Check out the new design

വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്. * - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക


പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: ന്നംല്   ആയത്ത്:
وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَآ إِلَىٰ ثَمُودَ أَخَاهُمۡ صَٰلِحًا أَنِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ فَإِذَا هُمۡ فَرِيقَانِ يَخۡتَصِمُونَ
Hakika tulimtumiliza kwa watu wa Thamūd ndugu yao Ṣāliḥ kwamba: Mpwekesheni Mwenyezi Mungu na musimchukue mungu mwingine mukamuabudu pamoja na Yeye. Alipowajia Ṣāliḥ kuwalingania kwenye kumpwekesha Mwenyezi Mungu na kumuabudu Peke Yake, watu wake walikuwa mapote mawili: mojawapo ya mapote mawili lilimuamini na lingine liliukanusha ulinganizi wake, kila mmoja kati ya watu wa mapote hayo mawili alikuwa akidai kwamba haki iko pamoja na yeye.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالَ يَٰقَوۡمِ لِمَ تَسۡتَعۡجِلُونَ بِٱلسَّيِّئَةِ قَبۡلَ ٱلۡحَسَنَةِۖ لَوۡلَا تَسۡتَغۡفِرُونَ ٱللَّهَ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ
Ṣāliḥ alisema kuliambia pote lililokanusha, «Kwa nini mnaharakisha ukanushaji na kufanya matendo mabaya ambayo yatawaletea adhabu na mnachelewesha kuamini na kufanya matendo mema ambayo yatawaletea malipo mazuri? Si mutake msamaha kutoka kwa Mwenyezi Mungu mwanzo na mtubie kwake kwa matumaini ya kurehemewa.»
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالُواْ ٱطَّيَّرۡنَا بِكَ وَبِمَن مَّعَكَۚ قَالَ طَٰٓئِرُكُمۡ عِندَ ٱللَّهِۖ بَلۡ أَنتُمۡ قَوۡمٞ تُفۡتَنُونَ
Wakasema watu wa Ṣāliḥ kumwambia, «Tumepata ukorofi kwa sababu yako wewe na watu walioko na wewe kati ya wale walioingia katika dini yako.» Ṣāliḥ aliwaambia, «Wema Anaowapatia Mwenyezi Mungu au uovu, basi hua umekadiriwa kwenu na Mwenyezi Mungu na Atawapa malipo yake. Bali nyinyi ni watu ambao mtapewa mtihani wa mambo ya furaha na maudhiko na mema na maovu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَكَانَ فِي ٱلۡمَدِينَةِ تِسۡعَةُ رَهۡطٖ يُفۡسِدُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا يُصۡلِحُونَ
Na katika mji wa Ṣāliḥ, nao ni mji wa Ḥijr, ulioko Kaskazini magharibi ya bara Arabu, kulikuwa na wanaume tisa, shughuli yao ni kufanya uharibifu katika ardhi usiochanganyika na wema wowote wa kutengeneza.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالُواْ تَقَاسَمُواْ بِٱللَّهِ لَنُبَيِّتَنَّهُۥ وَأَهۡلَهُۥ ثُمَّ لَنَقُولَنَّ لِوَلِيِّهِۦ مَا شَهِدۡنَا مَهۡلِكَ أَهۡلِهِۦ وَإِنَّا لَصَٰدِقُونَ
Watu tisa hawa wakaambiana wao kwa wao, «Apianeni kwa Mwenyezi Mungu, kila mmoja awaapie wengine:’Tunaapa tutamjia Ṣāliḥ kwa ghafla, kipindi cha usiku, tumuue yeye na tuwaue watu wake kisha tutamuambia atakayesimama kutaka kisasi cha damu yake miongoni mwa jamaa zake: ‘Hatukushuhudia kuuawa kwao.’ Na sisi tutakuwa ni wakweli kwa tuliyoyasema.»
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَمَكَرُواْ مَكۡرٗا وَمَكَرۡنَا مَكۡرٗا وَهُمۡ لَا يَشۡعُرُونَ
Basi wakazipanga hila hizi za kumuangamiza Ṣāliḥ na watu wake kwa kuwafanyia vitimbi, tukamuokoa Nabii wetu Ṣāliḥ, amani imshukie, na tukawapatiliza kwa mateso kwa ghafla na hali wao hawatazamii vitimbi vyetu kwao kama malipo ya vitimbi vyao.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَٱنظُرۡ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ مَكۡرِهِمۡ أَنَّا دَمَّرۡنَٰهُمۡ وَقَوۡمَهُمۡ أَجۡمَعِينَ
Basi tazama , ewe Mtume, mtazamo wa mazingatio, mwisho wa njama za ukatili za kundi hili kumfanyia Nabii wao Ṣāliḥ. Sisi tuliwaangamiza wao na watu wao wote.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَتِلۡكَ بُيُوتُهُمۡ خَاوِيَةَۢ بِمَا ظَلَمُوٓاْۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لِّقَوۡمٖ يَعۡلَمُونَ
Hayo ni makazi yao, yako matupu, hakuna yoyote ndani yake. Mwenyezi Mungu Amewaangamiza kwa sababu ya wao kuzidhulumu nafsi zao kwa ushirikina na kumkanusha Nabii wao. Kwa kweli, katika uvunjaji huo na uangamizaji pana mawaidha kwa watu wanaokijua kile tulichowafanya. Na huu ndio mwendo wetu kwa wenye kuwakanusha Mitume.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَأَنجَيۡنَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَكَانُواْ يَتَّقُونَ
Na tukamuokoa, na yale maangamivu yaliyowafika kina Thamūd, Ṣāliḥ na waliomuamini waliokuwa wakijikinga, kwa Imani yao, na adhabu ya Mwenyezi Mungu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَلُوطًا إِذۡ قَالَ لِقَوۡمِهِۦٓ أَتَأۡتُونَ ٱلۡفَٰحِشَةَ وَأَنتُمۡ تُبۡصِرُونَ
Na mkumbuke na umtaje Lūṭ, aliposema kuwaambia watu wake, «Hivi nyinyi mnaleta kitendo ambacho ni upeo wa ubaya, nanyi mnajua ubaya wake?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَئِنَّكُمۡ لَتَأۡتُونَ ٱلرِّجَالَ شَهۡوَةٗ مِّن دُونِ ٱلنِّسَآءِۚ بَلۡ أَنتُمۡ قَوۡمٞ تَجۡهَلُونَ
Hivi nyinyi mnawajia wanaume kwenye tupu zao za nyuma kwa matamanio badala ya wanawake? Bali nyinyi ni watu msiojua haki ya Mwenyezi Mungu juu yenu, ndipo mkaenda kinyume na amri Yake na mkamuasi Mtume Wake kwa kitendo chenu kibaya ambacho hakuwatangulia nacho yoyote katika viumbe.»
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
 
പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: ന്നംല്
സൂറത്തുകളുടെ സൂചിക പേജ് നമ്പർ
 
വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്. - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക

ഡോ. അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് അബൂബക്കർ & ശൈഖ് നാസ്വിർ ഖമീസ്

അടക്കുക