Check out the new design

വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്. * - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക


പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: ഇസ്റാഅ്   ആയത്ത്:
وَإِذَا مَسَّكُمُ ٱلضُّرُّ فِي ٱلۡبَحۡرِ ضَلَّ مَن تَدۡعُونَ إِلَّآ إِيَّاهُۖ فَلَمَّا نَجَّىٰكُمۡ إِلَى ٱلۡبَرِّ أَعۡرَضۡتُمۡۚ وَكَانَ ٱلۡإِنسَٰنُ كَفُورًا
Na mkipatikana na shida baharini mkakaribia kuzama na kuangamia, wanapotea kwenye akili zenu wale waungu ambao mlikuwa mkiwaabudu, na mkamkumbuka Mwenyezi Mungu Muweza, Peke Yake, Awasaidie na Awaokoe, hapo mnamtakasia katika kutaka msaada na uokzi, na Yeye Anawasaidia na Anawaokoa. Anapowaokoa kwa kuwaegesha kwenye nchi kavu, mnageuka mkaacha Imani, kumtakasia Mwenyezi Mungu na matendo mema. Na huu ni katika ujinga wa binadamu na ukafirir wake, kwani binadamu ni mkanushaji sana neema za Mwenyezi Mungu, Aliyeshinda na kutukuka.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَفَأَمِنتُمۡ أَن يَخۡسِفَ بِكُمۡ جَانِبَ ٱلۡبَرِّ أَوۡ يُرۡسِلَ عَلَيۡكُمۡ حَاصِبٗا ثُمَّ لَا تَجِدُواْ لَكُمۡ وَكِيلًا
Je, mumeghafilika, enyi watu, na adhabu ya Mwenyezi Mungu, ndipo mkajiaminisha kwamba ardhi haitawaporomokea ikawadidimiza au kwamba Mwenyezi Mungu Hatawanyesheza mvua ya mawe itokayo juu iwaue kisha msipate yoyote wa kuwalinda na adhabu Yake?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ أَمِنتُمۡ أَن يُعِيدَكُمۡ فِيهِ تَارَةً أُخۡرَىٰ فَيُرۡسِلَ عَلَيۡكُمۡ قَاصِفٗا مِّنَ ٱلرِّيحِ فَيُغۡرِقَكُم بِمَا كَفَرۡتُمۡ ثُمَّ لَا تَجِدُواْ لَكُمۡ عَلَيۡنَا بِهِۦ تَبِيعٗا
Au mumejiaminisha, enyi watu, kwamba Mola wenu, na hali nyinyi mumemkanusha, hatawarudisha baharini mara nyingine kisha akawaletea kimbunga kikali chenye kuvunjavunja kila kitu kinachokifikia, kikaja kikawazamisha kwa ukanushaji wenu, kisha msipate kitu chochote cha madai au malalamiko juu yetu, kwa kuwa Mwenyezi Mungu hakuwadhulumu kitu chochote hata wizani wa chungu mdogo?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
۞ وَلَقَدۡ كَرَّمۡنَا بَنِيٓ ءَادَمَ وَحَمَلۡنَٰهُمۡ فِي ٱلۡبَرِّ وَٱلۡبَحۡرِ وَرَزَقۡنَٰهُم مِّنَ ٱلطَّيِّبَٰتِ وَفَضَّلۡنَٰهُمۡ عَلَىٰ كَثِيرٖ مِّمَّنۡ خَلَقۡنَا تَفۡضِيلٗا
Kwa hakika tumewatukuza watu wa kizazi cha Ādam kwa akili na kuwapelekea Mitume, na tukawadhalilishia vilivyoko ulimwenguni vyote: tukawadhalilishia wanyama barani wa kuwapanda na vyombo baharini vya kuwabeba, tukawaruzuku vilaji na vinywaji vizuri na tukawapa daraja kubwa juu ya viumbe wengi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
يَوۡمَ نَدۡعُواْ كُلَّ أُنَاسِۭ بِإِمَٰمِهِمۡۖ فَمَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ فَأُوْلَٰٓئِكَ يَقۡرَءُونَ كِتَٰبَهُمۡ وَلَا يُظۡلَمُونَ فَتِيلٗا
Na kumbuka, ewe Mtume, Siku ya Kufufuliwa, kwa njia ya kutoa bishara na kuogopesha, pindi Mwenyezi Mungu, Aliyeshinda na ktukuka, Atakapoliita kila kundi la watu pamoja na kiongozi wao ambaye walikuwa wakimfuata ulimwenguni. Basi aliyekuwa mwema kati yao , na akapewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, hawa watasoma kitabu cha mema yao wakiwa katika hali ya kufurahika na kuterema, na kamwe hawatapunguziwa chochote katika malipo ya matendo yao mazuri, hata kama ni kadiri ya uzi unaokuwa kwenye mpasuko wa koko ya tende.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَمَن كَانَ فِي هَٰذِهِۦٓ أَعۡمَىٰ فَهُوَ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ أَعۡمَىٰ وَأَضَلُّ سَبِيلٗا
Na aliyekuwa kipofu wa moyo, katika ulimwengu huu, wa kutoziona dalili za uweza wa Mwenyezi Mungu, asiyaamini yale aliyokuja nayo Mtume Muhammad, rehema na amani zimshukiye, basi yeye, Siku ya Kiyama, atakuwa kipofu zaidi wa kutoiona njia ya Peponi na atapotea zaidi njia ya uongofu na usawa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِن كَادُواْ لَيَفۡتِنُونَكَ عَنِ ٱلَّذِيٓ أَوۡحَيۡنَآ إِلَيۡكَ لِتَفۡتَرِيَ عَلَيۡنَا غَيۡرَهُۥۖ وَإِذٗا لَّٱتَّخَذُوكَ خَلِيلٗا
Na kwa hakika washirikina walikaribia kukuepusha, ewe Mtume, na Qur’ani Aliyokuteremshia Mwenyezi Mungu ili utuzulie isiyokuwa hiyo tuliyokuletea wahyi nayo. Na lau ulifanya walivyotaka, wangalikufanya ni kipenzi msafiwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَلَوۡلَآ أَن ثَبَّتۡنَٰكَ لَقَدۡ كِدتَّ تَرۡكَنُ إِلَيۡهِمۡ شَيۡـٔٗا قَلِيلًا
Na lau si sisi kukuimarisha kwenye haki na kukuhifadhi usikubaliane nao, ungalikaribia kuelemea kwao kidogo katika yale waliyokushauri kwa nguvu za udanganyifu wao na wingi wa hila zao na kuwa na hamu kwako waongoke.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِذٗا لَّأَذَقۡنَٰكَ ضِعۡفَ ٱلۡحَيَوٰةِ وَضِعۡفَ ٱلۡمَمَاتِ ثُمَّ لَا تَجِدُ لَكَ عَلَيۡنَا نَصِيرٗا
Na lau ulielemea, ewe Mtume, upande wa hawa washirikina maelemeo madogo katika yale waliyotaka kwako, basi tungalikuonjesha mara mbili zaidi ya adhabu ya duniani na mara mbili zaidi ya adhabu ya baada ya kufa kesho Akhera, hivyo ni kwa ajili ya kutimia neema ya Mwenyezi Mungu kwako na ukamilifu wa kumjua Mola wako, kisha hutampata yoyote mwenye kukuepushia adhabu yetu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
 
പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: ഇസ്റാഅ്
സൂറത്തുകളുടെ സൂചിക പേജ് നമ്പർ
 
വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്. - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക

വിവർത്തനം: ഡോ. അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് അബൂബക്കർ & ശൈഖ് നാസ്വിർ ഖമീസ്

അടക്കുക