Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo saawaahiliiwo - Ali Muhsin Al-barwaany * - Tippudi firooji ɗii

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Firo maanaaji Simoore: Simoore al-adiya   Aaya:

Surat Al-Aadiyat

وَٱلۡعَٰدِيَٰتِ ضَبۡحٗا
Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,
Ninaapa kwa farasi wa Jihadi wendao mbio, na huku pumzi zao zinasikilizana kwa sauti inayo itwa "Dh'abh'an".
Faccirooji aarabeeji:
فَٱلۡمُورِيَٰتِ قَدۡحٗا
Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,
Na kwa farasi hao ambao hutoa cheche za moto zinapo gonga kwato zao kwenye ardhi wanapo kwenda.
Faccirooji aarabeeji:
فَٱلۡمُغِيرَٰتِ صُبۡحٗا
Wakishambulia wakati wa asubuhi,
Na kwa farasi hao wanao washambulia maadui asubuhi kabla jua halijachomoza;
Faccirooji aarabeeji:
فَأَثَرۡنَ بِهِۦ نَقۡعٗا
Huku wakitimua vumbi,
Wakatimua mavumbia mengi, farasi hao, kati ya makundi ya maadui!
Faccirooji aarabeeji:
فَوَسَطۡنَ بِهِۦ جَمۡعًا
Na wakijitoma kati ya kundi,
Ikawa vumbi limewagubika maadui hata wakaingiwa kiwewe na kufazaika.
Faccirooji aarabeeji:
إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٞ
Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!
Hakika mwanaadamu ni mwingi wa kuzikufuru neema za Mola wake Mlezi ambazo hazikadiriki.
Faccirooji aarabeeji:
وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٞ
Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka atakuwa mwingi wa kuja jishuhudia huko Akhera kwa kuungama madhambi yake.
Faccirooji aarabeeji:
وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلۡخَيۡرِ لَشَدِيدٌ
Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
Na hakika yeye kwa uchoyo na kuyapenda mali alio nayo, ni bakhili, hatoi kama inavyo mwajibikia katika mali yake.
Faccirooji aarabeeji:
۞ أَفَلَا يَعۡلَمُ إِذَا بُعۡثِرَ مَا فِي ٱلۡقُبُورِ
Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
Kwani hajui mwisho wa hali yake, hata hajui wakitolewa maiti waliomo makaburini,
Faccirooji aarabeeji:
وَحُصِّلَ مَا فِي ٱلصُّدُورِ
Na yakakusanywa yaliomo vifuani?
Na vikakusanywa viliomo vifuani navyo vimekwisha sajiliwa katika madaftari yao, yakiwa mema au mabaya waliyo yatenda?
Faccirooji aarabeeji:
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّخَبِيرُۢ
Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!
Kwamba hakika Mlezi wao na Muumba wao bila ya shaka anajua vyema vitendo vyao na malipo yao Siku ya Kufufuliwa na Kulipwa.
Faccirooji aarabeeji:
 
Firo maanaaji Simoore: Simoore al-adiya
Tippudi cimooje Tonngoode hello ngoo
 
Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo - Firo saawaahiliiwo - Ali Muhsin Al-barwaany - Tippudi firooji ɗii

Firo maanaaji al-quraan tedduɗo oo fayde e ɗemngal sawahili, firi ɗum ko Ali Muhsin Al-barwani

Uddude