Check out the new design

വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്. * - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക


പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: ബഖറഃ   ആയത്ത്:
إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡهِمۡ ءَأَنذَرۡتَهُمۡ أَمۡ لَمۡ تُنذِرۡهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ
Hakika wale walioyakanusha yalioteremshwa kwako kutoka kwa Mola Wako, kwa njia ya kiburi na ujeuri, hakutapatikana kuamini kutoka kwao; ni sawa kwao ukiwa utawatisha na kuwaonya adhabu ya Mwenyezi Mungu au utaacha kufanya hivyo, kwa sababu wao wameamua kukakamia kwenye njia yao ya batili.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
خَتَمَ ٱللَّهُ عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ وَعَلَىٰ سَمۡعِهِمۡۖ وَعَلَىٰٓ أَبۡصَٰرِهِمۡ غِشَٰوَةٞۖ وَلَهُمۡ عَذَابٌ عَظِيمٞ
Mwenyezi Mungu amewapiga muhuri nyoyo zao, masikizi yao na ameweka finiko juu ya macho yao ya kuonea kwa sababu ya ukafiri na ujeuri walionao, baada ya haki kuwabainikia. Mwenyezi Mungu hakuwaafikia kwenye uongofu. Wao watapata adhabu kali katika Moto wa Jahanamu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَمِنَ ٱلنَّاسِ مَن يَقُولُ ءَامَنَّا بِٱللَّهِ وَبِٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَمَا هُم بِمُؤۡمِنِينَ
Miongoni mwa watu kuna kundi linalokuwa katika hali ya kutokuwa na uamuzi, linasimama baina ya Waumini na makafiri, nao ni wanafiki wanaosema kwa ndimi zao, “Tumemuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho,’ na hali wao, katika undani yao, ni warongo, hawakuamini.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
يُخَٰدِعُونَ ٱللَّهَ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَمَا يَخۡدَعُونَ إِلَّآ أَنفُسَهُمۡ وَمَا يَشۡعُرُونَ
Wanaitakidi, kwa ujinga wao, kuwa wao wanamdanganya Mwenyezi Mungu na Waumini, kwa kudhihirisha kwao Imani na kuficha kwao ukafiri, na wao hawamdanganyi yoyote isipokuwa nafsi zao wenyewe, kwa kuwa madhara ya kudanganya kwao yanawarudia wao. Na kwa kuwa ujinga wao umekolea na nyoyo zao zimeharibika, huwa hawana hisia ya hilo.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ فَزَادَهُمُ ٱللَّهُ مَرَضٗاۖ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمُۢ بِمَا كَانُواْ يَكۡذِبُونَ
Ndani ya nyoyo zao kuna shaka na uharibifu, ndipo wakaomjwa kwa kufanya maasia yenye kuwafanya wastahiki kuadhibiwa, na Mwenyezi Mungu akawazidishia shaka. Watakuwa na adhabu yenye uchungu kwa sababu ya urongo na unafiki wao.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِذَا قِيلَ لَهُمۡ لَا تُفۡسِدُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ قَالُوٓاْ إِنَّمَا نَحۡنُ مُصۡلِحُونَ
Wanapopewa nasaha wakome kufanya uharibifu katika ardhi kwa kukanusha na kuasi kutoa siri za Waumini na kuwategemea makafiri, huwa wakisema kwa urongo na kubisha, “Sisi ndio watu wakutengeneza.”
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَلَآ إِنَّهُمۡ هُمُ ٱلۡمُفۡسِدُونَ وَلَٰكِن لَّا يَشۡعُرُونَ
Hili wanalolifanya na kudai kuwa ni utengefu ndio uharibifu wenyewe, lakini wao, kwa ujinga wao na ujeuri wao, hawana hisia ya hilo.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِذَا قِيلَ لَهُمۡ ءَامِنُواْ كَمَآ ءَامَنَ ٱلنَّاسُ قَالُوٓاْ أَنُؤۡمِنُ كَمَآ ءَامَنَ ٱلسُّفَهَآءُۗ أَلَآ إِنَّهُمۡ هُمُ ٱلسُّفَهَآءُ وَلَٰكِن لَّا يَعۡلَمُونَ
Na waambiwapo wanafiki, “Aminini kama walivyoamini masahaba, nako ni kuamini kwa moyo, ulimi na viungo,” huwa wakibisha na kusema, “Basi, tuamini kama vile madhaifu wa akili na maoni walivyoamini, tuwe kama wao katika upumbavu?” Mwenyezi Mungu aliwajibu kwamba udhaifu wa akili na maoni ni wao peke yao. Na wao hawajui kuwa msimamo walionao ndio upotevu na hasara.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِذَا لَقُواْ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ قَالُوٓاْ ءَامَنَّا وَإِذَا خَلَوۡاْ إِلَىٰ شَيَٰطِينِهِمۡ قَالُوٓاْ إِنَّا مَعَكُمۡ إِنَّمَا نَحۡنُ مُسۡتَهۡزِءُونَ
Hawa wanafiki wakikutana na waumini huwa wakisema, “Tumeiamini Dini ya Uislamu kama nyinyi,” na wakiondoka kwenda kwa viongozi wao makafiri wasiomjalli Mwenyezi Mungu, huwa wakiwahakikishia kuwa wao wako kwenye mila ya ukafiri, hawajaiacha, na kuwa wao walikuwa wakiwacheza shere waumini.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ٱللَّهُ يَسۡتَهۡزِئُ بِهِمۡ وَيَمُدُّهُمۡ فِي طُغۡيَٰنِهِمۡ يَعۡمَهُونَ
Mwenyezi Mungu anawacheza shere wao na kuwapa muhula, ili wazidi kupotea, kuwa na shaka na kutokuwa na uamuzi, na Atawalipa kwa kuwacheza shere kwao Waislamu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أُوْلَٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ ٱشۡتَرَوُاْ ٱلضَّلَٰلَةَ بِٱلۡهُدَىٰ فَمَا رَبِحَت تِّجَٰرَتُهُمۡ وَمَا كَانُواْ مُهۡتَدِينَ
Hao ndio wanafiki. Wamejiuza wenyewe katika mapatano ya hasara. Walichukuwa ukafiri na kuacha Imani. Hawakupata faida yoyote, bali walipata hasara ya kukosa uongofu. Huko ndiko kupata hasara kukubwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
 
പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: ബഖറഃ
സൂറത്തുകളുടെ സൂചിക പേജ് നമ്പർ
 
വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്. - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക

ഡോ. അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് അബൂബക്കർ & ശൈഖ് നാസ്വിർ ഖമീസ്

അടക്കുക