Check out the new design

വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - റുവ്വാദ് വിവർത്തന കേന്ദ്രം * - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക


പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: ത്തൂർ   ആയത്ത്:

At-Tur

وَٱلطُّورِ
Ninaapa kwa mlima wa T'ur.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَكِتَٰبٖ مَّسۡطُورٖ
Na Kitabu kilichoandikwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فِي رَقّٖ مَّنشُورٖ
Katika ngozi iliyokunjuliwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَٱلۡبَيۡتِ ٱلۡمَعۡمُورِ
Na kwa Nyumba iliyojengwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَٱلسَّقۡفِ ٱلۡمَرۡفُوعِ
Na kwa dari iliyonyanyuliwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَٱلۡبَحۡرِ ٱلۡمَسۡجُورِ
Na kwa bahari iliyojazwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَٰقِعٞ
Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
مَّا لَهُۥ مِن دَافِعٖ
Hapana wa kuizuia.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
يَوۡمَ تَمُورُ ٱلسَّمَآءُ مَوۡرٗا
Siku zitakapotikisika mbingu kwa mtikiso.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَتَسِيرُ ٱلۡجِبَالُ سَيۡرٗا
Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَوَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Basi ole wao siku hiyo hao wanaokadhibisha.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي خَوۡضٖ يَلۡعَبُونَ
Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
يَوۡمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا
Siku watakaposukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
هَٰذِهِ ٱلنَّارُ ٱلَّتِي كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ
(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mliokuwa mkiukadhibisha!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَفَسِحۡرٌ هَٰذَآ أَمۡ أَنتُمۡ لَا تُبۡصِرُونَ
Je, huu ni uchawi, au hamwoni tu?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ٱصۡلَوۡهَا فَٱصۡبِرُوٓاْ أَوۡ لَا تَصۡبِرُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡكُمۡۖ إِنَّمَا تُجۡزَوۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyokuwa mkiyatenda.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّٰتٖ وَنَعِيمٖ
Hakika wacha Mungu watakuwa katika Mabustani na neema.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَٰكِهِينَ بِمَآ ءَاتَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ وَوَقَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ عَذَابَ ٱلۡجَحِيمِ
Wakifurahi kwa yale aliyowapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyokuwa mkiyatenda.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ سُرُرٖ مَّصۡفُوفَةٖۖ وَزَوَّجۡنَٰهُم بِحُورٍ عِينٖ
Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyopangwa kwa safu. Na tutawaoza mahurulaini.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَٱتَّبَعَتۡهُمۡ ذُرِّيَّتُهُم بِإِيمَٰنٍ أَلۡحَقۡنَا بِهِمۡ ذُرِّيَّتَهُمۡ وَمَآ أَلَتۡنَٰهُم مِّنۡ عَمَلِهِم مِّن شَيۡءٖۚ كُلُّ ٱمۡرِيِٕۭ بِمَا كَسَبَ رَهِينٞ
Na wale walioamini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani, tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alichokichuma.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَأَمۡدَدۡنَٰهُم بِفَٰكِهَةٖ وَلَحۡمٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ
Na tutawapa matunda, na nyama kama watakavyopenda.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
يَتَنَٰزَعُونَ فِيهَا كَأۡسٗا لَّا لَغۡوٞ فِيهَا وَلَا تَأۡثِيمٞ
Watapeana humo bilauri zisizo na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
۞ وَيَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ غِلۡمَانٞ لَّهُمۡ كَأَنَّهُمۡ لُؤۡلُؤٞ مَّكۡنُونٞ
Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ
Wataelekeana wakiulizana.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالُوٓاْ إِنَّا كُنَّا قَبۡلُ فِيٓ أَهۡلِنَا مُشۡفِقِينَ
Waseme: Hakika tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa mno.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَمَنَّ ٱللَّهُ عَلَيۡنَا وَوَقَىٰنَا عَذَابَ ٱلسَّمُومِ
Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda mbali adhabu ya upepo wa Moto.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّا كُنَّا مِن قَبۡلُ نَدۡعُوهُۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡبَرُّ ٱلرَّحِيمُ
Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwingi wa kurehemu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَذَكِّرۡ فَمَآ أَنتَ بِنِعۡمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٖ وَلَا مَجۡنُونٍ
Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ يَقُولُونَ شَاعِرٞ نَّتَرَبَّصُ بِهِۦ رَيۡبَ ٱلۡمَنُونِ
Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قُلۡ تَرَبَّصُواْ فَإِنِّي مَعَكُم مِّنَ ٱلۡمُتَرَبِّصِينَ
Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ تَأۡمُرُهُمۡ أَحۡلَٰمُهُم بِهَٰذَآۚ أَمۡ هُمۡ قَوۡمٞ طَاغُونَ
Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ يَقُولُونَ تَقَوَّلَهُۥۚ بَل لَّا يُؤۡمِنُونَ
Au ndiyo wanasema: 'Ameitunga hii!' Bali basi tu hawaamini!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَلۡيَأۡتُواْ بِحَدِيثٖ مِّثۡلِهِۦٓ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ
Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ خُلِقُواْ مِنۡ غَيۡرِ شَيۡءٍ أَمۡ هُمُ ٱلۡخَٰلِقُونَ
Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ خَلَقُواْ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَۚ بَل لَّا يُوقِنُونَ
Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana yakini.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ عِندَهُمۡ خَزَآئِنُ رَبِّكَ أَمۡ هُمُ ٱلۡمُصَۜيۡطِرُونَ
Au wanazo hazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ لَهُمۡ سُلَّمٞ يَسۡتَمِعُونَ فِيهِۖ فَلۡيَأۡتِ مُسۡتَمِعُهُم بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٍ
Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja iliyo wazi!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ لَهُ ٱلۡبَنَٰتُ وَلَكُمُ ٱلۡبَنُونَ
Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ أَجۡرٗا فَهُم مِّن مَّغۡرَمٖ مُّثۡقَلُونَ
Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ عِندَهُمُ ٱلۡغَيۡبُ فَهُمۡ يَكۡتُبُونَ
Au wanayo elimu ya ghaibu, nao wameandika?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ يُرِيدُونَ كَيۡدٗاۖ فَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ هُمُ ٱلۡمَكِيدُونَ
Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao waliokufuru ndio watakaotegeka.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ لَهُمۡ إِلَٰهٌ غَيۡرُ ٱللَّهِۚ سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يُشۡرِكُونَ
Au wanaye mungu asiyekuwa Mwenyezi Mungu? Ametaksika Mwenyezi Mungu mbali na hao wanaowashirikisha naye.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِن يَرَوۡاْ كِسۡفٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ سَاقِطٗا يَقُولُواْ سَحَابٞ مَّرۡكُومٞ
Na hata wangeona pande linatoka mbinguni linaanguka wangesema: Ni mawingu yaliyobebana.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَذَرۡهُمۡ حَتَّىٰ يُلَٰقُواْ يَوۡمَهُمُ ٱلَّذِي فِيهِ يُصۡعَقُونَ
Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapohilikishwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
يَوۡمَ لَا يُغۡنِي عَنۡهُمۡ كَيۡدُهُمۡ شَيۡـٔٗا وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ
Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُواْ عَذَابٗا دُونَ ذَٰلِكَ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ
Na hakika wale waliodhulumu watapata adhabu nyingine isiyokuwa hii, lakini wengi wao hawajui.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعۡيُنِنَاۖ وَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ
Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu,
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَمِنَ ٱلَّيۡلِ فَسَبِّحۡهُ وَإِدۡبَٰرَ ٱلنُّجُومِ
Na usiku pia mtakase, na zinapokuchwa nyota.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
 
പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: ത്തൂർ
സൂറത്തുകളുടെ സൂചിക പേജ് നമ്പർ
 
വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - റുവ്വാദ് വിവർത്തന കേന്ദ്രം - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക

റബ്‌വ ഇസ്‌ലാമിക് ദഅ്'വാ ആൻഡ് ഗൈഡൻസ് സെൻററിൻ്റെയും കോൺടെന്റ് ഇൻ ലാംഗ്വേജസ് സർവീസ് അസോസിയേഷൻ്റെയും സഹകരണത്തോടെ മർകസ് റുവാദ് തർജമ വിഭാഗം വിവർത്തനം ചെയ്തതാണ്.

അടക്കുക