Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Ali Muchsen Al-Beruany * - Vertimų turinys

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Reikšmių vertimas Sūra: Sūra Al- ʻAadijaat   Aja (Korano eilutė):

Surat Al-Aadiyat

وَٱلۡعَٰدِيَٰتِ ضَبۡحٗا
Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,
Ninaapa kwa farasi wa Jihadi wendao mbio, na huku pumzi zao zinasikilizana kwa sauti inayo itwa "Dh'abh'an".
Tafsyrai arabų kalba:
فَٱلۡمُورِيَٰتِ قَدۡحٗا
Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,
Na kwa farasi hao ambao hutoa cheche za moto zinapo gonga kwato zao kwenye ardhi wanapo kwenda.
Tafsyrai arabų kalba:
فَٱلۡمُغِيرَٰتِ صُبۡحٗا
Wakishambulia wakati wa asubuhi,
Na kwa farasi hao wanao washambulia maadui asubuhi kabla jua halijachomoza;
Tafsyrai arabų kalba:
فَأَثَرۡنَ بِهِۦ نَقۡعٗا
Huku wakitimua vumbi,
Wakatimua mavumbia mengi, farasi hao, kati ya makundi ya maadui!
Tafsyrai arabų kalba:
فَوَسَطۡنَ بِهِۦ جَمۡعًا
Na wakijitoma kati ya kundi,
Ikawa vumbi limewagubika maadui hata wakaingiwa kiwewe na kufazaika.
Tafsyrai arabų kalba:
إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٞ
Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!
Hakika mwanaadamu ni mwingi wa kuzikufuru neema za Mola wake Mlezi ambazo hazikadiriki.
Tafsyrai arabų kalba:
وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٞ
Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka atakuwa mwingi wa kuja jishuhudia huko Akhera kwa kuungama madhambi yake.
Tafsyrai arabų kalba:
وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلۡخَيۡرِ لَشَدِيدٌ
Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
Na hakika yeye kwa uchoyo na kuyapenda mali alio nayo, ni bakhili, hatoi kama inavyo mwajibikia katika mali yake.
Tafsyrai arabų kalba:
۞ أَفَلَا يَعۡلَمُ إِذَا بُعۡثِرَ مَا فِي ٱلۡقُبُورِ
Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
Kwani hajui mwisho wa hali yake, hata hajui wakitolewa maiti waliomo makaburini,
Tafsyrai arabų kalba:
وَحُصِّلَ مَا فِي ٱلصُّدُورِ
Na yakakusanywa yaliomo vifuani?
Na vikakusanywa viliomo vifuani navyo vimekwisha sajiliwa katika madaftari yao, yakiwa mema au mabaya waliyo yatenda?
Tafsyrai arabų kalba:
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّخَبِيرُۢ
Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!
Kwamba hakika Mlezi wao na Muumba wao bila ya shaka anajua vyema vitendo vyao na malipo yao Siku ya Kufufuliwa na Kulipwa.
Tafsyrai arabų kalba:
 
Reikšmių vertimas Sūra: Sūra Al- ʻAadijaat
Sūrų turinys Puslapio numeris
 
Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Ali Muchsen Al-Beruany - Vertimų turinys

Kilniojo Korano reikšmių vertimas į suahilių k., išvertė Ali Muchsin Al-Birvany.

Uždaryti