi za wanyama nyumba mnazo ziona nyepesi wakati wa safari zenu na wakati wa kutua kwenu. Na kutokana na sufi zao na manyoya yao na nywele zao mnafanya matandiko na mapambo ya kutumia kwa muda.
Na Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taa'la ndiye aliye kujaalieni mkaweza kusimamisha nyumba zenu ili ziwe maskani yenu. Na akakujaalieni kutokana na ngozi za ngamia, na ng'ombe, na kondoo na wanyama wengineo mkafanya mahema ambayo ni kama nyumba za kukalia, na mkihama nayo mnapo safiri na mnapo tua. Na kutokana na sufi zao, na nywele zao, na manyoya yao, mkafanya matandiko ya kutumia hapa duniani mpaka itakapo fika ajali yenu ya kuondoka.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَٱللَّهُ جَعَلَ لَكُم مِّمَّا خَلَقَ ظِلَٰلٗا وَجَعَلَ لَكُم مِّنَ ٱلۡجِبَالِ أَكۡنَٰنٗا وَجَعَلَ لَكُمۡ سَرَٰبِيلَ تَقِيكُمُ ٱلۡحَرَّ وَسَرَٰبِيلَ تَقِيكُم بَأۡسَكُمۡۚ كَذَٰلِكَ يُتِمُّ نِعۡمَتَهُۥ عَلَيۡكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تُسۡلِمُونَ
Na Mwenyezi Mungu amekufanyieni vivuli katika vitu alivyo viumba,na amekufanyieni maskani milimani, na amekufanyieni nguo za kukingeni na joto, na nguo za kukingeni katika vita vyenu. Ndio hivyo anakutimizieni neema zake ili mpate kut'ii.
Na Mwenyezi Mungu amekuumbieni miti na vitu vyenginevyo vya kukupeni vivuli kukulindeni na taabu ya joto, na amekufanyieni mapango milimani, nanyi mkafanya humo maskani kama nyumba. Pia amekuumbieni nguo za sufi na pamba na kitani na vyenginevyo, ili kukuhifadhini na joto la jua, na nguo za chuma za kukulindeni katika vita na adui zenu. Kama alivyo kujaalieni hayo, basi kadhaalika amekutimizieni neema zake kwa kukupeni Dini iliyo simama sawa, ili mpate kuifuata amri yake, na mumsafie ibada Yeye tu si na mwenginewe.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّمَا عَلَيۡكَ ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ
Basi wakikengeuka lilio juu yako wewe ni kufikisha ujumbe waziwazi.
Wakikupuuza, ewe Nabii, hao unao waita wafuate Uislamu, basi wewe huna jukumu kwa mapuuza yao. Haikulazimu wewe ila kufikisha ujumbe kwa uwazi, na hayo umekwisha fanya.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
يَعۡرِفُونَ نِعۡمَتَ ٱللَّهِ ثُمَّ يُنكِرُونَهَا وَأَكۡثَرُهُمُ ٱلۡكَٰفِرُونَ
Wanazijua neema za Mwenyezi Mungu, kisha wanazikanusha; na wengi wao ni makafiri.
Kupuuza kwao hao makafiri si kwa kuwa hawajui kwamba Mwenyezi Mungu Subhanahu ndiye chanzo cha kila neema zote wanazo zipata, lakini wao hutenda vitendo vya wanao kanya neema, kwa vile hawamshukuru Mola Mlezi kwazo. Na wengi wao wamekazania kuwafuata baba zao katika kumkataa Mwenyezi Mungu, mpaka wakawa wengi wao ndio wapinzani.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَيَوۡمَ نَبۡعَثُ مِن كُلِّ أُمَّةٖ شَهِيدٗا ثُمَّ لَا يُؤۡذَنُ لِلَّذِينَ كَفَرُواْ وَلَا هُمۡ يُسۡتَعۡتَبُونَ
Na siku tutakapo wainua kutokana na kila umma shahidi, kisha hawataruhusiwa walio kufuru wala hawataachiliwa kutaka radhi.
Ewe Nabii! Mhadharishe kila anaye mkataa Mola wake Mlezi kwa yatakayo tokea Siku tutakapo muinua kutokana na kila umma shahidi wa kuwashuhudia kwa walivyo mpokea Mtume wa Mola wao Mlezi. Na pindi akitaka kafiri kutoa udhuru, hatapewa ruhusa ya kutaka kutoa udhuru. Wala hatapatikana mwombezi wa kumtengenezea maombezi, kwa kutakiwa warejee waache sababu za Mwenyezi Mungu kuwakasirikia. Kwani Akhera sio pahala pa kutubia.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَإِذَا رَءَا ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ ٱلۡعَذَابَ فَلَا يُخَفَّفُ عَنۡهُمۡ وَلَا هُمۡ يُنظَرُونَ
Na walio dhulumu watakapo iona adhabu hawatapunguziwa hiyo adhabu,wala hawatapewa muhula.
Na wale walio jidhullumu nafsi zao kwa kukufuru watakapo iona Jahannamu, na wakataka wapunguziwe adhabu, hawato jibiwa, wala hawato akhirishwa kuingia Jahannamu hata dakika moja.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَإِذَا رَءَا ٱلَّذِينَ أَشۡرَكُواْ شُرَكَآءَهُمۡ قَالُواْ رَبَّنَا هَٰٓؤُلَآءِ شُرَكَآؤُنَا ٱلَّذِينَ كُنَّا نَدۡعُواْ مِن دُونِكَۖ فَأَلۡقَوۡاْ إِلَيۡهِمُ ٱلۡقَوۡلَ إِنَّكُمۡ لَكَٰذِبُونَ
Na walio shirikisha watakapo waona hao walio washirikisha na Mwenyezi Mungu, watasema: Mola wetu Mlezi! Hawa ndio washirikishwa wetu ambao tulikuwa tukiwaabudu badala yako. Ndipo wale watakapo watupia kauli:Hakika nyinyi ni waongo!
Na walio wafanya miungu yao washirika wa Mwenyezi Mungu na wakawaabudu watapo sema: Ewe Mola Mlezi wetu! Hawa ndio washirikishwa wetu tulio tukiwaabudu kwa makosa. Basi tupunguzie adhabu kwa kuwapa wao baadhi ya adhabu! Washirikishwa wao watajibu: Ama hakika nyinyi washirikina waongo kwa kudai kwenu kuwa sisi ni washirika wa Mwenyezi Mungu, na kwamba nyinyi mkituabudu! La kweli ni kuwa mkiabudu matamanio yenu tu, wala sisi hatukuwa washirika kama mlivyo dai. (Nabii Isa a.s. amesema: "Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe, ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu." - Injili ya Mathayo 7.21-27)
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَأَلۡقَوۡاْ إِلَى ٱللَّهِ يَوۡمَئِذٍ ٱلسَّلَمَۖ وَضَلَّ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ
Na siku hiyo watasalimu amri mbele ya Mwenyezi Mungu, na yatapotea waliyo kuwa wakiyazua.
Hapo tena wale washirikina walio mshirikisha Mwenyezi Mungu watasalimu amri, waikubali hukumu yake, na yawaondokee yale mawazo yao kwamba walio kuwa wakiwaabudu yatakuja waombea na kuwakinga na adhabu!
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
 
ಅರ್ಥಗಳ ಅನುವಾದ ಅಧ್ಯಾಯ: ಅನ್ನಹ್ಲ್
ಅಧ್ಯಾಯಗಳ ವಿಷಯಸೂಚಿ ಪುಟ ಸಂಖ್ಯೆ
 
ಪವಿತ್ರ ಕುರ್‌ಆನ್ ಅರ್ಥಾನುವಾದ - ಸ್ವಾಹಿಲಿ ಅನುವಾದ - ಅಲಿ ಮುಹ್ಸಿನ್ ಅಲ್-ಬರ್ವಾನಿ - ಅನುವಾದಗಳ ವಿಷಯಸೂಚಿ

ಅನುವಾದ - ಅಲಿ ಮುಹ್ಸಿನ್ ಅಲ್-ಬರ್ವಾನಿ

ಮುಚ್ಚಿ